Mkuu umenena. Watu wengine wanashabikia kitu hata hawakijui . A black boxayatoayo mtu ni yale yaliyoujaza moyo wake, ukiona mtu anaongelea mabwabwabwabwa ujue moyoni na kichwani mwake umejaa ubwabwa tu...wewe ni bwabwa mwenyewe, huna maana. ungekuwa mwanaume halisi ungeelewa nilichoandika. siwezi kubishana na mabwabwa. sisi tunaokaa huku ubungo ndio tunaoliona joto ya jiwe, na mbunge huyu hatusaidii chochote, wala sijawahi kuona ameongelea matatizo yetu bungeni, zaidi ya kuongelea matatizo ya cdm in general kitaifa etc. ndo maana nimemshauri awaige wenzie kina tundu lisu, pamoja na kwamba ni wapambanani, wanajali kwao kwa wale waliompa kura. haiji akilini kuona mabomba yapo hadi majumbani mwetu lakini hayatoi maji...unataka matatizo yetu tumwambie nani ili atuwakilishie kwenye selikali kuu yatatulike? si kila mwanachadema anafanya kazi, wengine wapo hapo na wavivu na hawana faida kwenye chama wala kwa wananchi, zaidi ya kufurahia marupurupu, hata yale ya maendeleo ya jimbo basi tuyaone kwenye jimbo letu. kama hujaelewa hadi hapo, rudi shule kaanze chekechea.
keenja alijitahidi sana kutengeneza barabara, hela kidogo tu inahitajika hata kama si lami, kujaza mashimo tu ya zile barabara. fika pale kimara mwisho, nyooke either kwenda bonyokwa au upande mwingine kwenda king'ong'o kwa komba utarushwarushwa na mashimo kama huna akili nzuri. pale inahitajika hata ile hela ya mfuko wa jimbo tu kujaza mashimo kusawazisha ili tuendeshe magari na pikipiki kwa starehe. yeye hajawahi hata kufika kule tangu achaguliwe, wa nini sasa? halafu anamwita jk dhaifu, yeye pia ni dhaifu zaidi wasichekane....pia, usiseme mimi ni ccm...mimi ni chadema kwa taarifa yako...lakini inaniuma sana kununua maji wakati niko karibu na Ruvu na maji ya bomba la mchina yameingia hadi kwenye nyumba yangu lakini hayatoi maji....mbunge yupoyupo tu. barabara kwenda home ina mashimo ajabu.....anatusaidia nini sasa huyu? hivi ninavyoongea ndivyo raia wa mtaani wanavyoongea.
serikari yako dhaifu ya CCM imekufanyia nini kabla ya mbunge Myika wa CDM
Mnyika ni mbunge wangu kule kimara. hajafanya lolote kwenye jimbo langu tangu achaguliwe. mimi nilikuwa mmoja wapo wa watu waliopigwa na mbu na baridi kulinda kura zake zisiibiwe na magamba. lakini sasaivi maji naagiza lori lije nipandishe kwenye tank kwa pesa yangu binafsi wakati mabomba ya mchina yametandikwa hadi kwenye nyumba yangu, maji hayatoki. mbunge huyu anatusaidia nini? MWAKE 2015 NITACHAGUA MBUNGE WA CHADEMA, lakini nataka wambadilishe aje mgombea mwingine wa chadema na si mnyika, kwasababu akigombe atena, wananchi ha huku hawataki hata kumsikia...wanaona bora hata keenja. magari yanaharibika kwasababu barabara mbaya mno mitaa ya kimara...hatujawahi kuona ameongelea hilo bungeni hata siku moja ili tujue kuwa basi amehangaika kidogo, anachofanya ni kupigania chama kitaifa na kututelekeza...sisi hatuli chadema pamoja na kwamban i wanachadema, tunahitaji utujali ili tuone uzuri wa chama. amini msiamini, kama mtu mwingine wa chadema hatagombea ubungo, basi jimbo linaweza kurudi kwa magamba au kwenda cuf pamoja na kwamba kimara na ubungo tumejaa WACHAGA.
Huku Ludewa tangu uhuru hatujaona lami. Maji tunachota mtoni. umeme tunauona hospitali tu tena mwish saa nne usiku. Lakini tuna mbunge naitwa Filikunjommbe na tunamkubali. Sasa ndugu yangu sijui unalalamikia nini. Hali ya maisha na huduma za jamii katika nchi hii haziwezi kuja kwa kufumba na kufumbua. Inahitajika mipango ya muda wa mfupi, wa kati na mrefu, kwa kuanzia na kubadili mind set zetu kuwa mbunge atajenga miundombinu as if ana source of fund yeye kama yeye. I am sure hata ungepewa ubunge wewe usingefanya hayo unayomlaumu Mnyika.
Kwa sasa inatakiwa tujenge system ya utawala bora na uwajibikaji kama taifa. Hii itazuia ufisadi/wizi wa fedha za umma na hivyo itawezekana kujenga miundombinu hiyo unayodai ni kero. Kwa sasa nchi hii ni kama gunia lililotoboka ndugu yangu. Hata kama Mnyika akitaka kujenga hiyo miundombinu ya kijamii wakati fedha nyingi inaibwa na nyingine kutoroshewa Ulaya itawezekana wapi jamani?