Mad Max
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 31,139
- 88,800
Wimbi la makampuni feki yake kuchimba visima jijini Dodoma (na mikoa mingine) limekua kwa kasi sana, kutokana na changamoto ya maji na kasi ya ukuaji wa mji.
Sasa kushindana bei, wengi wao wasiowaaminifu wameanza uhuni na ujanja ujanja, ambao madhara yake hayataonekana ndani ya siku 2 au mwaka ila itapelekea visidumu zaidi ya miaka 5.
Ujanja wenyewe upoje?
1. Kuna watu wanawadanganya wateja wamechimba mita 100 mfano, kumbe wameishia mita 60 tu, na waipopata maji wakasitisha. Ila mteja wanamchaji kwa gharama za mita 100. Kwa mfano, Dodoma kuchimba ni Tsh 70,000 hadi 90,000 (kwa mita 1), kutegemea na diameter ya kisima, sasa imagine wakikuchimbia mita 60 tu na kukuibia mita 40 wamepiga kiasi gani?
2. Wengine hawaweki casing kisima chote. Mfano, wamwchimba mita 100 ila casing wanaweka kuanzia mita 40 kuja juu na kuacha mita 60 kwenda chini hazina casing. Hapa kisima kinaanza kucollapse mdogo mdogo haichukui muda mrefu na pia inaua pump kwasababu pump inakua inavuta mchanga.
3. Na wale watakao chimba urefu sahihi, na kuweka casings kisima chote, wanaweka PVC casings za grade ndogo kabisa. Hii nayo mbaya vile vile casings zinatabia ya kupasuka na kupelekea kisima kufukia kwasababu ya grade ndogo.
Kama mteja unatakiwa kufanya nini?
1. Kwanza hakikisha urefu wa kisima ni sahihi kama kwenye survey report na ukiweza aliefanya survey ndio asimamie uchimbaji na kuwe na makubaliano makali. Pia wakati wa survey aje na vifaa vya kisasa zaidi kwa mikoa kama Dodoma atleast aje na Magnetometer ya kisasa na Terrameter ya kisasa. Kwani combination yake ndio inatoa majibu mazuri.
2. Wakichimba omba wafanye borehole camera survey, kuna camera inaingizwa kwenye kisima na kukupa full picture ya kisima kwa ndani. Kama hajaweka bomba hadi chini itafahamika.
3. Hakikisha material anayoinstall ni sahihi na ya grade nzuri. Jipe muda kusoma nakuelewa kuhusu PVC grades.
4. Baada ya kumaliza hakikisha amefanya pumping test angalau ata kwa masaa 6 kama kisima binafsi ila kama cha jumuiya atleast masaa 24, pia hakikisha amefanya development kukiacha kisima safi.
Yote haya ni kwasababu kisima ni gharama sana kuchimba, zaidi ya mil 10 sasa kwanini kisidumu kwa saidi ya miaka 10?
Mjadala uko wazi.
Sasa kushindana bei, wengi wao wasiowaaminifu wameanza uhuni na ujanja ujanja, ambao madhara yake hayataonekana ndani ya siku 2 au mwaka ila itapelekea visidumu zaidi ya miaka 5.
Ujanja wenyewe upoje?
1. Kuna watu wanawadanganya wateja wamechimba mita 100 mfano, kumbe wameishia mita 60 tu, na waipopata maji wakasitisha. Ila mteja wanamchaji kwa gharama za mita 100. Kwa mfano, Dodoma kuchimba ni Tsh 70,000 hadi 90,000 (kwa mita 1), kutegemea na diameter ya kisima, sasa imagine wakikuchimbia mita 60 tu na kukuibia mita 40 wamepiga kiasi gani?
2. Wengine hawaweki casing kisima chote. Mfano, wamwchimba mita 100 ila casing wanaweka kuanzia mita 40 kuja juu na kuacha mita 60 kwenda chini hazina casing. Hapa kisima kinaanza kucollapse mdogo mdogo haichukui muda mrefu na pia inaua pump kwasababu pump inakua inavuta mchanga.
3. Na wale watakao chimba urefu sahihi, na kuweka casings kisima chote, wanaweka PVC casings za grade ndogo kabisa. Hii nayo mbaya vile vile casings zinatabia ya kupasuka na kupelekea kisima kufukia kwasababu ya grade ndogo.
Kama mteja unatakiwa kufanya nini?
1. Kwanza hakikisha urefu wa kisima ni sahihi kama kwenye survey report na ukiweza aliefanya survey ndio asimamie uchimbaji na kuwe na makubaliano makali. Pia wakati wa survey aje na vifaa vya kisasa zaidi kwa mikoa kama Dodoma atleast aje na Magnetometer ya kisasa na Terrameter ya kisasa. Kwani combination yake ndio inatoa majibu mazuri.
2. Wakichimba omba wafanye borehole camera survey, kuna camera inaingizwa kwenye kisima na kukupa full picture ya kisima kwa ndani. Kama hajaweka bomba hadi chini itafahamika.
3. Hakikisha material anayoinstall ni sahihi na ya grade nzuri. Jipe muda kusoma nakuelewa kuhusu PVC grades.
4. Baada ya kumaliza hakikisha amefanya pumping test angalau ata kwa masaa 6 kama kisima binafsi ila kama cha jumuiya atleast masaa 24, pia hakikisha amefanya development kukiacha kisima safi.
Yote haya ni kwasababu kisima ni gharama sana kuchimba, zaidi ya mil 10 sasa kwanini kisidumu kwa saidi ya miaka 10?
Mjadala uko wazi.