Mkopo wa milioni 10

Mkopo wa milioni 10

Mtendaji wa kaya

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2014
Posts
334
Reaction score
59
Naleta swali la ndugu yangu ambaye ni
mwajiriwa miezi miwili sasa! mshahara wake ni
laki sita na hamsini na ushee hela za kitanzania!
anataka kuomba mkopo wa milioni 10 benki
yoyote japokuwa mshahara wake unapitia
NMB,kama nilivyosema ana miezi miwili tu
kwenye utumishi! je anaweza kupata kiasi hicho
cha pesa kwa haraka? riba yake ni kiasi gani na
kama si benki ni wapi anaweza kupata mkopo
huo kwa riba nafuu? Lengo la mkopo ni kununua
gari! Nawasilisha
 
1.mkopo kununua gari,it's nt a nice idea.
2. ana muda mfupi kwenye ajira si rahisi akubaliwe.
3. kila bank wana riba zao, hazifanani.
 
Huyo mwambie asubiri mpaka apate comfirmation letter i.e apate utambulisho rasmi kuwa ni mwajiriwa wa serikali. Nafikiri ni baada ya miaka miwili kwa permanent government employement.
Hata hivyo sizani kama anaweza kupata kiasi hicho chote.
Pia kuchukua mkopo kwajili ya kununua gari ni ulimbukeni usio na maana. Mwambie asikubari kuendekeza utumwa, huo mshahara ni mdogo sana kama ataendekeza mikopo isiyo na tija maisha mazuri atayasikia kwenye radio na kuyashudia kwa majirani.
 
mkuu umepost thread mbili kwa mada moja:
mkuu huyo mtu mwenye ajira ya miezi miwili bado ni trainee au tuseme yuko kwenye probation period ivo kiutaratibu si mfanyakazi kamili na ivo hawezi kupata mkopo benki kwa dhamana ya mwajiri mpaka awe amethibitishwa kazini.
Lazima afanye kazi miezi kadhaa ili athibitishwe kazini...ivo sitegemei kama ataweza kupata huo mkopo bila kudhibitishwa kazini na iyo uthibitisho si chini ya miezi 6 au 12
Pia mwajiri hawezi kumdhamini mkopo wa milioni 10 mwajiriwa wa miezi2 na zaidi ya apo, mshahara wa laki6 ili alipe mkopo ndani ya miaka 3 (36moths au less) kama benki nyingi wanavofanya plus interest itabidi akatwe si chini ya laki 3 na ushee benki, je ataishi vipi kama akinunua gari?

Ushauri wangu ni kuwa awe na subira, baada ya mwaka mmoja mpaka miwili anaweza kuanza kuwaza ivo , vinginevo sijui kama kuna mwajiri au/benki itamsikiliza
 
Asubiri TSD No. alafu sio vizuri kutumia mkopo kununua liability anunue asset au aanzishe investment.
 
mkuu, sio lazima upate barua ya uthibitisho kazini (employment confirmation letter) ndipo upate mkopo. benki za CRDB na NBC ndio tu huhitaji hiyo document. benki ya NMB hawana hiyo complication--wao wanataka barua ya ajira tu--ambayo hutolewa pindi uajiriapo. wasiwasi wangu ni kwamba mwajiri hawezi kuidhinisha mkopo wako ikiwa bado hujamaliza probation ya mwaka 1.
 
mkuu, sio lazima upate barua ya uthibitisho kazini (employment confirmation letter) ndipo upate mkopo. benki za CRDB na NBC ndio tu huhitaji hiyo document. benki ya NMB hawana hiyo complication--wao wanataka barua ya ajira tu--ambayo hutolewa pindi uajiriapo. wasiwasi wangu ni kwamba mwajiri hawezi kuidhinisha mkopo wako ikiwa bado hujamaliza probation ya mwaka 1.

hapana labda nmb kwenu lkn wanataka hyo barua juz tu mtu kaenda katakiwa barua ya uthibitisho.
 
mkuu, sio lazima upate barua ya uthibitisho kazini (employment confirmation letter) ndipo upate mkopo. benki za CRDB na NBC ndio tu huhitaji hiyo document. benki ya NMB hawana hiyo complication--wao wanataka barua ya ajira tu--ambayo hutolewa pindi uajiriapo. wasiwasi wangu ni kwamba mwajiri hawezi kuidhinisha mkopo wako ikiwa bado hujamaliza probation ya mwaka 1.

teh teh teh una ongea vitu usivyo vijua wewe......
 
kwa mkopo wa NMB kinachotakiwa ni barua ya ajira na si ya kuthibitishwa kazini lkn wasiwasi wangu ni kuwa miezi miwili tu kazini anataka gari asije akakimbia kazi kwa madeni mana inaonekana ana haraka ya maisha na laki sita na nusu anaona nyingi sana.
 
