Moto waunguza eneo soko la samaki feri

Moto waunguza eneo soko la samaki feri

jmnamba

Senior Member
Joined
Mar 31, 2012
Posts
156
Reaction score
28
Ajali ya moto imetokea leo soko la samaki feri, umeteketeza upande ama mabanda kadhaa!

Wananchi wamejitahidi kuuzima ingawa inasemakana ukoaji wa mali haukufanikiwa sana.

Kikosi cha zima moto toka bandari na askari wa FFU walifika eneo husika baadae kidogo.
 
Maskini weee sasa mkulu si amepata moshi kidogo? poleni sana
 
Pole kwa wafanya biashara.

Si juzi tu walikuwa wanajibizana wizara na manispaa???:shut-mouth:
 
dah nawahurumia wafanyabiashara waliopoteza mali zao...kwani ule mgogoro kati ya manispaa ya ilala na jiji uliishia wapi...?
 
hii sredi ni ya lini maana nimetoka hapo feri saa hii hii kula mikiya ya pweza na moto niliuona ni majiko tu
 
Naomba watoe 'source' ya habari hii au watuoneshe picha za tukio ili tupate uhakika wa jambo hilo kutoka katika eneo hilo la tukio.:A S 39:
 
natamani huo moto ungesogea kwenye ile nyumba yetu tuliyompangisha mchekeshaji
 
Back
Top Bottom