Kimada alivyonifanya nimsahau mke wangu yaliyonikuta Najuta

Protector

JF-Expert Member
May 20, 2019
414
877
Hii ni story ya kweli nilisimuliwa na jamaa yangu nami naileta kwenu kama funzo.

Ilikuwa mwaka 2004 ujenzi wa barabara ya Shinyanga-Mwanza umepamba moto chini ya Grinaker LTA nami nikiwa mmojawapo kati ya wafanyakazi wa kampuni hiyo. Kazi yangu ilikuwa ni kugawa mafuta kwenye magari na mashine. Kazi niliyoipenda sana kwani ilikuwa inaniingizia pesa ya kutosha. Kwa wastani kwa siku nilikuwa na uwezo wa kuingiza 200k (kuna siku inakuwa zaidi na siku inakuwa chini). Hela hiyo nikipata kwa siku 2 inazidi mshahara wangu wa mwezi mmoja.

Hela ya mafuta ilinizuzua nikapata kimada mwalimu pale kando ya mgodi wa Mwadui panaitwa Maganzo, nikamsahau mke wangu aliyekuwa na watoto wawili nikaacha hata kwenda nyumbani nikahamia kwa kimada. Marafiki walinishauri lakini sikusikia la mtu, kwa kweli nilimpenda sana huyu mwalimu.

Mke wangu alikuwa anaishi mgodini Mwadui ambako nami nilikuwa nikiishi na kufanya vibarua humo kabla sijapata kazi ya barabara. Sheria ya nyumba za mgodini kama hufanyi kazi za kuinufaisha kampuni basi hutakiwi kuishi kwenye nyumba hizo.

Mke wangu hakuwa na kazi alikuwa akikaa kwa jina langu nami nimepotea sionekani basi uongozi ukamwambia aachie nyumba ili wakae wafanyakazi wengine. Nilipata taarifa hizo lakini sikujali mapenzi ndiyo yaliongezeka kwa huyu mwalimu.

Ni kweli aliondoka na sikutaka kujua ameenda wapi na ataishi vipi sikujali, mwalimu alijua kunilea mpaka nikasahau kila kitu kuhusu familia yangu na mke wangu tuliyefunga nae ndoa. Ilikuwa nikirudi jioni namuwekea hela zote mezani kesho yake naondoka na pesa kidogo tu kula kabla sijapata mlungula wa siku.

Sikutaka kujua pesa zinatumije niliamini huyo ndie mke wangu mpya tutakayeishi nae siku zote za maisha yetu. Kumbe mwalimu alinunua kiwanja na kujenga nyumba mimi nikiwa sijui. Haikuwa nyumba kali sana lakini ni nyumba ambayo ni standard mtu kuishi wa kipato cha kawaida.

Siku moja naambiwa nimejenga nyumba mme wangu wiki ijayo tutahamia, kwa kweli nilifurahi japo sikujua amejenga vipi. Siku ikafika tukahamia kwenye nyumba yetu maisha yakaanza. Muda ukaenda, miaka ikaenda kazi ya barabara ikaisha, nikapokea mafao yangu yote na NSSF nikamkabidhi mwalimu nikiamini ni mke wangu hela zangu ni zake pia.

Ilipita miezi miwili siendi kazini nashinda tu nyumbani kazi imeisha wa wakandarasi wameondoka, mwalimu akaniambia nitafute kazi nyingine sio vizuri kushinda nyumbani. Nikaanza kutafuta lakini sikupata sikuwa na cheti chochote cha taaluma hata hiyo ya mafuta sijui walitumia kigezo gani kunipa kwa sababu niliishia darasa la saba.

Ilifikia kipindi pesa ikakata, nilikuwa sijazoea kuombwa pesa na mwalimu ndiye alikuwa mmiliki wa pesa zangu hivyo alikuwa anajiamulia mwenyewe nini cha kufanya. Nikaanza kuombwa pesa mara unga na mchele umeisha, mara naomba pesa nikalipe mchezo, yaani vitu vingi sana. Nilimweleza hali halisi kuwa sina pesa kwa sasa asubiri nipate kazi nyingine.

Ilipita miezi 7 tangu kazi iishe na nyumbani nikaona kabisa mambo yamebadilika tukaanza kula dagaa mara nyingi kitu ambacho sikukizoea. Tuliendelea hivyo hivyo kigumu akiwa na tegemeo kuna siku nitapata kazi lakini mambo hayakuwa hivyo kwani sikupata kazi yoyote.

