PreGE2025 Mkitaka reforms mkapige kura

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Changamoto kubwa ya nyinyi wenzetu ni kuwaza kuwa mnayo hati miliki ya usahihi wa mawazo. Mtu asipoamini katika mnayoyaamini nyinyi mnamwona amepotoka, hafikiri vizuri, ni mjinga au ananufaika moja kwa moja na serikali. Nijibu objectively, moja, ukiwa na kadi ya CCM unakuwa umetenda kosa gani? Mbili kwakupiga kura, unakuwa umevunja sheria gani ya nchi? Tatu, kipi kinakufanya udhani mawazo yako ya no reform no election ndio mawazo bora kuliko no election no reform?
 
Ahadi ya katiba mpya ndio imekukera hivi? Kwani kwenye No reforms No election unadai nini?
Kwani kwenye uchaguzi wa mwaka 2019,2020 na 2024 kwenye serikali za mitaani nn kinaendelea hadi NO ELECTION NO REFORMS isiwe kitu cha maana kwa watanzania.
 
Tutabaki na kura zetu na kuzilinda kwa wivu mkubwa,
Kwa nini nipoteze muda wangu kupanga foleni ya kupiga kura wakati najua kabisa kuna majizi yanaivizia kura yangu waiibe
 
Nendeni mkachaguane muibiane wenyewe kwa wenyewe
Hatuna muda wa kupoteza
 
No reforms no election. Huu ujinga kajadili na mkeo usituletee huku
 
That's very good..

Umekuja precisely kutaka hoja, basi tutakupa hoja japo, from my persective najua kabisa kuwa unaelewa tatizo la chaguzi zetu liko wapi lakini unajifanya hamnazo tu...

It doesn't matter, kwamba, pamoja na kujifanya "mjinga", we will teach you as much as you want, mpaka ukiri kwa kinywa chako kuwa - NIMEELEWA...
Changamoto kubwa ya nyinyi wenzetu ni kuwaza kuwa mnayo hati miliki ya usahihi wa mawazo.
1. Sio kweli. Hiyo ni dhana yako tu na kutojiamini kwako kwa sbb unajua kuwa wewe na CCM yenu huko hamna hoja kabisa za kutetea uhalali wa ushindi wenu ktk chaguzi zote chini ya mfumo wa vyama vingi tangu mwaka 1995 ktk maswala haya...

2. Wazo sahihi ni sahihi tu, na wazo la kijinga ni la kijinga tu. Na usahihi au ubovu wa mawazo unapimwa kwa hoja kuhusu kinachojadiliwa. Mawazo yako yakiwa hovyo, hayajibu hoja basi automatic, yanakuwa ni upogo na ujinga tu kwa yeyote anayepima!
Mtu asipoamini katika mnayoyaamini nyinyi mnamwona amepotoka, hafikiri vizuri, ni mjinga au ananufaika moja kwa moja na serikali.
Wewe huamini nini na sisi tunaamini nini kwa ulinganifu?

Hoja zako ni zipi ambazo unazipima kutoka kwenye hoja zetu ili tukuamini?
Nijibu objectively, moja, ukiwa na kadi ya CCM unakuwa umetenda kosa gani?
Hakuna kosa...
Ni haki yako kuwa mwanachama wa chama chochote...
Na wewe nikuulize, kuna ubaya gani kuwa mwanachama wa kadi ya CHADEMA? Kuna kosa hapo kisheria? Why are harrasing, torturing and putting them in custodies just because of their dissent opinions against the govt..? Why..? Una hoja kwenye hili..?
Mbili kwakupiga kura, unakuwa umevunja sheria gani ya nchi?
Hakuna..
Na kutokwenda kupiga kura kwa kuwa unajua kuwa kura yako haitahesabiwa na kuhesabika kwa kiongozi uliyemchagua badala atatangazwa ambaye hukumchagua ni kuvunja sheria gani?
Tatu, kipi kinakufanya udhani mawazo yako ya no reform no election ndio mawazo bora
Kwa sababu;
1. Uchaguzi HURU, wa HAKI, wa WAZI na KUAMINIKA Tanzania kwa sasa haiwezekani. Ushahidi ni chaguzi za 2019, 2020 na 2024


