PostGE2025 Mkurugenzi wa ELAF, Hamis Masoud: Wanaotoa kauli za Udini wachukuliwe hatua

PostGE2025 Mkurugenzi wa ELAF, Hamis Masoud: Wanaotoa kauli za Udini wachukuliwe hatua

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Mkurugenzi wa Kituo cha Usaidizi wa Kisheria cha Everlasting Legal Foundation (ELAF), Dkt. Hamis Masoud, amelaani vikali lugha za uchochezi wa kidini, akisisitiza kuwa kama tunakwenda kwenye hatua ya maridhiano hatupaswi kutengeneza vita mpya ya migogoro ya kidini, akisisitiza kuwa Watanzania wanasimama kama taifa, wenye dini na wasio na dini wanaunganishwa na undugu ambao ni ubinaadamu

Akizungumza na waandishi wa habari, jana Novemba 23, 2025 katika makao ya Ofisi hizo jijini Dar es Salaam, Dkt. Masoud amesema mijadala ya Kitaifa inapaswa kuheshimu imani za watu wote, na si sahihi kutumia dini kama silaha ya kuudhalilisha au kuchochea migawanyiko katika jamii.

Amekemea matamshi yanayotolewa na baadhi ya viongozi wa dini na wahadhiri ambayo yamekuwa yakihamasisha vurugu, ikiwemo vitisho vya mashambulizi kwenye nyumba za ibada

Amesema vitendo hivyo vinakiuka sheria za nchi, hususan sheria za makosa ya jinai, hivyo hatua kali zinapaswa kuchukuliwa mara moja ili kuzuia madhara makubwa kwa ajili ya amani ya taifa.

Dkt. Masoud ametahadharisha kuwa taifa linaweza kuingia katika migogoro ya udini endapo hatua za kisheria hazitachukuliwa kwa wakati, akisisitiza kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria.

Aidha, ameitaka sekta ya umma kutimiza wajibu wake kwa kuzingatia maslahi ya taifa, akibainisha kuwa mamlaka wanazoshikilia viongozi zinatokana na wananchi na lazima zitumike kwa uadilifu.

Amesisitiza kuwa lengo la kauli zake ni kulinda umoja, mshikamano na amani ya taifa, huku akiwakumbusha viongozi wote kwamba mamlaka hutoka kwa Mungu na yanapaswa kutumiwa kwa uangalifu mkubwa.

Dkt. Masoud amelitaka tena Jeshi la Polisi kuchukua hatua dhidi ya wote wanaotoa matamshi ya uchochezi wa kidini, akisema kuwa endapo Jeshi la Polisi halitachukua hatua stahiki, watamshauri Rais kuchukua hatua dhidi ya viongozi wa usalama wanaoshindwa kutekeleza majukumu yao


 
Mkurugenzi wa Kituo cha Usaidizi wa Kisheria cha Everlasting Legal Foundation (ELAF), Dkt. Hamis Masoud, amelaani vikali lugha za uchochezi wa kidini, akisisitiza kuwa kama tunakwenda kwenye hatua ya maridhiano hatupaswi kutengeneza vita mpya ya migogoro ya kidini, akisisitiza kuwa Watanzania wanasimama kama taifa, wenye dini na wasio na dini wanaunganishwa na undugu ambao ni ubinaadamu

Akizungumza na waandishi wa habari, jana Novemba 23, 2025 katika makao ya Ofisi hizo jijini Dar es Salaam, Dkt. Masoud amesema mijadala ya Kitaifa inapaswa kuheshimu imani za watu wote, na si sahihi kutumia dini kama silaha ya kuudhalilisha au kuchochea migawanyiko katika jamii.

Amekemea matamshi yanayotolewa na baadhi ya viongozi wa dini na wahadhiri ambayo yamekuwa yakihamasisha vurugu, ikiwemo vitisho vya mashambulizi kwenye nyumba za ibada.

Amesema vitendo hivyo vinakiuka sheria za nchi, hususan sheria za makosa ya jinai, hivyo hatua kali zinapaswa kuchukuliwa mara moja ili kuzuia madhara makubwa kwa ajili ya amani ya taifa.

Dkt. Masoud ametahadharisha kuwa taifa linaweza kuingia katika migogoro ya udini endapo hatua za kisheria hazitachukuliwa kwa wakati, akisisitiza kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria.

Aidha, ameitaka sekta ya umma kutimiza wajibu wake kwa kuzingatia maslahi ya taifa, akibainisha kuwa mamlaka wanazoshikilia viongozi zinatokana na wananchi na lazima zitumike kwa uadilifu.

Amesisitiza kuwa lengo la kauli zake ni kulinda umoja, mshikamano na amani ya taifa, huku akiwakumbusha viongozi wote kwamba mamlaka hutoka kwa Mungu na yanapaswa kutumiwa kwa uangalifu mkubwa.

Dkt. Masoud amelitaka tena Jeshi la Polisi kuchukua hatua dhidi ya wote wanaotoa matamshi ya uchochezi wa kidini, akisema kuwa endapo Jeshi la Polisi halitachukua hatua stahiki, watamshauri Rais kuchukua hatua dhidi ya viongozi wa usalama wanaoshindwa kutekeleza majukumu yao.
 
Eti kama lile sheikh linasema "tutachinjana" lau kama amgekuwa anaipinga serikali yule saa hizi hajulikani alipo
 
Hamjambo wote!

1. Ipigwe marufuku na iundwe Sheria kuwa wewe ukiwa Dini Fulani ni jinai kuisema au kuiponda au kuikosoa Dini nyingine.
Mfano Mimi Msabato ni Marufuku kuwasema Wakatoliki sijui mafundisho ya papa ni mnyama. Sijui kuwasema waislam ipigwe marufuku.

