Mkutano wa Chadema M4C-Iringa wasitishwa!

Mkutano wa Chadema M4C-Iringa wasitishwa!

Inji hii bana

Kweli CCM ilikufa na mwalimu


Wanahangaika sana na Chadema
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mi naona wanataka wapae! Kutembea ni kosa, kupanda gari kosa!

Duuh ccm kazi wanayo!
 
Haya tena hata wakitembea ndani ya nchi yao wanawahofia? kwani msafara una viongozi gani?

Sikuweza kujua mara moja ila nilimuona dada mmoja mweupe akiwa amevaa magwanda alikuwa akibishana na polisi mmojawapo ambaye ndiye aliyekuwa kiongozi wao, msafara wenyewe niliuona haukuwa na magari mengi labda kama matano au sita tu... kama sikuona vibaya maana habari yenyewe ilikuwa fupi sana, lakini pia najiuliza ina maana sasa hata ikionekana gari ya ni kusimamisha tu au?
 
dah,[polis wananishangaza sana,sasa waliwataka hao chadema wapae na kujikuta wako ndani ya nyumba.
kweli polis wanaisaidia sana chadema kwenye harakati za ukombozi,
maana hata kama hukuwa na nia ya kufatilia chadema,inabidi tu ufatilie ili ujue hawa chadema kwanini wanapingwa hivi!


Halafu sasa wananchi wenyewe hawana uoga kabisa na polisi, maana walikuwa wanawazomea, polisi walikuwa wamebeba yale mabunduki yao ya mabomu na wamevalia tayari kwa kazi, CCm wakubali tu kwamba wananchi wamewachoka, wakubali kukaa pembeni wajifunze, hakuna haja ya kuwa na wasiwasi maana hata cdm nao wakichemsha tutawatoa.

Hii mimi naona ni sawa kwenda mahakami kupinga talaka wakati mke/mume hakutaki.
 
Polisi walikuwa wengi sana japokuwa tayari Dr. Slaa alikuwa ameshakubaliana nao kuwa CHADEMA itasitisha Operesheni kwa siku 5 kupisha sensa. Nafikiri huu ni Mpango wa Kamanda Chagonja kujipatia posho ili kitengo chake kionekane kina umuhimu. Maana bila kuwachokoza CHADEMA atalipwa posho za kazi gani?? Na hawa askari watapata wapi posho za safari na Mafuta???


Kamanda Chagonja kuwa creative na ubuni namna nyingine ya kupata posho za safari, service,mawasiliano,mafuta na sio kuitumia CHADEMA. Utakuwa ukisababisha vurugu na mauaji yasiyo na sababu kila siku. Maana jana hao FFU walilinda mkutano wa ndani wa CHADEMA na Diffender nne zilizojaa askari hadi saa 4 usiku. Hebu niambie huu sio utumiaji mbaya wa fedha za Wananchi???
Hali ilivyokuwa Mjini Iringa wakati Msafara wa Viongozi wa CHADEMA ulipoingia kuanza Operesheni - YouTube
 
Ipo siku polisi watajua KUWA walichelewa sana kujua ccm ni adui yao na familia zao. Angalia masiha yao? kama askari wa iringa ndio kabisa nyumba zao mbofu mbofu tu!!!!!!!
 
Yataisha tu hata nyerere alizuiwa hivyo hivyo.MUNGU ibariki Chadema,MUNGU ibariki Tz
 
Polisi wakisikia makamanda wa Chadema wameingia ktk eria yao basi matumbo jooto,hivi hawa polisi wanashinikizwa au wanajituma wao kuyafanya haya wanayoyafanya?Kwani Chadema wamekosa nini mpaka wazuiwe kuingia ktk ardhi ya nchi yao huko Iringa?

