Mnaopinga lockdown kuna vitu mfikirie kwa mapana

ndio sababu tunawaita wanga,yaani kumbe umekaa unasubiri maambukizi na vifo viongezeke kwa namna isiyovumilika ili tu tufungiwe.useme"NILISEMAAA"ONA SASA KIKO WAPII!!!

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu mwanga ni wewe.

Akili yako haiwezi kuwa inafanya kazi vizuri kudhani janga hili litaondoka lenyewe.

Umeona kuna siku hali imekuwa nafuu tangu ugonjwa uingie?

Takwimu zinaonyesha kwa ujinga wetu ikiwamo kuendekeza maombi (mods wamefuta uzi wangu kuhusiana na issue ya maombezi) badala ya kupambana, hali ya ugonjwa itakuwa mbaya zaidi.

Pana wana maombi waliwahi fika JKNIA kusafiri kwa ndege bila ticket wala viza kwenda USA miaka ya nyuma. Kwao biblia tu ndiyo ilikuwa inatosha. Sote kama taifa tuliwaona kama majuha na kipigo cha polisi walikipata.

Tofauti yao na sisi leo tuliomo katika hizi ibada za siku 3 pasipo na kufanya la maana, ni nini?

Ukweli mchungu namba zitapungua kwa kuchukua hatua stahiki tu, katu si kwa maombi yanayopelekea maambukizi mengine kwenye hiyo mikusanyiko.

Hatua stahiki hamzitaki mnategemea nini?

Kwa vile wanga nyie hamtaki ugonjwa huu kudhibitiwa subirini lichanganye, Ila msiyasahau maneno yenu litakapokuwa limekolea.

Ni hivyo tu - as plain as clear.

Waweza kujiridhisha hapo chini mwanga ni nani:

View attachment 1421809
 
Uvumilie na nani kama ww fridge limejaa usiseme tuvumilie lakin pia hata ww na familia yako mnaweza kujiweka lockdown

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makosa yalifanyika awali na kwa sasa kufanya total lockdown ni hatati zaidi.
Hatua za kufanya kwa sasa ni kuiweka kizuizini mikoa yote, kuzuia mikusanyiko na tahdhari nyingine za kiafya.
Total lockdown itatumiza kuliko corona.
 
Subirini mlango utajifunga wenyewe kwa lazima, ndio nchi za Africa zinavyokwenda.
 
Niambie tu ulikuwa wapi hadi kunitenga hivyo, japo niliogopa kukitafuta..
Wewe ni wa kuogopa kunitafuta kweeeliii! Upendo wako kwangu uko wapieti jamani kaka yangu kipenzi!!
Nilikuwa kwenye mfungo wa kwaresma!
 
Nani kakukataza kujifungia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie chadema kaeni lockdown

Sisi Watanzania tuliowengi tunakusikiliza maneno ya Rais wetu Magufuli

Tunachapa kazi

Ila ikifika mavuno msianze kusema serkali iwagawie chakula

Sent using Jamii Forums mobile app
Tangu zamani jiwe wenu aliwadanganya kuwa Tz ni matajiri na kama mko matajiri kwanini mnaogopa lockdown? ?
Kazi kusema2 tusitishane na corona huku amelala juu ya mawe
 
Wewe ni wa kuogopa kunitafuta kweeeliii! Upendo wako kwangu uko wapieti jamani kaka yangu kipenzi!!
Nilikuwa kwenye mfungo wa kwaresma!
Wow! Kumbe una imani kubwa kiasi hicho kipenzi changu?
 
Weka familia yako na ukoo wako wengine tutajifia ndan kwa sababu ya njaa wenye uwezo wa kujiwekea lockdown weken katika familia zenu
 
punguza povu
wewe na wamarekani nani mjinga kumzidi mwenzie,nani ana uwezo mzuri wa kupambana na huu ugonjwa kumzidi mwenzie???

unataka ujivishe crown ya umwamba hapa kwamba ulitumia akili zaidi ya wachina au unataka kufanya kitu gani??america,china,italy,iran wametumia kila mbinu wameangukia pua,labda utuambie wewe mbinu gani mpya unaweza kuja nayo ikasaidia au ndio wale wale,lawama zimwendee mwenyekiti chama tawala.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ishu ya lockdown ni ngumu sana kwa hali ya nchi yetu ni bora tu kufuata taratibu za kujikinga nalo tu hamna namna,,wakipiga lockdown nani wa kutulisha??

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Mkuu kati ya mimi na wamarekani mjinga utakuwa wewe.

Soma vizuri tokea uliporukia bandiko langu kama mnavyorukia matrenii mnapokuwa mmechoka kuishi.

Iko hivi nchi ulizozitaja USA, Italy na China tunayo mengi mno ya kujifunza kuhusu namna ya kuudhibiti na hata kuutokomeza ugonjwa huu. Siyo hao tu bali hata Germany, Kenya, Rwanda na Uganda.

Mwenyekiti wa chama tawala kuwa badala ya kujifunza kwa wenzetu na kutotenganisha imani za dini na uongozi wa nchi asipoyaona hayo akabadilika, si muda mrefu naye tutakosa uvumilivu.

Imeelezwa mno namna gani ya k uudhibiti na kumalizana na ugonjwa huu kama walivyifanikiwa wengine. Hakuna anayehitaji hata kutambuliwa kwa mchango wowote katika vita hivi kama ambavyo: kishamba shamba unajaribu wewe kudhani. Tunataka ugonjwa udhibitiwe si zaidi ya hapo.

Katika hilo hakuna povu wala nini. Povu unatoa wewe. Pitia mabandiko yako uliyoyahusianisha na yangu kutambua hilo.

Imependekezwa lockdown kuwa njia ya kwenda kuudhibiti ugonjwa huu. Hadi sasa hiyo ndiyo inaonyesha kuwa ingetufaa. Sijaona nyingine.

Angalau kwa kuanzia dar, Zanzibar na sehemu zilizo ishaathirika zingewekwa. Muda unazidi kuyoyoma. Ni mapopoma tu yasiyoona hayo.

Kama unataka waweza ona hapa pia:

Hoja za wanaoona lockdown haifai ni zipi? Tuelimishane - JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…