Mliowahi kufanyiwa operation ya Appendix njooni mnisaidie

Mliowahi kufanyiwa operation ya Appendix njooni mnisaidie

X_INTELLIGENCE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2014
Posts
10,721
Reaction score
14,852
Habarini, ndugu zangu.

Mnamo mwaka 2014 nilifanyiwa opperation ya Appendix, kidonda kilipona haraka haraka pasipo kupata maumivu yoyote,
Tokea mwaka huo 2014 hadi sasa ni miaka 3 sasa,

Ila chaajabu tokea mvua izi zianze kunyesha juzi napatwa na maumivu pale kwenye kovu la kidonda cha appendex...mara ya kwanza maumivu yalidumu kwa muda wa masaa 2 kisha yakapotea usiku wa kuamkia leo sijalala kabisa maumivu hapo kwenye kovu la kidonda cha apendex yamenianza tokea saa 6 usiku hadi kuna kucha, sijapata usingizi, naombeni ushauri wenu kwani miaka ya nyuma baada ya operation nilikuwa sipati maumivu ata nikiloana kwenye mvua...hii hali imenitisha sana
 
Ni kawaida, hali hio hujitokeza kipindi cha baridi, au pale mwili unapo hisi baridi kali, cha msingi hali hio ikijitokeza vaa nguo nzito au/na kunywa kinywaji cha moto kama chai hivi n. K
 
Hiyo kawaida bro nilifanyiwa operation ya mkononi inatokea Mara chache wkt wa baridi kuuma cha kufanya huwa napaka Vaseline kwny kovu hlf najifunika kitu kizito inasaidia kdg sio kama una tatizo
Asante kwa ushauri....nilianza kuchanganyikiwa
 
Ni kawaida, hali hio hujitokeza kipindi cha baridi, au pale mwili unapo hisi baridi kali, cha msingi hali hio ikijitokeza vaa nguo nzito au/na kunywa kinywaji cha moto kama chai hivi n. K
Asante sana kwa ushauri....
 
Habarini, ndugu zangu.

Mnamo mwaka 2014 nilifanyiwa opperation ya Appendix, kidonda kilipona haraka haraka pasipo kupata maumivu yoyote,
Tokea mwaka huo 2014 hadi sasa ni miaka 3 sasa,

Ila chaajabu tokea mvua izi zianze kunyesha juzi napatwa na maumivu pale kwenye kovu la kidonda cha appendex...mara ya kwanza maumivu yalidumu kwa muda wa masaa 2 kisha yakapotea usiku wa kuamkia leo sijalala kabisa maumivu hapo kwenye kovu la kidonda cha apendex yamenianza tokea saa 6 usiku hadi kuna kucha, sijapata usingizi, naombeni ushauri wenu kwani miaka ya nyuma baada ya operation nilikuwa sipati maumivu ata nikiloana kwenye mvua...hii hali imenitisha sana
Kawaida hiyo mkuu.... Pole sana... Huwa kuna contraction ya muscles wakati wa baridi inayosababisha compression ya mishipa ya fahamu iliyoharibika na kusababisha maumivu kwenye kovu.
 
Kawaida hiyo mkuu.... Pole sana... Huwa kuna contraction ya muscles wakati wa baridi inayosababisha compression ya mishipa ya fahamu iliyoharibika na kusababisha maumivu kwenye kovu.
Asante sana kwa kunitoa hofu
 
ukipata maumivu ya kovu la upasuaji kipindi cha baridi au mvua ni kawaida.lakini ikiwa kipindi tofauti na hivyo ni dalili ya uambukizo mfano UTI nakadhalika
 
kama ni appendexectomy hakuna zuio baada ya masaa 24 toka ufanyiwe upasuaji japo kienyeji hupendekeza usile maharage japo ndani ya mwezi 1 kuepuka kupumua(kujmba) hovyo tena kwa sauti
Asante sana
 
Hakuna zuio labda kwa alifanyiwa operation ya utumbo uliotobolewa na H pylori utaambiwa vyakula vyenye acid usile na stress punguza
 
Nimeuliza hapa Kuna mmoja hapa kasema kuna dawa ya maumivu inaitwa pyroxam (sina uhakika kama inaandikwa ivo ila ukienda pharmacy wataijua).

Mwingine pia kasema ni hali ambayo hua inatokea hasa kipindi cha baridi so yeye akijisikia maumivu kipindi cha baridi hua anakunywa chai ya moto au wakati mwingine hua anachemsha maji then anajikanda hapo juu ya mshono ili kuweka joto.

Kwakifupi mshono haupatani na baridi ivo hata mavazi jitahidi kuvaa ambayo yanazuia baradi.

Kama uvimbe umeanza kutokeza sehemu ya mshono ni vyema uende hospitali kwajili ya kupiga utrasound pamoja na kupata tiba na ushauri wa kitaalamu.

Nimeguswa na thread yako maana nimezungukwa na watu kadhaa wenye tatizo kama lako.pole mkuu.
 
Mimi ni mwenzio, nimefanyiwa mwaka 2000 Bugando ni kawaida. Ila epuka mkanda wa suruali inayopabana na hata suruali yenyewe isibane sana sehemu hiyo!!

Ni kawaida wakati wa mawingu kusikia maumivu japo hua si makali kama unavyohadithia!!
Yangu yalikuwa makali...sikulala...ila namshukuru Mungu mvua zimekata na maumivu yamekata
 
Nimependa polite language iliyotumiwa na wachangiaji wa thread na hali ya upole ya mletaji mada.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom