Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Nilikuwa nasoma gazeti la habari leo, kuhusu awamu ya nne kutoa ajira zaidi ya milioni moja. Nilipofika kwenye maoni ya wasomaji nikakutana na maoni haya. Its funny!!
Unaweza kusoma habari hii kutoka hapaHii inaweza kuwa kweli kwamba zaidi ya watu milioni moja wameajiliwa kwenye secta binafsi. Naungana na Kapuya kwa kiasi kikubwa. Maana tangu awamu hii iingie madarakani idadi ya vibaka imeongezeka kwa karibu asilimia 50, kwa hiyo secta ya vibaka pekee inaweza kuwa imeajiri watu si chini ya laki tatu au nnei, huku ile ya majambazi wa kufunga njia na kutufuata majumbani kwetu na mapanga na bunduki ikiajiri almost watu laki moja na ushee.
Kwa kweli namuunga mkono Kapuya kwamba serikali ya Kikwete imefanya kazi nzuri sana. Maana sasa hivi kila kona ya nchi si Arusha, si Dar es salaam na kwingineko kwingi watu wanalia kila kunapokucha, hadi mapadri wanataka kugoma kuzika watu kutokana na kila kunapokucha wanazika watu waliouawa na Majambazi.
Good job Kikwete and Kapuya.