Mkurugenzi wa TAKUKURU (Dr. Hosea) mgonjwa, yuko nje ya nchi kwa matibabu

Status
Not open for further replies.
*Yuko nje ya nchi kwa matibabu
*Waziri Mkuchika akataa kusema lolote
* Manumba aendelea kupumulia mashine
 
Ugonjwa wa mtu ni siri yake na wanaomuuguza jamani. Ni mpaka yeye mwenyewe aamue kudisclose! Kwa upande wangu sina haja ya kujua wanaumwa nini zaidi ya kujua anaendeleaje. Hawa ni tofauti na mwakyembe aliyedai kulishwa sumu hivyo ilitakiwa mambo yawekwe hadharani ili kuclear public doubts. Aafu watu waovu utawajua tu, hawajiamini na hawaamini wenzao. Huwezi muondoa mtu muhimbili na kumpeleka agha khan aafu muda huo huo unachukua madaktari wa muhimbili wakamtibu huko! Ni kwa uovu waliomfanyia ulimboka wataendelea kuishi maisha ya wasiwasi kila wanapougua. Ukimuuliza miraji leo atakueleza umuhimu wa madaktari wa muhimbili.!
 
Hawa wajamaa wawili ndo walitakiwa wachunguzi yale mabilioni yaliyofichwa uswiss. Ama wao ni mojawapo walioficha pesa au wahusika wanapambana
 
hawa si ndio wenyewe tukiwaambia kunaufisadi wanatuambie tupeleke ushaidi ni ngumu hata kuwaombea mema!
 
Usihukumu usije hukumiwa ww..mwil ni maua tu

kama unalijua ili iweje wao wasilijue? Hawakupewa madaraka makubwa hivyo kuwahukumu ws tzn visivyo! Hawa wawili wamekuwa mwanvuli wa kuficha uvundo wa rushwa na ufisadi zidi ya vigogo. Siku nyingi nimejiuliza Hossea amesaidia nini taifa hili..tumkumbuke kwa lipi?
 
Dhambi ya EPA, KAGODA, DEEP GREEN na kadhalika zote zitawatafuna. Hakuna mtu anayejua what these bigs wigs wanasumbuliwa nacho but watu wanaweza kupotea hivi hivi kimzaha kupoteza siri za madhambi ya SISIEMU ENTERPRISES. I DON'T FEEL SORRY AT ALL.
No offense intended kwa mtu yoyote but watu wanaweza kuzimishwa tu ili tembo aendelee na safari yake.
 
Mungu amjaalie arejee afya yake njema.
Mbona hawakumpeleka Muhimbili?

lol. Siku hizi Muhimbili nako kuna sehemu ya mapunziko kwa ajili ya likizo?

Kimisingi hii habari imekaa kiudaku zaidi. Kwanza kichwa cha habari kinakinzana na habari yenyewe.

Aya moja inasema yuko nje ya nchi kwa matibabu. Aya nyingine inadai yuko nje ya nchi kwa mapunziko ya likizo.

Which is which? Si heri wangekaa kimya tuu na kuchunguza kwanza ili kujua alipo na kwa sababu gani yupo hapo?

Halafu gazeti linatamba kuwa limepata hizo habari zinazokingana kutoka vyanzo vya kuaminika ndani ya TUKURURU.
 
Kauli zinazotolewa na baadhi yetu humu eti sijui "afe fasta" sijui apumzike jehanam", huu ni upumbavu na ni dalili ya laana. Tukumbuke sisi sote ni nyama na mavumbi tu na ipo siku tutapatwa na maladhi na pengine kupona ama kufa.. U- DCI ama U-Takukuru wa Hosea visiwe vigezo vya kuwaombea mabaya. Tuombeane mema enyi kizazi cha nyoka mnaoongozwa na nyoka mkuu chadema ingawa hamjitambui. Poleni maana laana i nyuma yenu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom