Mnyika - tatizo la maji sasa lipo shingoni.

Mnyika - tatizo la maji sasa lipo shingoni.

BABA E's

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
354
Reaction score
136
Sisi tunaoishi maeneo ya kimara hali sasa imeshakuwa mbaya sana. Ipo siku tutakapoona gari la Dawasco linapita tutachoma Moto. Hivi kama kweli kuna shida mahali ni kitu gani kinashindikana kutoa taarifa zinazoeleweka kwa wananchi. Kila mtu anajua maji ni kila kitu. Tumekuwa tukiuziwa maji ya chumvi ambayo nayo pia yanapatikana kwa shida na hata hatujui yanatoka wapi, sijui kwa mwarabu, huyu jamaa akiamua kutumaliza si tutakwisha wote. Kama kweli kuna tatizo mahali hasa linalochukua muda mrefu kwanini serikali isitafute njia mbadala ya kusaidia watu wanaoishi maeneo hayo!!. Ni kwamba huku hakuna viongozi wanaona hili. Haiwezekani watu hampati maji miezi miwili halafu mtu aseme eti wanatengeneza mitambo au njia za maji kwa muda wote huo. hii haiingii akilini.

Zimeni huo umeme wenu hatuutaki tupeni Maji.
 
Sisi tunaoishi maeneo ya kimara hali sasa imeshakuwa mbaya sana. Ipo siku tutakapoona gari la Dawasco linapita tutachoma Moto. Hivi kama kweli kuna shida mahali ni kitu gani kinashindikana kutoa taarifa zinazoeleweka kwa wananchi. Kila mtu anajua maji ni kila kitu. Tumekuwa tukiuziwa maji ya chumvi ambayo nayo pia yanapatikana kwa shida na hata hatujui yanatoka wapi, sijui kwa mwarabu, huyu jamaa akiamua kutumaliza si tutakwisha wote. Kama kweli kuna tatizo mahali hasa linalochukua muda mrefu kwanini serikali isitafute njia mbadala ya kusaidia watu wanaoishi maeneo hayo!!. Ni kwamba huku hakuna viongozi wanaona hili. Haiwezekani watu hampati maji miezi miwili halafu mtu aseme eti wanatengeneza mitambo au njia za maji kwa muda wote huo. hii haiingii akilini.

Zimeni huo umeme wenu hatuutaki tupeni Maji.
Fanyeni kama walivyofanya wale wa Ntwara... 'Gesi haitoki' iwe 'Maji hayapiti' nakuhakikishia mtapata hadi ya kumwagilizia nyasi..
 
Wizara ya maji ipo hapo ubungo kwanini wakazi wa kimara msiende hapo mkawashinikiza hao wa watendaji wa wizara? Mh. Mnyika anajitahidi hata bungeni wakati wa bajeti ya wizara ya maji alimbana waziri lakni bajeti ilipita.
 
Sisi huku kwa raha zetu saa24 nashindwa kuelewa hivi nikweli mnadhiki na maji kiasi hicho pole sana
 
Wizara ya maji ipo hapo ubungo kwanini wakazi wa kimara msiende hapo mkawashinikiza hao wa watendaji wa wizara? Mh. Mnyika anajitahidi hata bungeni wakati wa bajeti ya wizara ya maji alimbana waziri lakni bajeti ilipita.
Bomba la maji linapita kimara... sijui kwa nini hawa watu hawapigi hata MKWARA kidogo tu ili wapate maji?
 
Leta nguo uje kufulia huku kwetu, maji 24/7
 
Bomba kuu la maji liendalo mjini linapita Kibamba,Mbezi Kimara,Tabata na Ubungo ambamo kote humo ni jimbo la Mnyika. Yet shida ya maji humo mote na mitaa yake ni kubwa sana,watu wanachota mpaka maji ya mifereji,chemchem na madimbwi!. Wizara ya maji ipo jimboni kwa Mnyika,yet wameziba macho na masikio. Mnyika isulubu hiyo wizara ili upone. Usipoisuluaju 2015 utakua na uphill task!
 
