Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,557
- 21,512
Morogoro wamegoma kufanya kazi kwa zaidi ya saa nne wakishinikiza kulipwa mishahara yao huku baadhi yao zaidi ya 500 wa idara ya ushonaji wakigoma kwa zaidi ya saa sita wakishinikiza kuondolewa mkuu wa idara hiyo aliyefahamika kwa jina moja la crishna wakidai kuwa pamoja na manyanyaso mengi anayowafanyia amekuwa akiwakata mishahara yao bila utaratibu huku wakilalamikia kulipwa mshahara ndogo wa shilingi laki moja tu kwa mwezi.
Ni sauti za wafanyakazi wa kiwanda hicho waliogoma kushinikiza uongozi wa kiwanda kutimiza mahitaji yao ambapo pamoja na kero nyingi walizonazo wameiomba serikali kuingilia kati ili waweze kufanya kazi kwa amani.
Hata hivyo wafanyakazi hao wanatupia lawama uongozi wa kiwanda kuwa na tabia ya kuwafukuza wafanyakazi wanao onekana kuwa mbele kudai haki zao.
ITV