Mkullo: Maisha yangu yako hatarini!

..kwanini anataka akodi ndege kisirisiri?

..kwanini kuwe na usiri ktk matumizi ya fedha za walipa kodi?

..kwanini anafikiri maisha yake yako hatarini ikiwa anatekeleza majukumu yake kwa haki na uadilifu?

Just when others are fighting to have transparency in their governments, ours is preaching opacity... what bunch of loosers are leading this country...
 
Jamani ccm haihusiki, hili ni ni suala la Serikali kupitia wizara ya fedha

Asingekua hapo kama hakupata ubunge kupitia mlango wa CCM. Kwani kulikua hamna mbunge mwingine wakugombea huko kupitia hiki chama anayejali watu kuliko huyu? Au ndio mambo ya Masha yakupita bila kupingwa! Kati ya wabunge wote wa CCM Kikwete hakuona mtu mwenye uchungu na rasilimali za nchi anayeweza kuwa waziri wa fedha zaidi ya huyu? Si ameshafanya naye kazi for sometime ameona utendaji wake: au na Kikwete ni wale wale. It is real hard kuwatofautisha hawa watu, they always connect directly or indirectly kwa uwezo wao wakufikiri, na matendo yao.
 

Huyu jamaa ni fisadi mkubwa na hana uchungu na nchi hii kwa sababu si raia.
Angalia hata huko Kilosa ambapo yeye ni mbunge. Watu walipata janga la mafuriko wakapoteza mali, nyumba, mifugo na hata makazi.

Chanzo cha mafuriko hayo kilikuwa ni uzembe wa viongozi ambapo mkullo akiwa mbunge wa jimbo hilo ni mmoja wao. Viongozi walishindwa kufanyia matengenezo bwawa la kupunguza nguvu ya maji ya mto mkondoa ambao ulitiririsha maji yake kuelekea makazi ya watu.
Kingo za mto huo pia zilikuwa zimeharibiwa vibaya kwa muda mrefu hivyo nilitarajia viongozi wangechukua hatua za tahadhari mapema, lakini badala yake waliendelea kusinzia hadi watu walipopata maafa makuu.

Hata baada ya maafa Bw. Mkullo hakuonekana kutilia maanani janga hilo bali muda mwingi alikuwa Dar es salaam huku akisubiri kupewa taarifa za kwenda kupokea misaada ndio aende ili akauze sura na kuonekana kana kwamba yeye ndio ametoa hiyo misaada.

Serikali iliahidi kwa nyakati tofauti tofauti kuwalipa fidia na kuwajengea nyumba wale wote walioathirika lakini hadi leo hakuna lolote lililofanyika.
Watu waliandikishwa majina na kuahidiwa kupewa viwanja lakini hadi leo hakuna kitu. Je hii ni aina ya viongozi tunaowahitaji katika taifa letu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…