Midavudavu
JF-Expert Member
- Jan 23, 2012
- 287
- 59
Mmasai mmoja alipanda daladala eneo la hospitali kuu Moro. Daladala ilipofika eneo la shan darajani akamwambia konda " elo, imefika shusha hapahapa darajani" Konda akamwambia darajani hatushushi hakuna kituo. "Elo, mbona kupandisa inapandisa popote kwa nini kushusha inachagua?, na mimi sasa kukulipa inachagua itakulipa siku ingine kama inanipitisha hapa". Konda ikabidi amshushe darajani huku akilalama tatizo la wamasai wabishi. Abiria wakamtete yule mmasai na kusem si kweli ila yeye konda pale alipompakia hapakuwa na kituo hivyo kama anataka wengine wafuate sheria na yeye afuate sheria.