Hata police wanahitaji mabadiliko!Ongea nao kishikaji utawasikia wanavyotoa live!Wengine ni member humu Jf nawana hawataki kusikia utawala mbovu!Fb ndio wapo wengi,wanaponda mpaka noooma!
 
dah,[polis wananishangaza sana,sasa waliwataka hao chadema wapae na kujikuta wako ndani ya nyumba.
kweli polis wanaisaidia sana chadema kwenye harakati za ukombozi,
maana hata kama hukuwa na nia ya kufatilia chadema,inabidi tu ufatilie ili ujue hawa chadema kwanini wanapingwa hivi!

au tunatakakujua hawa cdm ni akina nani hasa au wale waliomkimbiza nduli idi amin.mbona wanatisha sana hawa watu ...!
 
Serikali ya Chama cha Mapinduzi inatumia gharama kubwa sana kuipa CHADEMA umaarufu. Aina maana kuleta au kusomba maaskali kutoka kutoka mikoa ya jirani kuwapeleka Iringa kwa ajili ya ulinzi na kuwapiga mabomu wana CHADEMA na viongozi wao.

CCM wanatakiwa kutafuta mbinu ya kujijenga na kujinusuru na aibu watakayoipata 2015 ingawa napenda na nina tamani sana hiyo aibu CCM waipate 2015.

Chadema ni noma
 
Nimejionea kwa macho yangu kupitia ITV jioni hii CDM wakiingia Iringa na
msafara wa magari 20. Wananchi wamejipanga barabarani bila hata ya kua
mbiwa wafanye hivyo na viongozi wa CDM....polisi walipotaka kuwatawanya
wananchi hao' wananchi waliwajibu polisi kwa sauti kubwa ya People'z power!

Kweli nimeamini Chadema ni nouma!....utaki unaacha
 
Nimeshangazwa na polisi kuzuia wakiwa na Silaha tu bila kuwa na ngao pamoja na vilungu inamaana wapo kwaajili ya kuua na si kazi nyingine
 
Salute CDM
scout%20salute2.jpg
 
Leo serikali kupitia jeshi la polisi imewazuia msafara wa CDM kuingia mjini Iringa kisa wananchi wamejipanga barabarani kwa mapenzi yao wenyewe na kusababisha kuvuta hisia ya wengi baada ya maafisa wa polisi kuzuia CDM wasitembee kwa miguu baada magari yao kuzuiwa. Kwa utaratibu huu hapa ni kama serikali imesaidia kufanya promotion ya M4C kwa kitendo cha kuzuia magari yao pia walipotaka kushuka kutembea kwa miguu pia wakazuiwa kwa hofu ya wananchi kuwashangilia ambao walijitokeza kwa hiari yao kama vile JK anavyopita sehemu nyingine za nchi na msafara na wananchi kujitokeza. Serikali inachotakiwa kuimarisha ulinzi na si kufanya kama ilichofanya leo haapo Iringa maana inawadhalilisha askari wa ngazi za chini wanashindwa kufanya maamuzi ama wawaruhusu waendelee na safari au la mpaka eti wapate maelekezo toka juu ambao hali halisi inayotokea eneo la tukio hawajaiona.
 
nimejionea kwa macho yangu kupitia itv jioni hii cdm wakiingia iringa na
msafara wa magari 20. Wananchi wamejipanga barabarani bila hata ya kua
mbiwa wafanye hivyo na viongozi wa cdm....polisi walipotaka kuwatawanya
wananchi hao' wananchi waliwajibu polisi kwa sauti kubwa ya people'z power!

Kweli nimeamini chadema ni nouma!....utaki unaacha

so what? Si jaona lolote jipya hapo. These are just normal things in politics and religion. Just get their emotions stirred up...peoples powers! Peoples power! You can get the same results or anything! It is a normal human response[mob psychology], especially when people are hungry and tired of the norms/status quo-same system. But the very same people kesho will take you to msalabani and say crucify him,crucify him, crucify him. Just wait, you will see it!
 
Back
Top Bottom