Mkurugenzi Mkuu VETA: Hata wenye PhD wanakaribishwa VETA

Mkurugenzi Mkuu VETA: Hata wenye PhD wanakaribishwa VETA

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Anthony Kasore amesema kuwa sio tu wenye Shahada ya Awali, hata wenye elimu za juu zaidi kama vile Shahada ya Uzamivu (PhD) wanaweza kujiunga VETA, na wamewahi kuwa na mwanafunzi mwenye PhD ambaye amesomea masuala ya uchomeleaji.

Soma: Waziri Mkuu Majaliwa: Wenye degree kasomeni ufundi VETA mjiajiri

Akizungunza kwenye Kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo Machi 17, 2025, Kasore amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma za elimu ya ufundi hasa miundombinu na kuwahimiza watu wote wanaohitaji kupata ujuzi wajiunge na vyuo vya VETA vinavyopatikana katika maeneo mbalimbali nchini.

 
Mimi kama kijana wa kitanzania nilijiunga na VETA licha ya kuwa nilikuwa na taaluma zangu zingine nilizohitimu awali. Sikuona kwa nini nina elimu kubwa halafu nikachanganyikane na vijana niliowazidi elimu nisomee ufundi. Elimu ya ufundi haijali una wajihi gani na haina mipaka, soko lake liko wazi. Wanachotakiwa VETA ni kuongeza wigo wa mafunzo yao na kuongeza fani za kusomea kulingana na mahitaji na muda huu wa kukua kwa sayansi na teknolojia, nadhani watafiti wa VETA wanalijua hili, Muda mfupi ujao VETA itakuwa na wanafunzi wengi wa fani mbalimbali
 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Anthony Kasore amesema kuwa sio tu wenye Shahada ya Awali, hata wenye elimu za juu zaidi kama vile Shahada ya Uzamivu (PhD) wanaweza kujiunga VETA, na wamewahi kuwa na mwanafunzi mwenye PhD ambaye amesomea masuala ya uchomeleaji.

Soma: Waziri Mkuu Majaliwa: Wenye degree kasomeni ufundi VETA mjiajiri

Akizungunza kwenye Kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo Machi 17, 2025, Kasore amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma za elimu ya ufundi hasa miundombinu na kuwahimiza watu wote wanaohitaji kupata ujuzi wajiunge na vyuo vya VETA vinavyopatikana katika maeneo mbalimbali nchini.

Dharau zimezidi sasa
 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Anthony Kasore amesema kuwa sio tu wenye Shahada ya Awali, hata wenye elimu za juu zaidi kama vile Shahada ya Uzamivu (PhD) wanaweza kujiunga VETA, na wamewahi kuwa na mwanafunzi mwenye PhD ambaye amesomea masuala ya uchomeleaji.

Soma: Waziri Mkuu Majaliwa: Wenye degree kasomeni ufundi VETA mjiajiri

Akizungunza kwenye Kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo Machi 17, 2025, Kasore amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma za elimu ya ufundi hasa miundombinu na kuwahimiza watu wote wanaohitaji kupata ujuzi wajiunge na vyuo vya VETA vinavyopatikana katika maeneo mbalimbali nchini.

Aibu naiona mimi Tanzania, kutoka zama za Specialization mpaka zama za ujima wa Jack of all traders. Yaani mtu usome mpaka PHD alafu uende Veta ? Kwann asingemaliza la nne akaenda Veta ?
 
Nataka nirudi VETA tena kwenda kusomea ufundi mwingine tena ili niweze kufanya shughuli nyingi. Wenzetu wachina wako mbele zaidi na wanatuonesha ufundi wao kwenye Tik Tok yao kwa nini sisi tudharau elimu ya ufundi itolewayo na VETA? Mind kwamba sie wengine tunaoenda VETA kusomea ufundi tuna elimu na taaluma zingine tulizohitimu vyuoni, kwa hiyo tuna vyeti vingi, ni multi purpose katika kulitawala soko la ajira na kuondoa mentality ya ajira ni chache.
 
Dah! taifa linatia huruma ya mtu aache PI,consultancy service,lecturers, for what?
veta mbona inawahitimu wasio na ajira badala serikali ya serikali kuwapa mikopo inapambana kujustify statement za kichawa waige china kwa maendeleo hasa sera yao road and belt initiative na sio kuwaiga kwa siasa kandamizi zisizo na tija kwa taifa.
 
Nataka nirudi VETA tena kwenda kusomea .........
Nukuu: "kwa nini sisi tudharau elimu ya ufundi itolewayo na VETA"?
Mkuu; Hapana -hakuna aliyeidharau elimu itolewayo na VETA ila Wadau hawajakubaliana na alichokisema (kauli) ya PM.
 
Kwanini isiwe kila shule ya msingi mpaka olevel veta inamtaala wake humo? Kuanza kusumbua watu wazima Sasa kulikoni?
 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Anthony Kasore amesema kuwa sio tu wenye Shahada ya Awali, hata wenye elimu za juu zaidi kama vile Shahada ya Uzamivu (PhD) wanaweza kujiunga VETA, na wamewahi kuwa na mwanafunzi mwenye PhD ambaye amesomea masuala ya uchomeleaji.

Soma: Waziri Mkuu Majaliwa: Wenye degree kasomeni ufundi VETA mjiajiri

Akizungunza kwenye Kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo Machi 17, 2025, Kasore amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma za elimu ya ufundi hasa miundombinu na kuwahimiza watu wote wanaohitaji kupata ujuzi wajiunge na vyuo vya VETA vinavyopatikana katika maeneo mbalimbali nchini.

Yeye ana PhD?
 
Back
Top Bottom