Mkuranga: Mtendaji wa Kijiji cha Mjawa, mwanakijiji mmoja wauawa

tejateja

JF-Expert Member
Feb 26, 2015
1,619
969
Mtendaji wa kijiji cha Mjawa na mwanakijiji mmoja wameuawa na wale maharamia walioua askari nane majuzi.

Hili tatizo ni kubwa mno, Serikali, vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vitumie umakini wa hali ya juu kutafuta suluhisho. Tena mapema.

TETESI.
 
Hii habari ya lini wakuu? Duh, juz walisema wameua majambazi 4 baada ya lile tukio,basi wako wengi sana hao majambazi. Mungu ibariki Tanzania.
 
Mtendaji wa kijiji cha mjawa na mwanakijiji mmoja wameuwawa na wale maharamia walouwa askari nane majuzi.
Hili tatizo ni kubwa mno na serikali na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama , vitumie umakini wa hali ya juu kutafuta suluhisho. Tena mapema ,
wewe tejateja huyo mtendaji si aliuwawa kipindi cha nyuma? au ni mwingine?
 
Tulia wewe, mbona unatoa taarifa kimwendokasi, au ni ili uwe wa kwanza kuileta humu?
Weka nyama taarifa yako mkuu!
 
Msipende kutuzingua. Wewe unalijua usemalo au unavuta zikiwa mbichi?? Angalieni jamani, bado ile sharia ya cyber crime ipo. Serekali haitavumilia maneno ya uchochezi kama haya. Wataka kutuaminisha kuwa wale majambazi 4 waliouliwa juzi kwa mpambano wamefufuka?? Msiwafanye wananchi wateswe na polisi hadi wawataje walipo nyiye.
 
Magaidi ndiyo wana tabia ya kushambulia soft spots, yaani wananchi wasio na silaha, wanawake au watoto.
Kwa hili binafsi naamini hawa ni magaidi, nisidanganywe kwamba ni majambazi.
 
Back
Top Bottom