GE2025 Monalisa wa ACT Wazalendo aandika barua kwa Msajili wa Vyama Vya Siasa kupinga Luhaga Mpina kuteuliwa kama mgombea Urais

GE2025 Monalisa wa ACT Wazalendo aandika barua kwa Msajili wa Vyama Vya Siasa kupinga Luhaga Mpina kuteuliwa kama mgombea Urais

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

McLaren

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2025
Posts
889
Reaction score
2,863
Katibu mwenezi ACT Wazalendo mkoa wa Dar es salaam Monalisa Ndala leo Agosti 19, 2025 ameandika Barua kwa Msajili wa vyama vya Siasa Nchini kama mlezi wa vyama vya siasa.

Hiyo ni hatua ya pili mara baada ya mara ya kwanza kuandika Barua kwa Katibu wa Chama Cha ACT wazelendo, Kupinga Mhe. Luhaga Mpina kuwa mgombea Urais mwakilishi kutoka ACT Wazalendo kwenye uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025.

“Leo nimechukua hatua ya pili ya kukitetea chama changu kwa kumuandikia barua Msajili wa vyama vya siasa nchini kama mlezi wa vyama hivi ili kuingilia kati uvunjifu wa wazi wa kanuni zetu za uendeshaji wa chama za mwaka 2015”. - ameandika Monalisa Ndala Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii

ACT.png


Uamzi wa Msajili, soma GE2025 - Msajili wa Vyama vya Siasa: Uteuzi wa Luhaga Mpina ni batili kisheria, hastahili kuwa Mgombea Urais kupitia ACT
 
Huyo Monalisa anataka kuharibu mchezo wa kuigiza kati ya CCM na ACT kuwazubaisha watu.Watamuua shauri yake.
 
Na msajili ata-react kwa speed ya 3×10ⁿm/s where n=8!

BTW:Achukue fomu ya ubunge tu kama yupo ndani ya muda asiwaponze wenzie wazuiwe kufanya shughuli za siasa yenyewe!
 
Ukitaka kuishi vizuri usiwe na ukaribu na masikini sana, mtu mwenye ndoto ya kuwa tajir sana na mwanasiasa




Fullstop, kwishaaaaaaa
 
Watu wameshauri, hamtaki sikia , ngoja tuelekee msalaba wa haki , tuone nani mkuu kati ya Mungu na binadamu, binfsi nitaenda huko juu ,mlima Kilimanjaro nimepewa heavy task na Mungu wangu , na nimejiandaa kwa lolote kunzia familia yangu ya baba na mama ,mke na watoto wangu, nahitaji maombi ya kila mmoja mpenda haki , sio kazi nyepesi ila katika Bwana kila jambo linawezekana .
 
Back
Top Bottom