Mkuu acha wivu utakufa kwa fedheha bure.
Wenzetu Chadema wanasonga mbele sisi CCM kutwa tunashinda hapa Lumumba kupika majungu tu na Propaganda za kitoto.
Ndugu yangu CCM kwa sasa katika mikoa ya Iringa, Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Dar ni kama imekufa kabisa wakati tuna viongozi na wanachama katika mikoa hiyo, nini tatizo hasa?
Amka sasa ndugu yangu ukafufue chama na sio kuropoka chuki tu mtandaoni.
Huyo Lukosi hana lolote la maana kwa CCM zaidi ya kutafuta dili za tender za kupiga. Infact kwa sasa anajuta kwa sababu ya kujidhalilisha na tender ya TBS kaikosa. Kwanza hakuhama CHADEMA bali alifukuzwa kwa aibu kutokana na tabia chafu ya kutaka kutumia chama kama mgongo wakutokea.
Eti kwa sasa anajipanga kugombea ubunge Iringa mjini kupitia CCM!!! Maajabu ya dunia, wakati kuna makada wa CCM kama 10 kwa sasa wamejipanga kimafia kupita kura za maoni, Lukosi anatoa mapovu tu humu JF.
Halafu hajui kabisa nguvu kubwa ya kisiasa aliyonao Pastor Msigwa pale Iringa kwa sasa.