DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Democratic Party (DP), Abdul Juma Mluya, akiambatana na Mgombea wake mwenza Sadoun Abrahman Khatib, leo Agosti 13, 2025, wamechukua fomu za uteuzi katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Njedengwa jijini Dodoma.
Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu, Mluya alisema huu ni wakati wa kuwakomboa Watanzania kwa kumaliza malalamiko ya muda mrefu kwenye huduma za kijamii, ikiwemo sekta ya afya, kuboresha maisha ya watumishi wa umma, na kuinua maslahi ya Jeshi la Polisi na Magereza.
“Serikali yangu itakuwa na wajibu wa kuwatunza mama mjamzito na mtoto kwa kumpa lishe bora kwa muda wa miezi mitatu,” amesema Mluya.
Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu, Mluya alisema huu ni wakati wa kuwakomboa Watanzania kwa kumaliza malalamiko ya muda mrefu kwenye huduma za kijamii, ikiwemo sekta ya afya, kuboresha maisha ya watumishi wa umma, na kuinua maslahi ya Jeshi la Polisi na Magereza.
“Serikali yangu itakuwa na wajibu wa kuwatunza mama mjamzito na mtoto kwa kumpa lishe bora kwa muda wa miezi mitatu,” amesema Mluya.