Mkuyu ni Mti gani?

Mkuyu ni Mti gani?

Mkuyu ni huo uliopo kwenye picha ya kwanza.

Lakini huo aliposimama huyo jamaa mwenye ndevu za mvi unaitwa: "mrumba".
 
Ulio Nyuma ya picha utakuwa Ficus religious (Ipo Asia hasa India).Mrumba unaitwa Kisayansi Fucus natalensis na ndiyo mingi IPO kuanzia Natal province Kule SA Hadi Kenya na Uganda,ndiyo inaitwa Mtoma Kule Bukoba Hadi Uganda.Mikoa ya Geita,Kagera na Kigoma magome Yake hutengeneza Mashuka ya Asili,lakini pia ni mahali Ibada za kiasili hufanyika.Ukipita Maeneo ya vijijini ilikuwa ikipandwa kichwani mwa kaburi na iliita hapo ndiyo Ibada za Kuomba Kwa waliokuwa zilifanyika.Ni Mtu ambapo ni sacred,pengine kama ulivyo Banyan tree Kwa Hindu na Budha.
 
kweli mkuu. Lkn pia nafikiri ana asili ya kwa Kenyatta.
Kiroho sisi ni wamoja haijalishi kabila wala asili ya ulikozaliwa. Huyo jamaa ni mwalimu mzuri sana wa physics, advanced mathematics na chemistry. Tulikutana naye wakati wa harakati za kujitafuta tuweze kujitambua sisi ni nani? Kwanini tumezaliwa? Kwanini tunaishi?

Kupitia huyo jamaa ambao wengi wame mjaji kwa kuona picha yake tulijifunza elimu ya Buddha ambayo ni adimu sana kwetu sisi wabongo na waafrika. Gordian Anduru uzidi kubarikiwa pamoja na vizazi vyako
 
Mti huu hukua popote lakini hupatikana sana kwenye mito,haya ndio mazingira mazuri zaidi ambako mkuyu hupatikana.Unahusishwa sana na imani za kiganga na inaaminiwa unafaa sana kupunga majini wachafu.Ni rafiki wa ndege maana una matunda yanayonukia vizuri na yenye mbegu mbegu ambazo hata binadamu waroho hujaribu kuyala.Ni mti wa imani pia
 
Back
Top Bottom