DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert John Chalamila, amefanya ukaguzi maalum katika eneo la Mbagala ili kujionea uharibifu uliotokea kufuatia tukio la maandamano lililotokea tarehe 29 Oktoba. Ukaguzi huo umefanywa kwa lengo la kutathmini athari zilizopata miundombinu ya mradi wa mabasi ya mwendokasi (BRT).
Katika ziara hiyo, Mhe. Chalamila alieleza kusikitishwa na vitendo vya baadhi ya waandamanaji vilivyoharibu miundombinu ya umma, akisisitiza kuwa uharibifu huo umeathiri huduma muhimu zinazotegemewa na wananchi wa Mbagala na maeneo jirani.
Ametangaza rasmi kuwa huduma za mabasi ya mwendokasi katika njia ya Mbagala, zilizositishwa kufuatia tukio hilo, zitaanza tena tarehe 20 Novemba kama kawaida. Ameeleza kuwa matengenezo yanayofanyika sasa yanahakikisha usalama wa abiria na ufanisi wa huduma hiyo pindi itakaporejea.
Amesisitiza pia kuwa serikali ya mkoa itaendelea kushirikiana na vyombo vya usalama na watendaji wengine kuhakikisha matukio ya uharibifu wa miundombinu ya umma hayajirudii, huku akiwaomba wananchi kulinda rasilimali hizo kwani ni mali yao na zinachangia kuboresha maisha ya kila siku
Katika ziara hiyo, Mhe. Chalamila alieleza kusikitishwa na vitendo vya baadhi ya waandamanaji vilivyoharibu miundombinu ya umma, akisisitiza kuwa uharibifu huo umeathiri huduma muhimu zinazotegemewa na wananchi wa Mbagala na maeneo jirani.
Ametangaza rasmi kuwa huduma za mabasi ya mwendokasi katika njia ya Mbagala, zilizositishwa kufuatia tukio hilo, zitaanza tena tarehe 20 Novemba kama kawaida. Ameeleza kuwa matengenezo yanayofanyika sasa yanahakikisha usalama wa abiria na ufanisi wa huduma hiyo pindi itakaporejea.
Amesisitiza pia kuwa serikali ya mkoa itaendelea kushirikiana na vyombo vya usalama na watendaji wengine kuhakikisha matukio ya uharibifu wa miundombinu ya umma hayajirudii, huku akiwaomba wananchi kulinda rasilimali hizo kwani ni mali yao na zinachangia kuboresha maisha ya kila siku