mfianchi
Platinum Member
- Jul 1, 2009
- 11,855
- 8,253
Kukua kwa teknolojia siku hizi kumerahisisha mambo mengi,moja wapo la hayo mambo ni uwekaji au uhamishaji wa fedha kwa kutumia kampuni zitoazo huduma za simu za mkononi,lakini kila jambo zuri lisipokuwa na uangalizi hatimaya yake ni kuwa kama DECI,karibu kampuni zote kubwa za huduma za simu za mkononi hufanya shughuli za kuhamisha au kuhifadhi fedha,mamilioni ya shilingi hupita katika hayo makampuni kila siku,tatizo langu ni kuwa je hizo shughuli zina sheria yoyote inayoziendesha kwani nilitegemea benki kuu kuwa msimamizi wa hizo shughuli za mamilioni ya pesa yanayopita nje ya utaratibu wa sheria za fedha,na je pale kampuni ya simu ikafilisika au ikafungasha virago je watu walioweka pesa zao watazipata wapi?na wataenda kudai wapi.Maoni yangu ni kuwa benki kuu iiweka utaratibu utakaofuatwa na kampuni zote,kwa benki kuu kukaa kimya na kujifanya hamnazo ni kukaribisha DECI mpya,au mpaka watu waje lizwandio benki kuu itatoka usingizini?