Mnyonge Mnyongeni Haki Yake Mpeni: Serikali ya Rais Magufuli Inajitahidi sana kwenye Suala la Miundombinu Hasa Barabara.

Louis II

JF-Expert Member
Mar 9, 2018
3,030
4,645
Assalaam Aleiqum wapendwa,

Niwe muwazi tu kwamba, miye si mpenzi/mfuasi wa siasa za Rais J.P Magufuli kwani kila mtu anafahamu hali halisi ya kisiasa ilivyo kwa sasa hapa nchini kwetu.

Chini ya uongozi wa rais JPM, hali ya kisiasa imekuwa mbaya hasa kwa upande wa upinzani kwani wanachukuliwa (considered) kama Wahaini (wanatumwa na mabeberu). Chini ya utawala wa Awamu ya tano, weaknesses zimekuwa nyingi na zimekuwa kama wimbo wa taifa maana zipo kila uchwao na hakuna Positive solution/action/change yoyote Inayochukuliwa. Kifupi sitataja madhaifu yote ya awamu hii ya tano Katika utawala wake kwa sababu mengi yanajulikana na yanasemwa kila siku humu na huko uraiani kuhusu "Tyrannic leadership" ya Mh. JPM.

Lakini Kama tittle ya Uzi hapo juu inavyojieleza "Mnyonge Mnyongeni Haki yake mpeni", kwa kweli Serikali hii kwenye suala la miundombinu hasa ya barabara imejitahidi sana kuboresha na kuzitengeneza kwa wingi hasa katika maeneo yaliyokuwa yamesahaulika hapo mwanzo. Mfano mzuri kwa hapa Dar ES Salaam, ni Wilaya Za Temeke na Ilala ukijumuisha viunga vyao, kumekuwa na utengenezwaji na uboreshaji wa barabara hasa zile ambazo zilikuwa kero kwa watumiaji kipindi cha Mvua na maeneo mengi yanapitishiwa barabara za lami.

Ushauri: Serikali ya awamu ya tano imefanya mambo mengi Mazuri ambayo Hayatasahaulika vizazi kwa vizazi mf. SGR, Stiglers Gorge, Kununua ndege n.k. lakini yapaswa Kufanya marekebisho kwenye baadhi ya mapungufu yake ambayo yamekuwa yakiimbwa na Watu wa kaliba zote kila uchwao....Nina imani, serikali hii itakuwa bora zaidi iwapo itafuata utawala Wa sheria unaozingatia maslahi ya taifa kwa manufaa ya jamii yake Kiuchumi, Kisiasa, Kijamii, Kiitikadi, na Kifikra. Wahaddha Assalaam Aleiqum!

Louis II
 
Serious?! Hivi miradi mingi ya barabara si ya tangu ya awamu ya 4?! Hivi kabisa unasifia kwamba anafanya vizuri kwenye barabara kwa kutaja barabara za Dar es salaam za kilometa 1-5?! Hivi wakati Magufuli anatamba watu kuweza kusafiri kutoka Mtwara hadi Bukoba kwa taxi ilikuwa ni awamu hii au awamu iliyopita?!

Btw, kwa mtu kama mimi wa Temeke utanitajia barabara ipi kwa mfano?!

Barabara ya Mbagala-Tandika kupitia stendi ya Shamba imejengwa awamu ya 5?

Barabara ya Kabuma imejengwa awamu ya 5?

Barabara ya Tandika - Buza imejengwa awamu ya 5?

Kilwa Rd yenyewe imejengwa awamu ya 5?

Kabaraba ka Mtoni Madafu kamejengwa awamu ya 5?

Barabara ya kutoka Kilwa Rd to Kurasini Highway imejengwa awamu ya tano?!

Barabara ya Mwembe Yanga - Tandika imejengwa awamu ya 5?!

Barabara ya Rangi 3 kuelekea Charambe na yenyewe imejengwa awamu ya 5?

Barabara zipi hasa unazozisema wewe?

Au unazungumzia barabara inayotoka Kijichi CCM kwenda kule Kota za Bank?
 
Mimi kiufupi sijawahi ona kitu chochote cha serious jiwe anachofanya, labda kuangamiza wapinzani wake


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ukitaka ujue uhai wa nchi tembea vijijini.

Acheni porojo, hayo mabarabara ya Dar hayawakilishi maendeleo ya Tanzania nzima.
 
Ukitaka ujue uhai wa nchi tembea vijijini.

Acheni porojo, hayo mabarabara ya Dar hayawakilishi maendeleo ya Tanzania nzima.

Mkuu huyu tunamkaribisha njia ya kuelekea kwetu Ngara njia kuu kwenda Burundi na Rwanda. Tokea nyakanazi wilaya ya biharamulo akifika huko ataomba mods waufute huu uzi. Hasa hasa akifahamu kuwa barabara hii imekuwa hivi kwa miaka lukuki na kila siku ni mbaya kuliko jana yake.
 
Back
Top Bottom