Baada ya miezi takribani 9 akaniambia nimtafute mke wangu kwani kuna watoto wananitegemea, nilimwambia aachane na stori za mke wangu mimi nipo nae na ninampenda yeye. Akaniuliza yeye ni nani kwangu mpaka nimpende? Nikamwambia ni mke wangu,. Lahaulaaa ni kama nimemtukana akaniambia nimkome akaniuliza tumefunga ndoa wapi nikabaki nashangaa. Akaniambia ana mchumba wake natakiwa kuondoka pale na wanategemea kufunga ndoa.
Kwa kweli niliumia sana.

Nilichoamua kufanya ............
Itaendelea
 
Aisee uje haraka watu tuna alosto hapa,usitikarishe kama watoto wadogo ..alaa
 
Hakuna chochote kinacho tuzuzuaga zaidi ya ujinga na ulimbukeni na hua tunakuja kukumbuka familia pale mrija wa ile pesa unavyo kuja kukata, tupo kama mi mbuzi sometimes, tena ni kipindi ambacho hua hatuhitaji kabisa ushauri
JamiiForums1371650826.jpg
 
Tabia ya mwanaume yajulikana akipata pesa, uvumilivu wa mwanamke unajulikana mme wake akikosa pesa
 
Hii ni story ya kweli nilisimuliwa na jamaa yangu nami naileta kwenu kama funzo.

Ilikuwa mwaka 2004 ujenzi wa barabara ya Shinyanga-Mwanza umepamba moto chini ya Grinaker LTA nami nikiwa mmojawapo kati ya wafanyakazi wa kampuni hiyo. Kazi yangu ilikuwa ni kugawa mafuta kwenye magari na mashine. Kazi niliyoipenda sana kwani ilikuwa inaniingizia pesa ya kutosha. Kwa wastani kwa siku nilikuwa na uwezo wa kuingiza 200k (kuna siku inakuwa zaidi na siku inakuwa chini). Hela hiyo nikipata kwa siku 2 inazidi mshahara wangu wa mwezi mmoja.

Hela ya mafuta ilinizuzua nikapata kimada mwalimu pale kando ya mgodi wa Mwadui panaitwa Maganzo, nikamsahau mke wangu aliyekuwa na watoto wawili nikaacha hata kwenda nyumbani nikahamia kwa kimada. Marafiki walinishauri lakini sikusikia la mtu, kwa kweli nilimpenda sana huyu mwalimu.

Mke wangu alikuwa anaishi mgodini Mwadui ambako nami nilikuwa nikiishi na kufanya vibarua humo kabla sijapata kazi ya barabara. Sheria ya nyumba za mgodini kama hufanyi kazi za kuinufaisha kampuni basi hutakiwi kuishi kwenye nyumba hizo.

Mke wangu hakuwa na kazi alikuwa akikaa kwa jina langu nami nimepotea sionekani basi uongozi ukamwambia aachie nyumba ili wakae wafanyakazi wengine. Nilipata taarifa hizo lakini sikujali mapenzi ndiyo yaliongezeka kwa huyu mwalimu.

Ni kweli aliondoka na sikutaka kujua ameenda wapi na ataishi vipi sikujali, mwalimu alijua kunilea mpaka nikasahau kila kitu kuhusu familia yangu na mke wangu tuliyefunga nae ndoa. Ilikuwa nikirudi jioni namuwekea hela zote mezani kesho yake naondoka na pesa kidogo tu kula kabla sijapata mlungula wa siku.

Sikutaka kujua pesa zinatumije niliamini huyo ndie mke wangu mpya tutakayeishi nae siku zote za maisha yetu. Kumbe mwalimu alinunua kiwanja na kujenga nyumba mimi nikiwa sijui. Haikuwa nyumba kali sana lakini ni nyumba ambayo ni standard mtu kuishi wa kipato cha kawaida.

Siku moja naambiwa nimejenga nyumba mme wangu wiki ijayo tutahamia, kwa kweli nilifurahi japo sikujua amejenga vipi. Siku ikafika tukahamia kwenye nyumba yetu maisha yakaanza. Muda ukaenda, miaka ikaenda kazi ya barabara ikaisha, nikapokea mafao yangu yote na NSSF nikamkabidhi mwalimu nikiamini ni mke wangu hela zangu ni zake pia.

Ilipita miezi miwili siendi kazini nashinda tu nyumbani kazi imeisha wa wakandarasi wameondoka, mwalimu akaniambia nitafute kazi nyingine sio vizuri kushinda nyumbani. Nikaanza kutafuta lakini sikupata sikuwa na cheti chochote cha taaluma hata hiyo ya mafuta sijui walitumia kigezo gani kunipa kwa sababu niliishia darasa la saba.

