profesawaaganojipya
JF-Expert Member
- Apr 21, 2015
- 1,485
- 3,134
Wakuu,
Nilikatiwa kipande cha ardhi na kanisa, kwa makubaliano kwamba nijenge fremu halafu tutakatana kwenye kodi na makato yakiisha fremu itakuwa mali ya kanisa.
Unapewa miezi 3 ya kujenga, hata kama hujamaliza fremu inaanza kusoma. Nilimaliza ujenzi ndani ya miezi tisa, nikaweka vifaa vya umeme wa majumbani.
Kwa kuwa mimi ni muajiriwa wa serikali, nikaona bora mke wangu akae maana alikuwa hana shughuli analala tu nyumbani.
Ni miaka miwili imepita bado mwaka mkataba uishe, hela anazouza mimi sizioni wala sijui ziko wapi, vifaa anaenda kujumua yeye, mambo yote ni yeye.
Sasa kuna wakati nakuwa sina hata hela ya kula, ilibidi leo nimuulize, inakuwaje fremu ni ya kwangu nimejenga mimi na mtaji ni wangu kwa nini hela anazificha na mimi sina hela.
Amenijibu kuwa nikiona hivyo, KUNA MAHALI NAFELI akanyamaza.
Sasa wakuu hivi nafeli wapi?
Nilikatiwa kipande cha ardhi na kanisa, kwa makubaliano kwamba nijenge fremu halafu tutakatana kwenye kodi na makato yakiisha fremu itakuwa mali ya kanisa.
Unapewa miezi 3 ya kujenga, hata kama hujamaliza fremu inaanza kusoma. Nilimaliza ujenzi ndani ya miezi tisa, nikaweka vifaa vya umeme wa majumbani.
Kwa kuwa mimi ni muajiriwa wa serikali, nikaona bora mke wangu akae maana alikuwa hana shughuli analala tu nyumbani.
Ni miaka miwili imepita bado mwaka mkataba uishe, hela anazouza mimi sizioni wala sijui ziko wapi, vifaa anaenda kujumua yeye, mambo yote ni yeye.
Sasa kuna wakati nakuwa sina hata hela ya kula, ilibidi leo nimuulize, inakuwaje fremu ni ya kwangu nimejenga mimi na mtaji ni wangu kwa nini hela anazificha na mimi sina hela.
Amenijibu kuwa nikiona hivyo, KUNA MAHALI NAFELI akanyamaza.
Sasa wakuu hivi nafeli wapi?