2. Electoral system ya Tanzania ni presidential (inadhibitiwa na Rais aliyeko madarakani) ambaye huwa ni wa chama kishiriki pia ktk uchaguzi na huyo Rais akiwa mgombea kupitia chama chake. Mfano, Rais ndiye anateua wasimamizi wa uchaguzi wote kuanzia kwenye vituo vya kupigia kura hadi Mwenyekiti wa Tume yenyewe na Mkurugenzi wa uchaguzi. Sasa ktk scenario hii, kwanini asijipendelee yeye na wagombea wengine wa chama chake? Kwanini asiwafanyie mtima nyongo washindani wake wa vyama vingine? What happened 2019? 2020? 2024?
√ Do you know that 96% ya opposition candidates in 2019 local gvt election walikuwa disqualified using baseless grounds?
√ Na unajua kuwa ktk uchaguzi mkuu wa 2020 wa Urais mpaka leo matokeo ya kura ya urais jimbo kwa jimbo hajatangazwa?
√ Si unajua kuwa, Magufuli/Samia walitangazwa tu randomly kuwa wameshinda lakini huwezi ku - verify ushindi wao popote..?

3. Tunahitaji referee aitwaye "Tume Huru ya uchaguzi" hapa Tanzania. Rais awe mbali kabisa na huyu refa...

4. Tunahitaji matokeo ya kura ya u - Rais kama yana utata na wagombea wengine hawajaridhika, basi waende mahakamanj wahoji. Hii itaepusha mtu kutangazwa tu bila verification yoyote ya uhalali wa kura za ushindi wake..!

5. Tunahitaji usawa wa mgawanyo wa majimbo ya uchaguzi kwa uwakilishi wa wabunge kwa kigezo cha idadi ya watu (ambao ndio wanaokilishwa). Mfano, inawekana vipi jimbo lenye wapiga kura 5,000 liwe na mbuge mmoja sawa na jimbo la wapiga kura 450,000+? Hii wewe inakupa maana gani ukiona mgawanyo wa majimbo kwa namna hii?
kuliko no election no reform?
√ Mimi ninataka tufanye mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi kwanza ndo twende kwenye uchaguzi ambayo ndiyo maana ya NO REFORMS NO ELECTION..

√ Hili la NO ELECTION NO REFORMS ni la kwako, wewe ndiyo toa sababu zako..
 
1. Sasa ndugu Dr Adam Francis, hivi kweli unaweza kumtofautisha mtu kwa kile asemacho (ajenda/hoja) na personality yake?

2. Kama siasa ni maisha ya watu, kwanini huko CCM mnatumia ulaghai wa kisiasa kulaghai/kuwadanganya watu wanyonge wapiga kura?

3. Kwanini CCM mnafanya manipulative politics, kuiba kura, kuiba uchaguzi, kuteka na kuua watu unaosema "siasa ni maisha ya watu lakini mnawaua" ili kubaki madarakani? Hizi ni siasa au ujangili wa kimadaraka?

4. Kwa ufahamu wangu mimi, siasa ni consensus au mapatano ya hiari (mutual agreement) kati ya viongozi na wanaoongozwa. Ikifika wakati viongozi wanajifosi kwa nguvu kwa watawaliwa kuwa viongozi na kuita hiyo ni siasa, basi utakuwa very wrong kwa kuwa hizo sio siasa bali ujangili kwa jina la siasa..!!
 
Mleta mada nina swali moja tu.

Je Tundu Lissu angekua ndio anateua mkurugenzi wa tume, mwenyekiti wa tume , wajumbe na makamishna wa tume na kikawepo kifungu ambacho kinaipa nguvu tume kwa maamuzi ya na matokeo kutopingwa mahakamani yoyote.

Je CCM mngeshiriki uchaguzi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…