2. Kama ni muislam owe marufuku kuwasema Wakristo. Vivyohivyo kwa Wakristo kuwasema waislam.

3. Wewe kama ni muislam Baki na dini yako ya kiislam na hubiri uislam wako bila kutaja dini na madhehebu mengine. Hasa kuyakosoa au kukejeli.

4. Wewe kama ni Mkristo iwe jinai kutaja au kukejeli waislam kwa namna yoyote Ile.

5. Uhuru wa kuabudu sio kukejeli dini za watu. Imani ni suala la mtu binafsi.

6. Viongozi wa dini madai Yao yapelekwe kwa serikali na waishutumu serikali kwa sababu yenyewe ndio ipo na wajibu wa kutoa huduma mbalimbali.

7. Maana halisi ya kuingiza siasa kwenye Dini ndio huko sasa.

8. Viongozi wa Dini kuiponda au kuikosoa serikali au kuishauri serikali huko sio kuingiza siasa kwenye Dini.

9. Ila viongozi wa Dini kutaka kushinikiza serikali na kutaka kupata ushawishi kwenye serikali kuliko Dini nyingine huko ndiko kuingiza siasa kwenye dini.

10. Tayari ipo chuki ya kisiasa baina ya vyama vya upinzani hasahasa Chademw na CCM.
Viongozi na mashabiki wa chadema wamejikuta wakinyimwa amani ndani ya taifa hili Jambo ambalo limechangia jwa kiasi kikubwa Yaliyotokea 29 October

11. Sasa kuongeza Chuki nyingine za kidini kwa kuwapa airtime viongozi wa Dini kurusha maneno kwa dini zingine ni kuchochea chuki isiyo na sababu.

12. Viongozi watoe madai yao bila kutaja wala kuhusisha dini zingine.

13. Chuki isipewe nafasi. Na mbinu za kushughulika nayo isiongeze ufa.

Ni hayo tuu!

TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
 
Hamjambo wote!

1. Ipigwe marufuku na iundwe Sheria kuwa wewe ukiwa Dini Fulani ni jinai kuisema au kuiponda au kuikosoa Dini nyingine.
Mfano Mimi Msabato ni Marufuku kuwasema Wakatoliki sijui mafundisho ya papa ni mnyama. Sijui kuwasema waislam ipigwe marufuku.

2. Kama ni muislam owe marufuku kuwasema Wakristo. Vivyohivyo kwa Wakristo kuwasema waislam.

3. Wewe kama ni muislam Baki na dini yako ya kiislam na hubiri uislam wako bila kutaja dini na madhehebu mengine. Hasa kuyakosoa au kukejeli.

4. Wewe kama ni Mkristo iwe jinai kutaja au kukejeli waislam kwa namna yoyote Ile.

5. Uhuru wa kuabudu sio kukejeli dini za watu. Imani ni suala la mtu binafsi.

6. Viongozi wa dini madai Yao yapelekwe kwa serikali na waishutumu serikali kwa sababu yenyewe ndio ipo na wajibu wa kutoa huduma mbalimbali.

7. Maana halisi ya kuingiza siasa kwenye Dini ndio huko sasa.

8. Viongozi wa Dini kuiponda au kuikosoa serikali au kuishauri serikali huko sio kuingiza siasa kwenye Dini.

9. Ila viongozi wa Dini kutaka kushinikiza serikali na kutaka kupata ushawishi kwenye serikali kuliko Dini nyingine huko ndiko kuingiza siasa kwenye dini.

10. Tayari ipo chuki ya kisiasa baina ya vyama vya upinzani hasahasa Chademw na CCM.
Viongozi na mashabiki wa chadema wamejikuta wakinyimwa amani ndani ya taifa hili Jambo ambalo limechangia jwa kiasi kikubwa Yaliyotokea 29 October

11. Sasa kuongeza Chuki nyingine za kidini kwa kuwapa airtime viongozi wa Dini kurusha maneno kwa dini zingine ni kuchochea chuki isiyo na sababu.

12. Viongozi watoe madai yao bila kutaja wala kuhusisha dini zingine.

13. Chuki isipewe nafasi. Na mbinu za kushughulika nayo isiongeze ufa.

Ni hayo tuu!

TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
Wakati Mukuuu kageuka mchochezi wa udini!
 
Na ikiwa hivyo Kuna watu watapotea kwenye midia za bongo
Maana wao wakiitisha press tu A_Z ni kuisema dini nyingne ambayo ata haijawahi kuwasema mahali popote
 
Kwa ubaya au kwa maana ya kuidunisha na haya yaingie kwenye katiba mpya tuliyo ahidiwa mchakato wake kuanza ndani ya siku mia za kwanza za utendaji wa sirikali ya muhuli yapili ya awamu ya sita!

Ndio. Kuna mambo yasipowekewa mkazo yatatuletea shida huko mbeleni
 
Serikali izuie na kupiga marufuku mtu wa dini moja kuisema Dini nyingine inachochea Chuki na kuhatarisha usalama wa nchi. Iwe Jinai.
Tatizo ni watawala. Wakiona wamekabwa na maswali magumu wakakosa majibu, wanakodi wahuni na kuwalipa pesa ili wachomekee udini ili mambo muhimu ya kitaifa yasijadiliwe
 
Mkuu wa serikali ndiye mwanzilishi wa kupandikiza chuki za kidini. Sasa serikali gani unayoishauri?
 
Back
Top Bottom