MUSHEKY
JF-Expert Member
- May 9, 2014
- 2,812
- 2,765
Habarini wakuu,
Kwa nyakati tofauti ndani ya jiji la Dar nilikua nikisikia tuhuma mbali mbali zinazotupiwa kwa hii hospitali yetu kubwa ya kisasa na yenye sifa za kimataifa
Nimesikia mara kadhaa kwa watu kwamba ukimpeleka mgonjwa wako pale kama ni serious case basi ujue atapotea tu
Minong'ono hii inakuja kwa dhana kuu mbili ambazo serikali hasa wizara ya afya naomba ifanye uchunguzi ili kubaini ukweli wake na kuleta ufumbuzi
Dhana ya kwanza ni kwamba madaktari wengi wa pale ni madaktari wanafunzi ambao hufanya mazoezi kwa vitendo kwa wangonjwa.......
Dhana hii imepelekea wagonjwa wengi wanaopewa rufaa ya kwenda kule kuikacha hospitali hiyo na kurudi majumbani
USHUHUDA: wiki kadhaa zilizopita nikikua pale muhimbili kumuuguza mgonjwa wangu ambaye hata hivyo aliamriwa na madaktari afanyiwe upasuaji tumboni ili kuondoa uvimbe aliokua nao
Jambo la kushangaza ambalo pia ndilo limenisukuma kuandika mada hii ni baada ya ndugu yangu huyo pamoja na wagonjwa wengine kama kumi na tano waliokua wodini hapo kupewa rufaa ya kwenda hospitali ya mloganzila
Wodi iligeuka kua uwanja wa mabishano kati ya aliyetoa maelekezo hayo na wagonjwa.....wengi walilalama kwamba hawawezi kwenda kule kufa
Ghafla niliona wagonjwa hao wanafungasha mabegi na kusepa bila kwenda walikoamriwa
Dhana ya pili ni gharama kubwa ambayo inalalamikiwa hospitalini hapo ambayo pia inawafanya wagonjwa wapakimbie
Kwa kua haya ni maneno yanazungumzwa kwa wingi, naiomba wizara husika ichunguze jambo hili kwa makini
Nawasilisha
Kwa nyakati tofauti ndani ya jiji la Dar nilikua nikisikia tuhuma mbali mbali zinazotupiwa kwa hii hospitali yetu kubwa ya kisasa na yenye sifa za kimataifa
Nimesikia mara kadhaa kwa watu kwamba ukimpeleka mgonjwa wako pale kama ni serious case basi ujue atapotea tu
Minong'ono hii inakuja kwa dhana kuu mbili ambazo serikali hasa wizara ya afya naomba ifanye uchunguzi ili kubaini ukweli wake na kuleta ufumbuzi
Dhana ya kwanza ni kwamba madaktari wengi wa pale ni madaktari wanafunzi ambao hufanya mazoezi kwa vitendo kwa wangonjwa.......
Dhana hii imepelekea wagonjwa wengi wanaopewa rufaa ya kwenda kule kuikacha hospitali hiyo na kurudi majumbani
USHUHUDA: wiki kadhaa zilizopita nikikua pale muhimbili kumuuguza mgonjwa wangu ambaye hata hivyo aliamriwa na madaktari afanyiwe upasuaji tumboni ili kuondoa uvimbe aliokua nao
Jambo la kushangaza ambalo pia ndilo limenisukuma kuandika mada hii ni baada ya ndugu yangu huyo pamoja na wagonjwa wengine kama kumi na tano waliokua wodini hapo kupewa rufaa ya kwenda hospitali ya mloganzila
Wodi iligeuka kua uwanja wa mabishano kati ya aliyetoa maelekezo hayo na wagonjwa.....wengi walilalama kwamba hawawezi kwenda kule kufa
Ghafla niliona wagonjwa hao wanafungasha mabegi na kusepa bila kwenda walikoamriwa
Dhana ya pili ni gharama kubwa ambayo inalalamikiwa hospitalini hapo ambayo pia inawafanya wagonjwa wapakimbie
Kwa kua haya ni maneno yanazungumzwa kwa wingi, naiomba wizara husika ichunguze jambo hili kwa makini
Nawasilisha