Onduru Ogy
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 1,136
- 1,179
Naleta swali la ndugu yangu ambaye ni
mwajiriwa miezi miwili sasa! mshahara wake ni
laki sita na hamsini na ushee hela za kitanzania!
anataka kuomba mkopo wa milioni 10 benki
yoyote japokuwa mshahara wake unapitia
NMB,kama nilivyosema ana miezi miwili tu
kwenye utumishi! je anaweza kupata kiasi hicho
cha pesa kwa haraka? riba yake ni kiasi gani na
kama si benki ni wapi anaweza kupata mkopo
huo kwa riba nafuu? Lengo la mkopo ni kununua
gari! Nawasilisha
Wasikuzingue hao watu wanaokosoa Mipango yako ya pesa..
kila mtu anayo vipaumbele vyake kwenye maisha..
wakati wengine wanataka pesa kwa ajili ya mahari, wengine wanataka pesa za kufanya biashara, kujenga, Kulisha familia n.k.
ili kutimiza masharti, nafikiri kwa taasisi ya fedha isiyoumiza kwa makato( siyo makanjanja) watahitaji salary slips, barua ya ajira na dhamana ya mwajiri kwa kujaza fomu ya taasisi husika.
ukivipata hivyo vitu mkopo unao ila bado una gap ya miezi kadhaa kwa sababu salary slips hazifiki haraka.
Pesa ukipata ni yako mtu asikupangie matumizi tumia ulivyodhamiria.
