Simba Mkali
JF-Expert Member
- Jan 31, 2012
- 620
- 239
MLIMANI CITY 'SI SALAMA?'
Na Mwandishi Wetu
MAEGESHO ya magari mbele ya masoko ya Mlimani City yameelezwa kuwa 'si Salama'.
Habari zinaeleza kuwa hivi karibuni Prof. Kulikoyela Kahigi alivunjiwa kioo cha dirisha na kompyta yake ndogo kuibiwa. Naye Prof. Joseph Mbelle wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam amewahi kuibiwa kompyuta yake ndogo kwenye maegesho hayohayo. Dirisha la gari lake wahusika kutokomea.
Juzi, Jumatatu ofisa mmoja alisema " Nilipaki gari langu tarehe 21 Febr. mwaka huu, nikaondoka na kuingia sokoni, nilikuta wamebomoa," aliezea ofisa huyo katika sauti ya huzuni " Niliporudi nilikuta kioo cha dirisha nyuma kimevunjwa na kompyta yangu imechukuliwa."
Amesema kuwa alipomweleza ndugu yake juu ya tukio hilo, alielezwa kuwa yeye si wa kwanza kuibiwa katika viwanja hivyo vya kuegesha magari.
Ofisa aliyeibiwa kompyuta yake alivyoliarifu tukio hilo kwa kampuni ya OMEGA Nitro inayofanya lindo katika eneo hilo,walisajili tukio hilo kwa Kumb. OB NO1763 kwa lindop la Mlimani City.
Aidha , walitoa OB No 684 kwa makao makuu yao yaliyopo Mikocheni Dar es salaam na kuahidi kuendelea na uchunguzi. OB ni kama RB za polisi wakati mtu anaporipoti shauri.
Aliyeibiwa kompyuta anasema alikuwa ameegesha gari "hatua chache" kutoka kwenye kichanja alipokuwa amekaa askari wa kampuni hiyo ya ulinzi.
Mkaguzi wa malindo wa OMEGA Nitro inayotokea Afrika Kusini alilifika kushuhudia jinsi wizi ulivyotokea.
"Cha kushangaza ni kwamba atafutwe askari aliyekuwa analinda eneo hilo, aliyekuwa kwenye kichanja pale juu: lakini walishindwa kumpata, eti hawamjui.
"Jambo hilo lilinipa mashaka kwa kuwa wizi unaotokea hapo una uhusiano wa moja kwa moja na walinzi wa kampuni iliyopata kandarasi ya kusimamia usalama wa wateja na mali zao." anasema.
Ofisa huyo anasema ni aibu kwa eneo la Mlimani City kutokuwa na kamera za usalamala (CCTV) za kusaidia lindo kwa kuonyesha kila tendo ndani ya maegesho.
"Nimeambiwa kila anayeibiwa huambiwa kuwa utawalawa eneo hauusiki na lindo la gari lake. Huu ni upuuzi," amesema akionyesha kulalamika.
"Wanakimbilia kuonyesha kadi kwa kuwa unapoingia na gari lako, unapewa kadi ambayo nyuma yake inaeleza kuwa usalama wa mali zako ni juu yako na kwamba unatakiwa kuondoa vitu vya thamani katika gari ulilopaki," anaeleza.
Ofisa huyo anakataa maelezo hayo akisema, " Kama hivyo, kwanini wanatoa kandarasi ya kuhakikisha usalama wa eneo lao?"..... SOURCE GAZETI LA MWANAHALISI - JUMATANO MACHI 21-27
Na Mwandishi Wetu
MAEGESHO ya magari mbele ya masoko ya Mlimani City yameelezwa kuwa 'si Salama'.
Habari zinaeleza kuwa hivi karibuni Prof. Kulikoyela Kahigi alivunjiwa kioo cha dirisha na kompyta yake ndogo kuibiwa. Naye Prof. Joseph Mbelle wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam amewahi kuibiwa kompyuta yake ndogo kwenye maegesho hayohayo. Dirisha la gari lake wahusika kutokomea.
Juzi, Jumatatu ofisa mmoja alisema " Nilipaki gari langu tarehe 21 Febr. mwaka huu, nikaondoka na kuingia sokoni, nilikuta wamebomoa," aliezea ofisa huyo katika sauti ya huzuni " Niliporudi nilikuta kioo cha dirisha nyuma kimevunjwa na kompyta yangu imechukuliwa."
Amesema kuwa alipomweleza ndugu yake juu ya tukio hilo, alielezwa kuwa yeye si wa kwanza kuibiwa katika viwanja hivyo vya kuegesha magari.
Ofisa aliyeibiwa kompyuta yake alivyoliarifu tukio hilo kwa kampuni ya OMEGA Nitro inayofanya lindo katika eneo hilo,walisajili tukio hilo kwa Kumb. OB NO1763 kwa lindop la Mlimani City.
Aidha , walitoa OB No 684 kwa makao makuu yao yaliyopo Mikocheni Dar es salaam na kuahidi kuendelea na uchunguzi. OB ni kama RB za polisi wakati mtu anaporipoti shauri.
Aliyeibiwa kompyuta anasema alikuwa ameegesha gari "hatua chache" kutoka kwenye kichanja alipokuwa amekaa askari wa kampuni hiyo ya ulinzi.
Mkaguzi wa malindo wa OMEGA Nitro inayotokea Afrika Kusini alilifika kushuhudia jinsi wizi ulivyotokea.
"Cha kushangaza ni kwamba atafutwe askari aliyekuwa analinda eneo hilo, aliyekuwa kwenye kichanja pale juu: lakini walishindwa kumpata, eti hawamjui.
"Jambo hilo lilinipa mashaka kwa kuwa wizi unaotokea hapo una uhusiano wa moja kwa moja na walinzi wa kampuni iliyopata kandarasi ya kusimamia usalama wa wateja na mali zao." anasema.
Ofisa huyo anasema ni aibu kwa eneo la Mlimani City kutokuwa na kamera za usalamala (CCTV) za kusaidia lindo kwa kuonyesha kila tendo ndani ya maegesho.
"Nimeambiwa kila anayeibiwa huambiwa kuwa utawalawa eneo hauusiki na lindo la gari lake. Huu ni upuuzi," amesema akionyesha kulalamika.
"Wanakimbilia kuonyesha kadi kwa kuwa unapoingia na gari lako, unapewa kadi ambayo nyuma yake inaeleza kuwa usalama wa mali zako ni juu yako na kwamba unatakiwa kuondoa vitu vya thamani katika gari ulilopaki," anaeleza.
Ofisa huyo anakataa maelezo hayo akisema, " Kama hivyo, kwanini wanatoa kandarasi ya kuhakikisha usalama wa eneo lao?"..... SOURCE GAZETI LA MWANAHALISI - JUMATANO MACHI 21-27