Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 887
- 2,201
Wajumbe, mara kadhaa mmekuwa mkiambiwa kuwa wachekeshaji wa redio ya Wasafi Maulid Kitenge, Zembwela na Paul James au PJ ni wajinga, wavivu wa kufikiri na pengine wanaoshambiliwa na ugonjwa mbaya wa ujinga msiwe mnabisha.
Leo asubuhi wameendeleza komedi yao huko Morogoro wakiendelea na kile wanachokiita "Wekeza Tanzania ya Samia". Hapa walikuwa "serious" kumshauri RC wa Mkoo huo Adam Malima wakisema;
"Mhe, unajua sisi tunazunguka sana ndani na nje ya nchi wananchi wengi sana wanatuambia na hata kabla ya kuja hapa wametuomba tukuambie hivi,
"Kwa kuwa Moro Kuna fursa nyingi za uchumi kama Utalii, Kilimo nakadhali wanaomba ujenge hapa kiwanja kikubwa Cha ndege kama Julius Nyerere International Airport ili watu wawe wanakuja na midege mikubwa ya mizigo kuchukua bidhaa hapa hapa na kuruka nayo kwenda Ulaya". Wote wakaitikia hata na PJ ambaye walau amesoma kidogo kati Yao.
Yani hawa wachekeshaji hawaioni uwanja wa ndege unaojengwa Msalato Dodoma. Hawaioni JNIA. Hawaioni SGR. Eti Hawa ndio watetezi wa DP World! Hebu Serikali tuweni basi serious hata mara moja moja kwa mwaka.
Leo asubuhi wameendeleza komedi yao huko Morogoro wakiendelea na kile wanachokiita "Wekeza Tanzania ya Samia". Hapa walikuwa "serious" kumshauri RC wa Mkoo huo Adam Malima wakisema;
"Mhe, unajua sisi tunazunguka sana ndani na nje ya nchi wananchi wengi sana wanatuambia na hata kabla ya kuja hapa wametuomba tukuambie hivi,
"Kwa kuwa Moro Kuna fursa nyingi za uchumi kama Utalii, Kilimo nakadhali wanaomba ujenge hapa kiwanja kikubwa Cha ndege kama Julius Nyerere International Airport ili watu wawe wanakuja na midege mikubwa ya mizigo kuchukua bidhaa hapa hapa na kuruka nayo kwenda Ulaya". Wote wakaitikia hata na PJ ambaye walau amesoma kidogo kati Yao.
Yani hawa wachekeshaji hawaioni uwanja wa ndege unaojengwa Msalato Dodoma. Hawaioni JNIA. Hawaioni SGR. Eti Hawa ndio watetezi wa DP World! Hebu Serikali tuweni basi serious hata mara moja moja kwa mwaka.