Kimwakaleli
JF-Expert Member
- Apr 16, 2018
- 3,897
- 5,354
Habari wanajf kwa ujumla,wakubwa shikamoo,wenzangu na mie mambo vipi poa,wadogo zangu,marahaba.Nimekuwa nikifuatilia sana mambo mbalimbali yanayohusu ujenzi na ushauri unaotolew kwa kweli!Nimeamini ndo maana wenye nyumba wanakuwa wakali!Ukiwacheleweshea kodi yao.Maana uhalisi wa makisio na yaliyopo field ni tofauti kwa sana.Matofali sawa,cementi sawa,mchanga sawa,lakini unakutana na gharama zingine ambazo hata hukuwaza kabisa!Kama vile kungoa visiki,mara wa kumwagilia,mara sururu,kuchimba msingi,ndoo cha kuchotea maji,kuchimba vyoo,kuweka mbao za kuweka renta na za kusimania na makorokoro kibao!Nawapa maua yenu wenye nyumba,punguzeni sasa kodi.