Duh, hii kali sana, ijumaa yangu itakuwa safi kweli kumbe hawa akina mama wako kama Mbowe eeeh, ndio maana jana nimenuniwa home kisa eti housegirl wetu ambaye aliondoka tu mwenyewe kaja jana usiku, hana sababu ya msingi iliyomleta, mara nikashtukia nimeitwa chumbani, kufika naulizwa kafwata nini huyu?? nilishtuka ila nikajibu kwa ujasiri na hekima tu kuwa, ni vyema tukamuulize yeye na sio mimi!!!
Mkuu kufikia huko kwenye mseto inabidi upitie maandamano na pengine damu kadhaa kupotea ka Arusha, halafu mimi negotiation skills zangu zinaishia kwenye amani tu ikivurugika naishiwa maujanja.Mwishoni atasikia kuwa Mbowe kagombea Uraisi na kushinda na yeye ataamu Awe baba ndani ya nyumba na wewe uwe MAMA wa nyumba chukua Tahadhari....Anzisheni Mapenzi ya mseto Tafuteni muungano kama wa Cuf n CCm
Maggy, hii ya kushare gari inapendeza kama bado ni ile ngazi ya boyfriend na girlfriend mkiingia kwenye mseto mnaitakiwa mpeane nafasi kidogo ya kuji missyaani huyo sista wangu nimempenda sana. Asante kutuletea hili,maana hata mie nilishaanzisha hili kwa shem wako.In one car sasa hivi, mambo ya kila mtu na gari wakati wote mwaelekea mjini hakuna. After all ni kwa faida yetu sote na familia nzima.
Sijakosea jukwaa maana kuna walioanza kununa, mwezenu nyumbani kumeanza kuwa kuchungu baada ya wifi yenu kuanza visa baada ya vikao vya bunge kuanza. Wiki ya kwanza alianza kama utani eti anataka kupendekeza baba kivuli ili awe ananikosoa na kutoa mtazamo mbadala kwa masuala yetu pale nyumbani. Hili nililipinga kwa nguvu zote kwa kuwa sikuwa na uhakika na hadidu za rejea za baba kivuli, wiki iliyofuata akaanza kupinga posho zangu na misafara mikubwa ya marafiki ninapokwenda bar.
Nikidhani itaishia hapo sasa baada kiongozi wa upinzani bungeni kurudisha shangingi lake, yeye sasa ndio amekuja na kali eti anataka kupiga bei ka vitz kake ili tuwe tunapanda gari moja kwenda na kurudi kazini sasa mimi hapo naona kama uhuru wangu unaelekea kunitupa mkono, Nifanyeje wandugu kwa hatua za mwanzo nimepiga marufuku bunge nyumbani kwangu.
Ndio maana mimi nilishtuka mapemaaa. Hamna kutumia gari tofauti kwenda kazini. Haya mambo ya wadada kukusubili kwenye kona uwape lifti marufuku. Tutabana mpaka penati mwaka huu.