Chadema haifai tuitoe tu, mbona tunajuta.

Yaan naona ulichosema ni jambo la maana mkuu maana kuna vitu vingine mbunge haitaji support ya serikali zaid angeitisha mkutano.wa dharura na kuchimba mifumo ya maji na kutandaza bomba kwa kutushirikisha wananch, hata.hk kdg kinawashinda?? Maji yalikua yanaishia sehemu.moja wanaita vinane, kwingine wanadai.hayana pressure kwa nini asiitishe mkutano tuweke harambee tununue pump??mnyika ana maeneo ambayo anayapigania huku.kimara bonyokwa hali ni mbaya sana bara bara ndo usiombe kila week tunaenda service inauma sana kwa kwel hiz siasa bana?? Mnyika alitaka kupitisha kibubu kupata 1m ktk blog kwa nn asiengeitisha mkutano?? Nasikia manispaa ukipeleka laki tatu wanachonga 1m ya nini?? Tuchukue hatua 2015 c mbali.tufanya maamuz sahihi na c ya kishabiki!!
 
Dawa ni kuhakikisha mnyika hapati tena ubunge 2015 sababu toka aingie hamna alichokifanya zaidi ya kupiga blah blah
 
Dawa ni kuhakikisha mnyika hapati tena ubunge 2015 sababu toka aingie hamna alichokifanya zaidi ya kupiga blah blah
Mnyika angekuwa anapiga kelele za tatizo la maji kama afanyavyo kwenye shughuli za chama, wakazi wa jimbo lake wasingelalamika hivi, na mnyika akicheza tu 2015 watamuondoa kutokana na tatizo la maji.
 
mbunge kazi yake nikuishauri serikali na kutunga sheria kazi yakuleta maji ni ya serikali so ilaumuni serikali ya ccm bwana na muihukumu 2014 na 2015
 
mbunge kazi yake nikuishauri serikali na kutunga sheria kazi yakuleta maji ni ya serikali so ilaumuni serikali ya ccm bwana na muihukumu 2014 na 2015

Tatizo la mnyika ana maeneo anawapa kipaumbele km mabibo, ubungo na manzese, huku haji ana diwan wake anaitwa manota ndo kabisaa hana mpango makelele tu, tulianzisha ulinz shirikishi hatak tuchangie anasema ni serikali, hii serikal imetutelekeza yy angekaa na wananchi wa kimara na tukaweka mmpango mkakati, tusipopiga kelele hatusikilizwi, hk kwa wapiga kura had anasubir uchangu, mm binafsi cimp maana cjaona alichotufanyia, barabara mbovu, maji hakuna, ulinzi shirikishi hakuna, walianzisha kituo cha police hapa mavurunza kimetelekezwa alikuja na vuuai hapa wakatushika mikono na tukachangia kikafungea lenta mpaka leo, I hate siasa maana ni maneno matamu ila utekelezaji ni sifuri
 
Hao wa mtwara walipata walichotaka?

THE BIG SHOW alichezea kichapo cha haja. Kuna habari ambazo nusu zilithibutishwa kuwa wanajeshi walivamia nyumbani kwake wakafanya ubakaji. Baada ya hayo yote 'kamanda' akalazimika kuwa mpole. 'kaachia' kwa wanajeshi na kaachia gesi pia
 
Last edited by a moderator:
Wewe unadhani dar ndio ubungo? kuna sehemu hazina shida ya maji kama ilivyo ubungo.
Nimekwambia kama siyo tatizo la maji safi basi kutakuwa na tatizo la maji taka. Hilo ni tatizo dar nzima, si city center wala si Oysterbay. Chemba zinazovuja vinyesi ziko kila mahali... yule msanii aliyesema dar inanuka hakukosea.
 
Back
Top Bottom