MTAZAMO
Platinum Member
- Feb 8, 2011
- 19,997
- 34,886
Wakuu,
Mkoa wetu wa Kagera umekutana na majanga mazito kuliko mkoa wowote Tanzania. Pengine kila Rais aliyetawala Taifa hili kakutana na hayo mapigo ya mkoa wa Kagera!
Mwl Nyerere alipigana vita kuukomboa mkoa wetu mikononi mwa Idd Amin! Mh Mwinyi yeye akakumbana na pigo la ugonjwa wa ukimwi kuteketeza wananchi na kuacha miji ya watu ikijaa makaburi na yatima wengi.
Mh Ben Mkapa yeye akakutana na ajali nzito ya Mv Bukoba iliyoua watu zaidi ya 800 wengi wakiwa wakazi wa huko. Mh Kikwete akakutana na ugonjwa wa mnyauko ulioteketeza migomba kama ugonjwa wa ukimwi ulivyotekeza watu! Mpaka leo bado kuna athari za ugonjwa huo wa Mnyauko.
Mh JPM yeye akakutana na tetemeko la ardhi lililoacha uharibifu mkubwa kuwahi kutokea. Sasa Mh Rais Samia tayari nae amekutana na ajali mbaya ya ndege!
Nafikiri mkoa wetu unahitaji maombi ya kipekee sana! Imekuwa ardhi inayokumbana na kila janga baya linaloibuka. Inawezekana kwenye ulimwengu wa kiroho mkoa huu una potential nzito ndio maana umejaa mashambulizi ya kila aina.
Kama Taifa upo umuhimu wa kufikiria mkoa huu kimkakati kutokana na historia hizi zinazojirudia!
Mkoa wetu wa Kagera umekutana na majanga mazito kuliko mkoa wowote Tanzania. Pengine kila Rais aliyetawala Taifa hili kakutana na hayo mapigo ya mkoa wa Kagera!
Mwl Nyerere alipigana vita kuukomboa mkoa wetu mikononi mwa Idd Amin! Mh Mwinyi yeye akakumbana na pigo la ugonjwa wa ukimwi kuteketeza wananchi na kuacha miji ya watu ikijaa makaburi na yatima wengi.
Mh Ben Mkapa yeye akakutana na ajali nzito ya Mv Bukoba iliyoua watu zaidi ya 800 wengi wakiwa wakazi wa huko. Mh Kikwete akakutana na ugonjwa wa mnyauko ulioteketeza migomba kama ugonjwa wa ukimwi ulivyotekeza watu! Mpaka leo bado kuna athari za ugonjwa huo wa Mnyauko.
Mh JPM yeye akakutana na tetemeko la ardhi lililoacha uharibifu mkubwa kuwahi kutokea. Sasa Mh Rais Samia tayari nae amekutana na ajali mbaya ya ndege!
Nafikiri mkoa wetu unahitaji maombi ya kipekee sana! Imekuwa ardhi inayokumbana na kila janga baya linaloibuka. Inawezekana kwenye ulimwengu wa kiroho mkoa huu una potential nzito ndio maana umejaa mashambulizi ya kila aina.
Kama Taifa upo umuhimu wa kufikiria mkoa huu kimkakati kutokana na historia hizi zinazojirudia!
