Ni chotara wa kiisraeli, na kwa kipindi kirefu amekuwa akishirikiana na wafanyabiashara wa Israeli katika utafiti wa mafuta na biashara za uchimbaji madini nchini humo. Kwa hiyo ana ushawishi kiasi fulani ukizingatia siasa za Kongo zinavyokwenda, ambapo hata rais aliyepo madarakani kuna madai ya kuwa ni pandikizi kutoka nchi jirani.
Baada ya kupinduliwa Laurent Kabila, kwa nafasi kubwa serikali ya Kongo inaongozwa na raia wa kigeni kuanzia ikulu hadi kwenye majimbo. Mwanasiasa aliyekuwa na harakati za kuirudisha Kongo kwa wakongomani alikuwa ni Jean-Pierre Pemba, ambaye amefungiwa na mahakama ya ICC kushiriki siasa za Kongo.