Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
- Thread starter
- #141
Lowasa nimjuaye mimi ni yule aliyekuwa hana pesa alipokuwa chuoni UDSM na hata alipokwenda UK kusoma.
Alipopewa uDirector AICC alikuwa hana hata suti na usafiri wa maana. AICC akaifanya kijiwe chake cha kujipalilia kwa jumuiya za CCM hasa vijana. Mapato ya AICC yakashuka kupita kiasi. Mikutano AICC ikawa ni jumuiya za CCM kuliko ya kimataifa.
Then alipoingia Wizara ya Ardhi, akaendelea kujipanga. Akamchukua mshikaji wake yule mnyarwanda, Haruni Masebu akamuweka NHC, si unajua tena NHC kulivyo. Baadaye akamuweka EWURA, kule kwenye mambo yote ya mafuta.
Halafu akapitisha mkwara hapo wizarani na kufukuza watu kazi akiwasingizia ubadhilifu, kisha yeye akaketi chini kuanza kuinywa wizara taratibu na kujitajirisha. Ghafla yule masikini akawa ananukia utajiri. Akawa hata na uwezo wa kujenga majumba ya mamilioni overnight, likiwemo lile la Masaki lililopangishwa na ubalozi wa SA, licha ya kipato chake tu cha utumishi serikalini. Labda mwenzetu alishinda bahati nasibu ya Power Ball.
Mara akaanza kujishaua, akaweza kukodisha ndege ya kumpeleka Dodoma kugombea uraisi, kabla ya kupigwa buti na mwalimu. Juzi juzi tena akakodi nyingine ya kumpeleka kwenye mazishi ya Mwalimu na Monduli alipofukuzwa uPM. Hivi ni watumishi wangapi wa serikalini tena waliofukuzwa kazi lakini bado wanakuwa na uwezo wa kukodisha ndege ya kuwarudisha majimboni kwao? Kumbuka huyu ndiye yule yule Lowasa aliyekuwa masikini miaka michache iliyopita na ajira yake, ukiachilia ile ya AICC, ni hizi za serikali ambazo mishahara na marupurupu yake tunayajua.
Ingekuwa vema watu wote wanaogombea uraisi wafanyiwe auditing ya mapato/matumizi yao na kodi walizolipa. Hapo madudu mengi yangegundulika.
Umeweka simulizi ya mapito ya rais mtarajiwa,
Hiyo ni hadithi ya kufikirika tu!
Ili ueleweke leta ushahidi halisi wa ufisadi wa Lowasa hapa!
Skani nyaraka zinazo onyesha kuwa Edward Lowassa ni Fisadi na zilete hapa