Mnyaa athibitisha kuwa CUF ni CCM B!

Mnyaa athibitisha kuwa CUF ni CCM B!

Habib Juma Mnyaa ninayemjua mimi ni Mhandisi (Engineer ) wa umeme. Nilimfahamu toka akiwa shirika la umeme Zanzibar (ZSTC) na baadae ofisi yake kama mkandarasi pale daraja bovu Zanzibar.

Kuna maana gani kumkutanisha Lawyer na Engineer katika suala la kisheria? Kwanini wasimchukue ismail Jussa kumkutanisha na Lissu kwani wote hawa ni fani moja.

Lakini pia Chadema lazima wakubali mawazo mgongano.Sio kila wanachosema au kuamua wao tu ni kweli na hawaruhusu watu wengine kupingana nao.Huo ni udikteta.



Umeianza vema hoja yako,lakini umaliziaji mmh... Kupingana juu ya kupata KATIBA halali ? kivipi mkuu wangu.
 
CUF na wananchi wa ZNZ watakapogundua kuwa nani aliyeingiza mambo ya 11 ya muungano kinyemela na kuifanya znz ikamezwa na TZ bara kama wanavyotaka tuamini basi hapo ndipo wataamka usingizini na kujua kuwa ile Damu ya wazanzibar waliofariki 2001 ilikuwa na thamani kuliko uroho wa madaraka walionao. Na ndipo watagundua kuwa mwaka 2010 walishinda uchaguzi Znz na CCM ilistahili kuwa chama cha upinzani Znz na ndio ilikuwa ndoto ya wale waliopoteza maisha 2001.

Lakini kwa kuwa ndoa ni tamu basi damu ile itaendelea kuwalaani na hadi hapo watakapo jitambua kuwa wanatumiwa kama mpira wa Kiume na CCM.

Wakati wabunge wa CUF wanapiga makelele kumsema T.Lisu na chadema kuwa hakiwatakii mema Znz na muungano lkn wamesahau kuwa mamilioni ya pesa yanatumika kujadili kero za muungano zisizo na utatuzi wa kudumu.
CUF wamesahau kuwa familia za waliopoteza maisha hazikupata msaada wowote toka serikalini Leo hii wanajiita wanamuafaka ambao ni upuuzi. Waznz lazima wajue kuwa CCM ndio tatizo na muafaka uliopo ni kiini macho ili waweze kupitisha madudu yao na ndio maana Sharifu Hamad hana maamuzi yoyote zaidi ya kukata tepe na kuliko makamu wa pili wa rais ndio maana nina wasiwasi Seif huenda alikula mlungula kabla ya kukubali.

Ukitaka kujua CUF inatekeleza sera za CCM ni hivi majuzi tu wananchi wa ZNZ wamefikia hatua ya kupeleka barua UN lkn wabunge wa CUF/CCM ZNZ hawaliona hilo zaidi ya kukumbatia muungano hivyo kupoteza uwakilishi wa nini watu wao wanataka na kujifanya wametuma maoni yao wakati wote tuliona kwenye TV walivyochana mswada ule sasa sijui lini walituma maoni. Ni wananchi wa znz hao hao walipinga rais wao kuapishwa kama waziri lakini sikulisikia hilo bungeni zaidi ya kutumiwa kutukana. Hivi mtu kama T.Lisu akisimama na kusema CUF wanachotaka ni madaraka na sio kusikiliza wananchi wanataka nini hivi kuna haja kweli ya kuwa na degree ya kuweza amini kuwa anachosema yuko sahihi?

Lakini kwakuwa wa ZNZ wamelishwa kitu kinachoitwa serikali ya umoja wa kitaifa basi chochote kile kisemwacho wao wanaona ni matusi kwao na kuona CCM sio tatizo kwao lkn ni hao hao CCM waliopora uhuru wao wa kuchagua kwa kumpachika rais asiyechaguliwa na wananchi na CUF wakakubali kwakuwa wanataka madaraka na hakika yale machozi waliolia baadhi ya wana Znz sio bure mungu atayasimamia na hakika CUF itaendelea kubaki kwenye laana hadi hapo watakapojitambua
 
Ndo tatizo la wapinzani wa bongo, badala ya kuungana _ _ _ kunyoosheana vidole.
 
Hivi angeiunga mkono chadema angekuwa chadema B? Ujinga huu wa kudhani kwamba wapinzani ni sharti wakubaliane kila kitu na wakosoe kila kitu cha chama tawala ni ujinga mkubwa. Ulitaka Mnyaa akubaliane na upotoshaji wanaoufanya akina Kitila Mkumbo ambao wanajadili hoja kwenye midahalo wakiwa ni viongozi wa chadema na wakizidiwa hoja wanaenda Chuo Kikuu na kutoa statements wakijiita ni viongozi wa UDASA. Unafiki mtupu!
Acha ulevi wewe!!!
mail
 
Back
Top Bottom