Mi nakushauri tafuta hizi gari ambazo watu wanauza used Tanzania..mfano kwenye mtandao Wa zoom..unaweza kupata gari ndogo kwa bei ndogo hadi milioni 6..alafu hiyo milioni nne nunua kiwanja Mdogo Wangu...kumbuka kuhudumia gari kwa mshahara wa laki sita ni ngumu sana...
 
  • Thanks
Reactions: KUN
Nmb ukiwa na salary slip ya mwisho tu unachukua mkopo..na riba yao iko poa...
 
Yupo mtu sina hakika ni wa benki gani anaitwa bob rama atamsaidia kupata huo mkopo nina hakika namba yake ni 0715293293 wasiliana nae
 
Naleta swali la ndugu yangu ambaye ni
mwajiriwa miezi miwili sasa! mshahara wake ni
laki sita na hamsini na ushee hela za kitanzania!
anataka kuomba mkopo wa milioni 10 benki
yoyote japokuwa mshahara wake unapitia
NMB,kama nilivyosema ana miezi miwili tu
kwenye utumishi! je anaweza kupata kiasi hicho
cha pesa kwa haraka? riba yake ni kiasi gani na
kama si benki ni wapi anaweza kupata mkopo
huo kwa riba nafuu? Lengo la mkopo ni kununua
gari! Nawasilisha

Mamaye zake hana akili.
Yeye miezi 2 anawaza gari la 10m.
Mwambie asote kwanza hiyo 6 laki si pesa
 
Mamaye zake hana akili.
Yeye miezi 2 anawaza gari la 10m.
Mwambie asote kwanza hiyo 6 laki si pesa

Vijana mnapenda kujionesha! Eti miezi miwili kazini mburura anawaza gari, hovyo kabisa! Mshahara wenyewe laki 6 anaona amepaaaaata! Kazi tunayo!!
 
Wadau wengi hapa naona mnamponda badala yakutoa ushauri! Sio vizur asee
 
Asubiri TSD No. alafu sio vizuri kutumia mkopo kununua liability anunue asset au aanzishe investment.
. Watu kama nyie ndiyo huwa mnadanganya watu Gari ni asset inayo depreciate compared na asset kama nyumba inayo appreciate na ndiyo maana inakubalika benki kama dhamana. investiment nayo ni liability mpaka itakapoanza kutoa faida.
 
Hiyo laki sita ni baada ya makato au ndo mshahara wote? Kwa maelezo ya uhakika niliyoyapata NMB nilipoitembelea wiki hii, hesabu rahisi ya kujua kiasi gani unachoweza kukopa mkopo wa mshahara ni sawa x20 take-home yako (+/- kidogo sana).
Masharti muhimu ni kupeleka barua ya kuajiriwa, barua kutoka kwa mwajiri wako (bosi wa kituo chako cha kazi; sio barua ya uthibitisho kazini) na salary slips za miezi mi3 ya karibuni!!
Nikiangalia masharti japo mepesi kabisa sioni ni jinsi gani utayatimiza...ndio kwanza una miezi miwili, slips za miezi mitatu utazitoa wapi?
Ushauri wa bure:
Kaa chini utafakari mara ya pili kama una hitaji la gari kiasi hicho. Ongea na seniors wako ofisini wenye magari upate picha ya kuhudumia gari pale utakapokua umeanza makato! Nina hakika kuna jambo zuri zaidi ya gari. Kuchukua mkopo na ukafanyia jambo la kuzalisha utaona uzuri wa kazi, upande wa pili itakua majuto mpaka makato yaishe (3, 4 hadi miaka 5). Kaa tafakari vizuri.
 
Back
Top Bottom