MO na Halima Mdee, patachimbika Jimbo la Kawe!

MO na Halima Mdee, patachimbika Jimbo la Kawe!

alexelias

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2017
Posts
2,032
Reaction score
3,198
Kuna kila dalili mfanyabiashara mkubwa na kada wa CCM ndugu Mohammed Dewji almaarufu 'Mo' atagombea Jimbo la Kawe katika uchaguzi ujao wa 2020.

Inasemekana CCM inamshawishi MO ili akubali kuwa mshindani wa Halima Mdee kwenye Jimbo hilo mwakani.

Mytake;Ufalme wa Halima unaenda kukoma rasmi kwa mwamba huo wa CCM endapo tu utakubali kugombea Jimbo la Kawe.
 
Mo asikubali tena kurudi kwenye Siasa hata kama atashawishiwa NA watawala. Nashauri asikubali kabisa kuingia kwenye Siasa, ajitahidi sana kuzikwepa Siasa NA wanasiasa. Ajiweke kando NA wanasiasa kama alivyo Mzee Bakhressa.

Amuulize Mzee Bakhressa nini kilimkuta mwaka 1995 baada ya yeye kujiingiza kwenye siasa chafu za Tz! Asikubali kugombea tena ubunge wala kujihusisha na siasa kWA namna yoyote ile.
 
Ameshauriwa na nani au amelazimishwa?!

#BringBackMo sasa imeleta maana?!
 
Mkuu acha ramli chonganishi
Mkuu,hiyo nimekupa ya ndani kabisa!

Ilikuwa Makonda akapambane naye lakini imeonekana Boniphace kule Ubungo lazima awepo mtu jembe wa kupambana naye ndiposa CCM kimeonelea Makonda abaki Ubungo kummaliza Bon na Mo akammalize Halima.


Mo anapelekwa pale kwa ajili ya jambo moja tu kummaliza Halima.
 
- KumbukiziMTAFUTANO.jpg


Mo hajasahau huu unyama aliofanyiwa
 
Kwa kusema ukweli bila kumung`unya maneno Halima mdee kupita uchaguzi ujao jimbo la kawe itakuwa ni muujiza wa karne,jimbo halina jipya,barabara zilikuwa hazipitiki mpaka walipokuja makonda na Meya Sita wakaahidi ndipo baada ya miezi michache barabara zikaanza kutengenezwa.Simlaumu Halima Mdee haya ni matokeo ya Siasa za Tanzania ukiwa mbunge wa jimbo halafu unatoka upinzani sahau kupata maendeleo jimboni kwako.
 
Back
Top Bottom