Mnaoendesha Tanesco mjitafakari sana

Mnaoendesha Tanesco mjitafakari sana

Secret Star

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2011
Posts
1,829
Reaction score
2,001
Huu uzi nauandika kwa masikitiko makubwa sana! Tanzania Umeme Umekuwa ukikatika tangu miaka 60 iliyopita, hadi leo umeme bado unaendelea kukatika na natumai miaka 50 ijayo ukija Tanzania utakuta hali ni hii hii!. Leo sababu ni hii miaka 100 ijayo kutakuwa na sababu nyingine mbalimbali, ni kama sababu mbalimbali zilizokuwepo miaka 50 iliyopita.

Shida ni kubwa ila leo nitazungumzia Kero ya ubadilishwaji wa nguzo! Sababu hii inawafanya Tanesco wakate umeme hovyo. Ni kweli Tanesco wanashindwa kutumia akili ndogo ya busara kukata umeme usiku labda kuanzia saa sita usiku hadi saa kumi na mbili asubuhi, ili watu wanavyoenda kutafuta mkate wa kila siku wasipate shida hiyo!

Tanesco mnawezaje kukata umeme mchana kwa siku tatu mfululizo!? Mnataka watu wale wapi!? Watu ambao ni masikini wa kutupwa wanaotegemea kipato cha kila siku ili wale chakula duni!. Tanesco mnashindwa kuwa na mitambo ya mwanga ili muwe mnafanya marekebisho ya miundombinu yenu usiku wa manane!

Yaani Tanesco nao wanataka Kwenda kazini saa mbili muda ambao raia nao wanaenda kazini, kisha Tanesco wakifika kazini wanakata umeme hadi jioni kisha wanarudisha na kurudi kutoka kazini!!! Nchi nyingine sio kwamba hawakati kabisa umeme ila wakitaka kifanya marekebisho wanatafuta muda ambao hautaathiri shughuli za wananchi!

😔😔Dah waTZ Hakyamungu tumekwisha!!!
 
Tulichagua viongozi wabovu ,Sasa no reform No election tuwe na viongozi wanaojali Kura za wananchi yaani mtu anazima umeme ,hakuna taarifa hakuna neno ukiuliza unaambiwa nenda burundi
 
Inaumiza sana maana Kuna biashara haziwezi kufanyika bila ya uwepo wa umeme

Ila ndiyo hivyo tunalalamika sana ila hakuna kipya mwendo ni ule ule

Oooh nchi yangu
 
Tumeitaka wenyewe, tumeipenda wenyewe wacha tuisome namba eeeyeeehh ssm mbele kwa mbele.
 
Tulichagua viongozi wabovu ,Sasa no reform No election tuwe na viongozi wanaojali Kura za wananchi yaani mtu anazima umeme ,hakuna taarifa hakuna neno ukiuliza unaambiwa nenda burundi
Chakandumuz kuna anayefaa kuongoza tanesco apewe?
 
Back
Top Bottom