Mke wangu na "Mheshimiwa Mbowe!"

Jamani hii title ya thread hii kiboko!!!!! utafikiri magazeti ya udaku mana ndio title inakupa hekaheka ndani hakuna kitu
 
Mwishoni atasikia kuwa Mbowe kagombea Uraisi na kushinda na yeye ataamu Awe baba ndani ya nyumba na wewe uwe MAMA wa nyumba chukua Tahadhari....Anzisheni Mapenzi ya mseto

Tafuteni muungano kama wa Cuf n CCm
 
Duh, hii kali sana, ijumaa yangu itakuwa safi kweli kumbe hawa akina mama wako kama Mbowe eeeh, ndio maana jana nimenuniwa home kisa eti housegirl wetu ambaye aliondoka tu mwenyewe kaja jana usiku, hana sababu ya msingi iliyomleta, mara nikashtukia nimeitwa chumbani, kufika naulizwa kafwata nini huyu?? nilishtuka ila nikajibu kwa ujasiri na hekima tu kuwa, ni vyema tukamuulize yeye na sio mimi!!!

sasa mkuu na hali hii jumlisha umetoka kibaruani mkoloni kakuzingua ile mbaya,umepita kitaa washkaji wanakwambia ile dili mliyotegemea i-materialize siku hiyo imebuma na hiyo wiki ndio ya kukamilisha ada ya kina 'junior' na hujapeleka 'kabajaji' kako garage coz mileage ishapitiliza kwahiyo hata kale ka-vekesheni ulikopanga kum-suprise nako wife ndo kanaota mbawa hivo na salio halisomi,afu unarudi nyumbani unaulizwa(ki-shaari shari!) beki tatu alieondoka bila taarifa siku kadhaa nyuma amefuata nini?!unaweza ukafyatuka kibao cha ghafla bila utashi hivihivi hakyanani!!
 
huyo ongozana nae bar na misele yako mingine baada ya kipindi fulani atachoka. atarudi nyumbani mapema mwenyewe.
 
huyo ongozana nae bar na misele yako mingine baada ya kipindi fulani atachoka. atarudi nyumbani mapema mwenyewe.
Du grey nikizunguka naye si itakuwa natangaza vivutio vya utalii, wakitaka kuja nitafanyaje?
 
Mwishoni atasikia kuwa Mbowe kagombea Uraisi na kushinda na yeye ataamu Awe baba ndani ya nyumba na wewe uwe MAMA wa nyumba chukua Tahadhari....Anzisheni Mapenzi ya mseto Tafuteni muungano kama wa Cuf n CCm
Mkuu kufikia huko kwenye mseto inabidi upitie maandamano na pengine damu kadhaa kupotea ka Arusha, halafu mimi negotiation skills zangu zinaishia kwenye amani tu ikivurugika naishiwa maujanja.
 
babu mi ndo nafanya shortlisting ya baba kivuli hapa, kivuli chako kina urefu na upana wa kutosha kukinga jua na mwezi 24/7?
Jamani mbona hivyo option ya baba kivuli haitumiki hapa, labda na mimi nianze kutekeleza sera ya majimbo.
 
yaani huyo sista wangu nimempenda sana. Asante kutuletea hili,maana hata mie nilishaanzisha hili kwa shem wako.In one car sasa hivi, mambo ya kila mtu na gari wakati wote mwaelekea mjini hakuna. After all ni kwa faida yetu sote na familia nzima.
Maggy, hii ya kushare gari inapendeza kama bado ni ile ngazi ya boyfriend na girlfriend mkiingia kwenye mseto mnaitakiwa mpeane nafasi kidogo ya kuji miss
 
Inakubidi udai uhuru tena. Hata katiba yetu hii ina insist uhuru wa mtu kuishi atakavyo bila kuingiliwa na yeyote ila ukivunja sheria. Au taarifa za intelijensia zimemfikia?
 
Ecoli asante for making my day!! Nimecheka saaana!! Ila on a serious NOTE ni kuwa UNALO!!! Yani kama issue ya kupunguza matumizi unaina ni kunyimwa uhuru; basi ulipoteza uhuru wako siku ulipofunga ndoa!!! Maana marriage is all about sharing...Kam huwezi ndoa si yako Kaka...
 
Naomba mwongozo wa Spika! Kikanuni tunapokaa bar, pale New Africa, kuwe na posho ya kikao maana tunajadili masuala mengi ya muhimu kwa familia.
 
Sikiliza..... huwezi kumtenga mtu ambay e ni mke wako...yaani izo strategies zako hazina mshiko...Hapo Mama ana kila mantiki kwenye what she wants in the family... tulia wnawake wa nje wanakutia n dimu tu.........
 
Sijakosea jukwaa maana kuna walioanza kununa, mwezenu nyumbani kumeanza kuwa kuchungu baada ya wifi yenu kuanza visa baada ya vikao vya bunge kuanza. Wiki ya kwanza alianza kama utani eti anataka kupendekeza baba kivuli ili awe ananikosoa na kutoa mtazamo mbadala kwa masuala yetu pale nyumbani. Hili nililipinga kwa nguvu zote kwa kuwa sikuwa na uhakika na hadidu za rejea za baba kivuli, wiki iliyofuata akaanza kupinga posho zangu na misafara mikubwa ya marafiki ninapokwenda bar.

Nikidhani itaishia hapo sasa baada kiongozi wa upinzani bungeni kurudisha shangingi lake, yeye sasa ndio amekuja na kali eti anataka kupiga bei ka vitz kake ili tuwe tunapanda gari moja kwenda na kurudi kazini sasa mimi hapo naona kama uhuru wangu unaelekea kunitupa mkono, Nifanyeje wandugu kwa hatua za mwanzo nimepiga marufuku bunge nyumbani kwangu.

Andamana mkuu...
 
mkuu hapo bwana lazima mambo ya muumgano yabainishwe na mambo ya zanzibar pekeyake yawe wazi ila jamhuri iendellee kubaki na kutambulika vilevile ha ha ha haaaaa
 
Ndio maana mimi nilishtuka mapemaaa. Hamna kutumia gari tofauti kwenda kazini. Haya mambo ya wadada kukusubili kwenye kona uwape lifti marufuku. Tutabana mpaka penati mwaka huu.


Hahahahahahah lol! NK! umenichekesha sana hahahahahah unakaba mpaka penalty lol! hupepesi macho hata sekunde! Kila la heri :) Timu lazima itatoa wachezaji uwanjani ikiwa unakaba mpaka penalty :)

 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom