Mkutano wa CUF kuhusu gesi wafana Mtwara

Mkutano wa CUF kuhusu gesi wafana Mtwara

mcubic

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2011
Posts
10,310
Reaction score
6,548
Leo kuanzia mida ya saa kumi jioni kulikuwa na mkutano mkubwa uliofanyika katika viwanja vya bima katikati kabisa mwa mji wa Mtwara. Mkutano huo ulioandaliwa na CUF ulihudhuriwa na Bwana Katani Katani ambaye alikuwa mgeni rasmi wa mkutano huo. Bwana Katani aligombea ubunge katika wilaya ya Tandahimba na kushindwa kwa mizengwe na Ndugu Njwayo wa CCM, alivalia pensi na Tshirt aliushangaza umati huo kwa mavazi yake lakini alipoanza kutoa hoja wananchi hao walisahau mavazi yake hayo.

Hoja
Wengi wa wazungumzaji walishikilia msimamo ule ule "Gesi haitoki ikiwa Ghafi" huku kauli mbiu nyingine ikiibuka na kusema "Gesi kusini kwanza Dar Baadae". Moja ya hoja ni kuwa ni lazima gesi ichakatwe hapa mkoani Mtwara na plant ya umeme ianzishwe hapa Mtwara na kisha usafirishwe kunufaisha watanzania wengine. Mmoja wa wazungumzaji alisema Wanamtwara wamechoka kuwa vipofu wa kushikwa mkono wakati wa kula ugali na sasa wanaona na wanataka kula ugali huo bila kushikwa tena mkono.

Wananchi wengi walikuwa wanajibu maswali wanayoulizwa kwa hamasa kubwa...Mfano swali moja liliuliza "wangapi wapo tayari kufa ili gesi isitoke Mtwara?" wananchi karibu wote waliokuwepo pale walinyoosha mikono..(Mtaona picha hizo kwenye magazeti na blog mbalimbali...kwani niliona waandishi wengi wa habari...binafsi sikufanikiwa kupiga picha)

Wazungumzaji wengi waliwashutumu Mh Ghasia kwa kufananisha jina lake na neno "FUJO" huku Mkuchika akianikwa hadharani kuwa ni mnafiki namba moja na kwamba mawaziri hao kwa sasa hawawezi kutembea tena Mchana wakiwa Mtwara na wamekuwa wakiingia kimya kimya tena usiku kuepuka dhahma kutoka kwa wananchi hao.

Roma Mkatoloki, Kalapina Na Kundambanda Kupamba Mkutano
Mgeni rasmi aliutaarifu umma kuwa tarehe kumi na tisa ya mwezi huu kutakuwa na maandamano na mkutano mkubwa mwingine wa kupinga suala la gesi na kusema Mkutano huo utahudhuriwa na Wasanii Roma Mkatoliki, Kalapina na Kundambanda. Alisema wameshindwa kumualika "Diamond" kwa kuwa suala hilo si la burudani bali la kiharakati zaidi ndio maana amewaalika wasanii wanaharakati.


Wacha niishie hapa...kwa jinsi nilivyoona Wananchi waliopo mkutanoni......Kuna haja ya Serikali kukutana na Wanaanchi kupata muafaka wa suala hili....vinginevyo tunapoelekea si kuzuri...
 
all the best mtwara kwanza kwa hili la gesi....inshaallah mungu atatuelewa ana atatupigania tu.
 
eti mungu atawapigania thubutuuuu, komaeni na kuanza kunoa mapanga kwaajili ya mapambano
 
boko aramu hiyooooooo

pole mkuu najua habari kama hizi zinapasua kichwa chako kwa maumivu, ushauri tafuta diclopa umeze, binafsi nimepita maeneo haya mida hiyo hawa wana mtwara hawatanii mahudhurio kwenye mikutano yao watu hawapungui zaidi wanaongezeka kila mkutano ukiitishwa, ebu fanya mpango uje uyaseme haya maneno yako yatakupata kama yaliyo mpata rafiki yako mbatia
 
Kwa taarifa nilizozipata, kesho CUF watakuwa na mkutano wa hadhara, Tandahimba.
Majira ya saa 6 mchana.
Mgeni rasmi ni Katani A. Katani.
 
i was there.nimeshindwa kuamini macho yangu. watu wa Mtwara wameungana kikweli kuona gesi haitoki mtwara ikiwa ghafi. watu walikuwa wengi kuliko kawaida, haijapata kutokea kwa miaka mingi.
kwa maoni yangu serikali ikubali kukaa pamoja na watu wa mtwara wajadili jambo hili tunako kwenda ni kubaya.kuna kila dalili kuwa vijana wale wanaweza kutumiwa na watu wabaya na kujikuta tumeingia kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe.watu wamehamasika kupita maelezo.
 
CUF watapewa talaka na bwana wao CCM kama wataanza siasa za kuikosoa ohoooo!
Leo kuanzia mida ya saa kumi jioni kulikuwa na mkutano mkubwa uliofanyika katika viwanja vya bima katikati kabisa mwa mji wa Mtwara. Mkutano huo ulioandaliwa na CUF ulihudhuriwa na Bwana Katani Katani ambaye alikuwa mgeni rasmi wa mkutano huo. Bwana Katani aligombea ubunge katika wilaya ya Tandahimba na kushindwa kwa mizengwe na Ndugu Njwayo wa CCM, alivalia pensi na Tshirt aliushangaza umati huo kwa mavazi yake lakini alipoanza kutoa hoja wananchi hao walisahau mavazi yake hayo.

Hoja
Wengi wa wazungumzaji walishikilia msimamo ule ule "Gesi haitoki ikiwa Ghafi" huku kauli mbiu nyingine ikiibuka na kusema "Gesi kusini kwanza Dar Baadae". Moja ya hoja ni kuwa ni lazima gesi ichakatwe hapa mkoani Mtwara na plant ya umeme ianzishwe hapa Mtwara na kisha usafirishwe kunufaisha watanzania wengine. Mmoja wa wazungumzaji alisema Wanamtwara wamechoka kuwa vipofu wa kushikwa mkono wakati wa kula ugali na sasa wanaona na wanataka kula ugali huo bila kushikwa tena mkono.

Wananchi wengi walikuwa wanajibu maswali wanayoulizwa kwa hamasa kubwa...Mfano swali moja liliuliza "wangapi wapo tayari kufa ili gesi isitoke Mtwara?" wananchi karibu wote waliokuwepo pale walinyoosha mikono..(Mtaona picha hizo kwenye magazeti na blog mbalimbali...kwani niliona waandishi wengi wa habari...binafsi sikufanikiwa kupiga picha)

Wazungumzaji wengi waliwashutumu Mh Ghasia kwa kufananisha jina lake na neno "FUJO" huku Mkuchika akianikwa hadharani kuwa ni mnafiki namba moja na kwamba mawaziri hao kwa sasa hawawezi kutembea tena Mchana wakiwa Mtwara na wamekuwa wakiingia kimya kimya tena usiku kuepuka dhahma kutoka kwa wananchi hao.

Roma Mkatoloki, Kalapina Na Kundambanda Kupamba Mkutano
Mgeni rasmi aliutaarifu umma kuwa tarehe kumi na tisa ya mwezi huu kutakuwa na maandamano na mkutano mkubwa mwingine wa kupinga suala la gesi na kusema Mkutano huo utahudhuriwa na Wasanii Roma Mkatoliki, Kalapina na Kundambanda. Alisema wameshindwa kumualika "Diamond" kwa kuwa suala hilo si la burudani bali la kiharakati zaidi ndio maana amewaalika wasanii wanaharakati.


Wacha niishie hapa...kwa jinsi nilivyoona Wananchi waliopo mkutanoni......Kuna haja ya Serikali kukutana na Wanaanchi kupata muafaka wa suala hili....vinginevyo tunapoelekea si kuzuri...
 
Safi kabisa wana-Mtwara!!! Historia inajirudia!! Hata vita vya majimaji vilianzia huko kusini!!
 
Kuna ntu huku kashasema serikali isipokua makini tena swala hili la gesi litamwaga damu
 
Kuna ntu huku kashasema serikali isipokua makini tena swala hili la gesi litamwaga damu
Damu wameizoea toka ukombozi wa Msumbiji. Watu wa Mtwara waliuwawa sana na mabomu yaliyokuwa yanategwa na Wareno maeneo ya Mahurunga na kwingineko!
 
Kuna ntu huku kashasema serikali isipokua makini tena swala hili la gesi litamwaga damu

Hapo ndipo utaona mawazo ya wanadamu walivyo madogo kuliko ya yule aliyeumnba Mungu katoa hizi natural resources ili zifaidishe watu lakini zinageuka kuwa sumu ya kuwamwaga damu
 
Hapo ndipo utaona mawazo ya wanadamu walivyo madogo kuliko ya yule aliyeumnba Mungu katoa hizi natural resources ili zifaidishe watu lakini zinageuka kuwa sumu ya kuwamwaga damu

Ndiyo maana ya uchaguzi. Unapewa dhamana na wananchi uwaongoze,na kuweka mifumo bora ya kuwaletea maendeleo,na kulinda rasilimali za Taifa kwa faida ya wananchi.
 
Wana hoja, hasa ya kujenga viwanda vya kuchakata, ila serikali yetu sikivu inaendeleza ubabe katika hili
 
Wananchi wa Mtwara na Lindi ni maskini kwa sababu ya Uislam wao. Uislam uko intertwined na umaskini, ujinga na maradhi.
 
hatutakubaliana na serikali ccm milele hata wakijenga power plant mtwara maana tushaona kama wababaishaji, kwanini hawatimizi wajibu wao wanabaki kufevor baadh ya sehemu 2?
 
Sasa viwanda vitawasaidia nini au ndio kazi za vibarua , coz vitaajiri wasomi ambao ni wachaga ,wahaya,wanyakyusa etc...... Mimi nadhani wangeomba wapewe vitu muhimu kama shule ,vyuo na mahospital. Lakini ajira bila elimu
 
Wananchi wa Mtwara na Lindi ni maskini kwa sababu ya Uislam wao. Uislam uko intertwined na umaskini, ujinga na maradhi.


:blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah::blah:
 
Back
Top Bottom