tarimemjini
Member
- Jul 10, 2025
- 71
- 142
Kutokana na hali ya joto na mivutano ndani ya CCM juu ya uteuzi wa watia nia watatu katika kugombea nafasi za Ubunge na udiwani imebidi mkutano mkuu maalum uitishwe kwa njia ya mtandao.
Madhumuni ya mkutano huo mkuu ni kutengua kanuni waliyoipitisha January 2025 juu ya mchakato wa uteuzi wa wagombea katika uwakilishi katika vyombo vya Dora.
Maandalizi yamekamilika ili mkutano huo mkuu utengue kanuni hiyo ili wagombea wote waliochukua fomu waingie katika kura za maoni.
Ikumbukwe hadi sasa kuna wagombea wanaozunguka na kugawa pesa kinyume na taratibu, kanuni na maagizo ya Chama.
Huu ni mtego kwa wagombea ambao hawaamini katika rushwa na uvunjifu wa kanuni za Chama.
Jambo hili likifanyika litazidi kuifanya CCM kuwa sehemu muhimu ya ufisadi na uhujumu uchumi.
Madhumuni ya mkutano huo mkuu ni kutengua kanuni waliyoipitisha January 2025 juu ya mchakato wa uteuzi wa wagombea katika uwakilishi katika vyombo vya Dora.
Maandalizi yamekamilika ili mkutano huo mkuu utengue kanuni hiyo ili wagombea wote waliochukua fomu waingie katika kura za maoni.
Ikumbukwe hadi sasa kuna wagombea wanaozunguka na kugawa pesa kinyume na taratibu, kanuni na maagizo ya Chama.
Huu ni mtego kwa wagombea ambao hawaamini katika rushwa na uvunjifu wa kanuni za Chama.
Jambo hili likifanyika litazidi kuifanya CCM kuwa sehemu muhimu ya ufisadi na uhujumu uchumi.