madaili
Member
- Mar 6, 2014
- 32
- 27
Mlevi mmoja aliona tangazo la kazi kwenye kampuni moja ya bia, sharti lilikuwa ni moja tuu, awe mtaalam wa kunywa pombe, akatuma maombi ya kazi. Baadaye akaitwa kwenye usahili.
Siku ya usahili akawekewa glasi za bia tofauti tofauti kama kumi hivi. Alipomaliza kuonja bia zote, aliweza kusema aina ya bia, mwaka iliotengenezwa, kiwango cha alcohol na viwango vyote vinavyohusu kila bia iliyopo kwenye glasi. Wasahili wote wakabaki na butwaa. Meneja wa kiwanda akajifikiria kidogo, akamwita secretary wake akamnong'oneza kisha secretary akatoka, baada ya dakika chache akarudi na glasi imejaa nusu na akamkabidhi mlevi. Baada ya mlevi kunywa akasema "mwanamke, miaka 25, ana mimba ya miezi miwili" , baada ya hapo watu wote wakawa kimya kama jini limepita. Mlevi akahisi jamaa hawataki kumpa kazi, akasema hivi "Sasa kama hamnipi hii kazi nitasema mpaka jina la baba wa huyo mtoto", kabla hajamalizia kuongea wasahili wa kiume wote pamoja na meneja wakasema "umepita, umepita, kazi umepata bwana", halafu kila mmoja akatoka na kichwa ameinamisha chini.
Jumapili njema wanajamii
Siku ya usahili akawekewa glasi za bia tofauti tofauti kama kumi hivi. Alipomaliza kuonja bia zote, aliweza kusema aina ya bia, mwaka iliotengenezwa, kiwango cha alcohol na viwango vyote vinavyohusu kila bia iliyopo kwenye glasi. Wasahili wote wakabaki na butwaa. Meneja wa kiwanda akajifikiria kidogo, akamwita secretary wake akamnong'oneza kisha secretary akatoka, baada ya dakika chache akarudi na glasi imejaa nusu na akamkabidhi mlevi. Baada ya mlevi kunywa akasema "mwanamke, miaka 25, ana mimba ya miezi miwili" , baada ya hapo watu wote wakawa kimya kama jini limepita. Mlevi akahisi jamaa hawataki kumpa kazi, akasema hivi "Sasa kama hamnipi hii kazi nitasema mpaka jina la baba wa huyo mtoto", kabla hajamalizia kuongea wasahili wa kiume wote pamoja na meneja wakasema "umepita, umepita, kazi umepata bwana", halafu kila mmoja akatoka na kichwa ameinamisha chini.
Jumapili njema wanajamii