Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Mikopo na wengine watatu wasimamishwa kazi

Brigedia Chan-ocha

JF-Expert Member
Mar 7, 2014
1,353
2,842
ndalichako.jpg


Waziri wa Elimu Sayansi, Teknolojia na ufundi, Prof Joyce Ndalichako amesitisha mkataba wa kazi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo George Nyatenga (Pichani chini).

Pia amewasimamisha kazi Wakurugezi watatu wa Bodi hiyo ambao ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala Yusufu Kisare, Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo Juma Chagonja na Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo.

Prof. Ndalichako amemwagiza Mkaguzi wa ndani Mkuu wa Serikali ahakiki maelezo na Nyaraka zilizowasiliwa na Bodi ya Mikopo pamoja na kufanya ukaguzi maalum kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013 hadi sasa.

Amewateua wafuatao ku Kaimu nafasi; Kaimu Mkurugenzi Mtendaji mteule ni Bw. Jerry Sabi kutoka Mzumbe University na Kaimu Mhasibu Mkuu mteule ni Bw. Daniel Mafie kutoka NECTA
 
Good ....wamechezea sana wadogo zetu.

kodi zetu....mikopo walikuwa hawatoi kutwa kucha kuwazunguusha.

watoto wakiandamana wanapigwa mabom na kufukuzwa vyuoni............

Ninafuhia sana kuona serikali inafanya kwa vitendo.....Decision making and actioning.

............................
 
Pesa za field zilicheleweshwa sana mpaka wengine wameenda field bila pesa. Hiyo imewakuta wanafunzi wa mwecau walioenda teaching practice! Kuna wengine mpaka sasa hawajapewa hizo pesa na wakp field, sijui wanaishije!
 
Mwaka huu noma kwa watumishi wa serikali. Kasi ya Kikwete ndio imewaponza mkawekeza kwenye ufisadi na kusahau weledi...

Ngoja nicheki brela kama hawajafuta kale ka kampuni kangu ka kufundisha ujasiliamali, naweza kupata sana wateja mwaka huu kwa hali ilivyo maana hawa jamaa walizoea mahela marefu ya kwenye vikao vya bodi wataweza kweli kusubiri hadi nyuki atoe asali ndio wapate hela? Au kusubiri kuku watage mayai, au mpunga ukomae ndio wauze. Nichangamkie fursa
 
Ndalichako wewe mama ni jembe hawa jamaaa wazembe sana nimeandika maandiko humu mengi kuishauri taasisi hiii hatimaye mama ndalichako kasikia hongera sana mama mungu akubariki lakini wanafunzi mikopo yetu wa mwaka wa kwanza iloenda sehemu nyingine mikopo yetu tumepata allocation malipo bado(means chip bado hakijaingiziwa boom na chuo ili tusaini) Hongera mama
 
Hii kasi itakuja kuwaadhiri sana walionufaika na mikopo ambao wanafanya kazi sekta binafsi. Kwa style hii nao wataanza kulipa. Mm niligraduate 2010 na wananidai around 7m ila kwasababu nipo private sijaanza kulipa.

Duc in Altum
 
Jamani hivi hawa watu kweli hawaji kututia hasara ya kufidiwa huko mbele ya safari maana nahofu kama mahakama haitawapata na hatia? maana wanaobgezeka tu kila kukicha. Lakini bora ''something is happening''
 
Back
Top Bottom