GE2025 Monalisa wa ACT Wazalendo anapinga Mpina Kugombea Urais, ahoji 'Kwanini anavaa T-shirt yenye picha ya Magufuli?

GE2025 Monalisa wa ACT Wazalendo anapinga Mpina Kugombea Urais, ahoji 'Kwanini anavaa T-shirt yenye picha ya Magufuli?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,777
Monalisa Joseph Ndala, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa ACT-Wazalendo Dar es Salaam, anazimwaga lawama za kutosha kwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama chao Luhaga Mpina kwa kusema yeye kama mgombea hakupaswa kuvaa nguo yenye picha ya aliyekuwa kiongozi kwenye chama kingine. Kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel yetu ya EastAfricaRadio


 
Luhaga Mpina bado ana maluweluwe/mawenge.Bado hajaamini katika kuamini anapoamini.The day-dreamer!
 
Luhaga Mpina anatumia njia kama ile ya Edward Lowassa ya mwaka 2015! Yaani hana mapenzi yoyote yale na ACT Wazalendo! Na jambo hili ni vizuri mkalifahamu mapema. Luhaga Mpina amejiunga na ACT kwa lengo la kupoza tu machungu, ila baadaye uchungu wa kukatwa jina ukipoa, atarejea tena ccm.

Tofauti yake na Lowassa ni moja tu! Mwenzake alikuwa ana nguvu na ushawishi mkubwa ndani ya chama! Na haikishanhsza CHADEMA kupata zaidi ya wabunge 75 kwenye ule uchaguzi! Ila mwisho wa siku wengi wa hao wabunge waliishia tu kununuliwa na ccm, kwa kisingizio cha kuunga mkono juhudi.
 
Kwa hio yeye ana Chuki za Waziwazi na Magufuli alitaka avae picha za Sa100 si ndio?
 
Jamaa anagombea Urais ila ndani ya Chama anachogombea kuna wanaomchukia vibaya sana na kuona kwamba hakutakiwa yeye kugombea Urais kwa sababu walishajipanga na kale kamama wakitegemea kwamba kale kamama katashinda uchaguzi wewe kiongozi hata kusoma tu speech ni mtihani kuzungumza mbele ya watu kisanga ushinde Urais nani kasema?
 
Ana hoja, asikilize.

Kama lengo ni kuwaenzi viongozi, kwann hajavaa t-shirt yenye picha ya Maalim Seif?
 
Amevaa picha ya Magufuli kama short cut ya kuitafutia kura na famousity ACT bila kutumia nguvu nyingi maeneo ya huko kwao ambayo Yeye na Magufuli wanatokea huko.

It's cleverly a political gear, japo ina ukanda lakini inaweza kuleta better results kuliko asipofanya hivyo...

Kwasababu Kule ACT WAZALENDO haina Mvuto...haijulikani....nobody know it....ipoipo tu.
ACT is deeply rooted only in Zanzibar.
Sasa yeye ni kama anajaribu ku-replace kivuli cha Magufuli kwenye siasa za huko kwa Interest ya ACT na yeye binafsi...
Undoubtedly atakuwa alikuwa vijijini.
Yule ni mtu mzima, naye anajua fika hawezi kushinda.
 
Back
Top Bottom