Natumain umzima na unaendelea vizuri na majukumu yakoo..mimi ni mpiga kura wangu kaka tena nilikuwa mbele kuona ukiingia madarakani lakini sasa mambo yamekuwa kinyume na sikuone tena huku jimboni kwako Maeneo ya manzese, kwamfuga mbwa na ukombozi....
Ukweli huku hali ni mbaya sana na hatuna pa kukimbilia, huduma ya maji ni kiama, miundo mbinu ni uchafu mtupu, takataka ndo usiseme spidi ya kukusanya hela ya taka ni kubwa kuliko huduma yake, barabara zimeekwa taa ila ziliwaka siku moja na nadhani zitawaka tena siku MH RAIS AKITEMBELEA MANZESE USIKU....! Yapo mengi ya kuongea na wewe kuhusu jimbo lako .........
WAKE UP GUY DON'T LET US DOWN
Hii kali sasa yaani kwa kuwa Mnyika ni Mbunge wenu mnataka mpaka taka awazolee Lol!!kweli Watanzani ani wavivu sana hata kufikiria pia mnakuwa wavivu hii ni hatari,Mijitaka mtupe wenyewe na wewe ukiwa mmoja wapo then Mbunge aje kwenye mkutano aongelee mambo ya usafi?Hivi wewe kama mwana Manzese ulifanya nini kwa mtaa wako au hata nyumba ya jirani zako kama tano tu,umewashauri vipi kuhusu utupaji wa takataka?Kuhusu maji hili ni la wote sio Mbunge tu kumbuka kilio cha wengi ni Sauti ya Mungu so komaeni nyie wote kwa usafi kwanza then Mbunge wenu anapambana na mambo ya maji.
Nini wasiwasi sana na wewe kaka kwani naona hata hufuatilii nchi yako inavyokwenda yaani umeshindwa hata kusikia kwa news au hata kufuaatili Bungeni ni juzi tu Mh Mnyika alikuwa anaongea habari za maji hususani Dar Es Salaam yote hata hili hujasikia mie niko mbali sana na home lakini nilisoma na nimesikia hata kupitia youtube nini kiliendelea Bungeni.Tusiwe wepesi wa kushabikia vitu ambavyo ni vya kusikia sikia tu kabla ya kusema au kuandika kitu jaribu kufuatilia kwanza.Kumbuka tu kama Dar Es Salaam yote itapata maji basi na Manzese basi yatapatikana kwa kuwa nayo iko Dar Es Salaam.