GE2025 Mkoa wa Mara: Matukio na Matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2025 kama yanavyotujia

GE2025 Mkoa wa Mara: Matukio na Matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2025 kama yanavyotujia

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Wakuu,

Mada hii itakuwa na 'Updates' za Uchaguzi Mkuu 2025 kama yanavyotujia kutoka kwenu kutoka mkoa wa Mara. Ukiwa na taarifa yoyote ambayo ni ya eneo hili tafadhali usisite kuweka

Mkoa wa Mara una jumla ya Majimbo ya uchaguzi 10
  1. Jimbo la Musoma Mjini
  2. Jimbo la Musoma Vijijini
  3. Jimbo la Rorya
  4. Jimbo la Butiama
  5. Jimbo la Bunda Mjini
  6. Jimbo la Bunda
  7. Jimbo la Serengeti
  8. Jimbo la Tarime Mjini
  9. Jimbo la Tarime Vijijini
  10. Jimbo la Mwibara
Updates (Walioshinda Ubunge Mkoa wa Mara)

CCM iimeshinda majimbo yote kama ifuatavyo;

  • Mgore Miraji (Musoma Vijijini)
  • Mary Daniel (Serengeti)
  • Ester Bulaya (Bunda Mjini)
  • Jafari Chege (Rorya)
  • Profesa Sospeter Muhongo ( Musoma Vijijini)
  • Mwita Waitara (Tarime Vijijini)
  • Kangi Lugola (Mwibara)
  • Boniphace Getere (Bunda)
  • Dk Wilson Mahera (Butiama)
  • Ester Matiko (Tarime)

Kupata matukio ya nyuma kabla ya siku ya Uchaguzi soma > GE2025 - Mara: Matukio yanayojiri kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Katika kituo cha kupigia kura cha Bweri, Shule ya Msingi Manispaa ya Musoma, Mkoa wa Mara ambacho kina vituo vinne vya kupigia kura, hadi saa 1:13 asubuhi ya leo Jumatano, Oktoba 29, 2025 wasimamizi wanaendelea na maandalizi ya mwishomwisho ikiwa ni pamoja na kubandika majina, huku wananchi waliofika kituoni wakisubiri kuanza kupiga kura. Watapiga kura kumchagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wabunge na madiwani

1761716596247.png
 
Wakati zoezi la kupiga kura likiendelea leo Oktoba 29, 2025 nchi nzima Katika Jimbo la Tarime Vijijini, Nyamongo hali imekuwa ya sintofahamu ikiwa mida ya Saa 5 asubuhi vituo vya kupigia kura vikiwa wazi huku wananchi kutoonekana kusogea kupiga kura wakidai kusimama na Makamu Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) John Heche anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kuvunja sheria

Soma pia GE2025 - Tarime wananchi wanaandamana wakitaka John Heche aachiliwe huru


 
Wakati zoezi la kupiga kura likiendelea leo Oktoba 29, 2025 nchi nzima Katika Jimbo la Tarime Vijijini, Nyamongo hali imekuwa ya sintofahamu ikiwa mida ya Saa 5 asubuhi vituo vya kupigia kura vikiwa wazi huku wananchi kutoonekana kusogea kupiga kura wakidai kusimama na Makamu Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) John Heche anayeshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kuvunja sheria

Soma pia GE2025 - Tarime wananchi wanaandamana wakitaka John Heche aachiliwe huru


Safi sana
 
Back
Top Bottom