Mnachotufanyia mawakala ni dhambi

Mnachotufanyia mawakala ni dhambi

Line moja kila mtandao ni wazo zuri lakini kuna mapungufu.
Mfano ndugu X ana kampuni kubwa ya kimataifa ambayo iko nchi mbali mbali Africa.
Ana line ya voda hii ni kwa ajili tu ya kuwasiliana na wakurugenzi wake wa kanda za nchi za kusini mwa Africa kuliko na coverage nzuri ya voda.
Ana line ingine ya pili ya voda ajili ya kuwasiliana na ma manager wake walio mikoani Tanzania.
Ana line ya tatu ya voda ajili ya wakurugenzi wake walioko Africa mashariki.
Ana line ya nne ya voda ajili ya kuwasiliana na wanachama wa club yake vile yeye ni mfadhili mkuu na mwenyekiti wa club.
Ana line moja ya airtel kwa ajili ya kuwasiliana na ndugu zake tu na baba yake kijijini kwao kuliko na coverage nzuri ya airtel.
Ana line moja ya tigo kuwasiliana na mtu mshikaji kama wewe na washikaji wengi wa Dar kuliko na watumiaji wengi vile tigo wakazi wa dar wanaipenda sana.
Ana line ingine ambayo huitumia only for international calls kuongea na matajiri wenzake na hata maraisi mambo ya kuwekeza.

Kwa vyovyote mtu kama huyu akiwa na line moja kutatokea msongamano mkubwa mno taarifa zingine atazikosa.
Kumbuka mtu kama huyu ni jicho la taifa kwa kodi zake anazolipa na idadi kubwa ya watanzania amewaajiri nyuma yake kuna maelfu ya familia wanaishi kwa ajili yake.
Hapo hapo asubuhi akifika akifungua computer yake anakuta email 700 na zote anatakiwa azijibu.

Wazo lako ni zuri la kizalendo.Wazo langu watu kama hawa kuwe na utaratibu maalum kuwatambua.Kama ilivyo TANESCO mwenye kiwanda rate ya kulipa haiwezi kuwa sawa na mwenye bulb moja.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ilinitokea ikagoma, Akasema nirudie. Mimi nilishakataa KUMSAJILIA MTU,

Hata MKE wangu Nimekataa KUMSAJILIA.
Kaenda mwenyewe kupambana na Hali yake.

Sasa Kama ALITUMIA MBINU hiyo nitafanyaje nimjue au nimjue aliyemsajilia kutumia laini yangu?
 
Habari ndugu wana JamiiForums!

Kuna tabia imejitokeza baadhi ya mawakala wanaosajili laini za simu kwa alama za vidole kutumia gepu hilo kufyatua laini za ziada kwa kitambulisho cha mtu aliyeenda kusajili laini kwa alama za vidole bila yeye kujua. Mfano, anakuwa ameandaa laini katika simu yake ukimpatia kile kitambulisho anaingiza particular zako then anakwambia weka dole gumba, unaweka anajifanya kama imekataa anaanza kujaza upya kumbe ile aliyojifanya imekataa ilikubali, hapo hapo ataanza tena kujaza particular zako upya na kukusainsha kwa dole gumba kwa mara nyingine. Hivyo basi, utaondoka pale na kuacha laini iliyosajiliwa kinyemela bila wewe kujua kitu ambacho laini hizi pengine zikaanza kuuzwa hovyo mtaani kwa watu wenye nia ovyo na wakaja kuwajibishwa watu wasiokuwa na hatia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu unachokisema ni kweli post yako naikubali manake mimi mwenyewe juzi nilipita maeneo ya stand kubwa ya mabasi Arusha nikaingia kusajili line zangu mbili, cha ajabu line ya kwanza ya Tigo ikaleta shida sana mara mbili tatu naambiwa mtandao umegoma imekataa wakaniambia nijaribu tena nikaingiza dole gumba karibu mara tatu nne lakini nikamuuliza shida ni nini kwanini igome?

Nikahisi kama kuna ujanja flani wa kuongeza line zao za wizi hivyo nilitaka kugombana naye nikaona ngoja nitulie manake siku ikifika mambo kama haya yakijitokeza basi serikali ijue wazi kwamba huu usajili haukufanywa kwa uaminifu kuna watu watabambikiza kesi watu wengine hivyo ikitokea kosa kama hilo serikali isimuhukumu mtu mapema lazima upewe nafasi ya kujitetea. Kuna udanganyifu unafanywa na mawakala wa usajili.
 
Mimi verification zote za chip zangu nimefanyia HQ za mitando husika.
 
Vidole vyako ukivitazama vinafanana na vya mgonga kokoto au mkulima kama mimi?
 
Back
Top Bottom