Ilifikia kipindi pesa ikakata, nilikuwa sijazoea kuombwa pesa na mwalimu ndiye alikuwa mmiliki wa pesa zangu hivyo alikuwa anajiamulia mwenyewe nini cha kufanya. Nikaanza kuombwa pesa mara unga na mchele umeisha, mara naomba pesa nikalipe mchezo, yaani vitu vingi sana. Nilimweleza hali halisi kuwa sina pesa kwa sasa asubiri nipate kazi nyingine.

Ilipita miezi 7 tangu kazi iishe na nyumbani nikaona kabisa mambo yamebadilika tukaanza kula dagaa mara nyingi kitu ambacho sikukizoea. Tuliendelea hivyo hivyo kigumu akiwa na tegemeo kuna siku nitapata kazi lakini mambo hayakuwa hivyo kwani sikupata kazi yoyote.

Baada ya miezi takribani 9 akaniambia nimtafute mke wangu kwani kuna watoto wananitegemea, nilimwambia aachane na stori za mke wangu mimi nipo nae na ninampenda yeye. Akaniuliza yeye ni nani kwangu mpaka nimpende? Nikamwambia ni mke wangu,. Lahaulaaa ni kama nimemtukana akaniambia nimkome akaniuliza tumefunga ndoa wapi nikabaki nashangaa. Akaniambia ana mchumba wake natakiwa kuondoka pale na wanategemea kufunga ndoa.
Kwa kweli niliumia sana.

Nilichoamua kufanya ............
Itaendelea
Mwenye kisu kikali ndiye hula nyama.. Kama kisu hakuna, ulaji hakuna!
 
........ Inaendelea
Baada ya kuambiwa niondoke nilienda kwa mwenyekiti wa mtaa kushtaki kuwa nafukuzwa na mke wangu na nikamweleza kila kitu kama nilivyoeleza sehemu iliyopita. Mwalimu akaitwa akaulizwa kwa nini anafanya vile akasema kwa sababu ni kwake na mimi nilikaribishwa tu pale kama mchepuko. Mwenyekiti nilimweleza mpaka nilivyokuwa namwachia pesa zote ninazozipata kazini, niliulizwa kama nina ushahidi wowote nikawa sina, yule mwanamke akashinda nikaondoka.
Baada ya kuondoka pale nikawa sina pa kwenda ndugu zangu wamenitenga na marafiki pia nikawa mtu wa kuhangaika. Ndipo nikapata wazo la kumtafuta mke wangu sikujua ameenda wapi. Baadae nikaambiwa alienda Bariadi nyumbani kwa wazazi wake, kwa kuwa nilikuwa napajua nikaenda mpaka ukweni sina mbele wala nyuma. Baba mkwe aliponiona hakutaka hata salamu yangu, nilipomsalimia kabla hajajibu aliniuliza nimefata nini? Nikamwambia nimemfata mke wangu. Nikajibiwa hapa mke hayupo ameolewa na sijui ameolewa wapi, alishindwa kukaa nasi sababu ya ugumu wa maisha na kutunza watoto ilikuwa kazi ngumu kwake na sisi ni wazee hatuwezi kumsaidia kwa chochote hivyo aliamua kuolewa kupunguza ugumu wa maisha. Na watoto wako anao wanalelewa na baba wa kambo. Nilisikitika sana hasa nikikumbuka wanangu sijawatunza inavyotakiwa na uwezo huo nilikuwa nao. Leo nimeenda nikiwa mikono mitupu watanielewa kweli? Niajipiga konde moyo nikasema liwalo na liwe naenda kumtafuta mke wangu huko alikoolewa angalau niwachukue wanangu hata kama yeye nikimwacha itakuwa sawa.
Nikaanza kumtafuta bahati nzuri nilimpata nikaonana nae. Kwanza nilianza kwenda kwa siri mumewe akiwa hayupo ndiyo naenda baadae ilibidi mumewe ajue kuwa mimi ndio baba wa watoto, na alipojua hakuwa na shida yoyote aliniambia hawa wanao mimi sina shida unaweza kuwachukua au kuwaacha wakae na mama yao. Nikajisemea moyoni nikiwachukua nitawapeleka wapi sina pa kuishi naishi kama mkimbizi popote kambi, wakati mwingine naenda stendi najifanya nasafiri nalala pale asubuhi naondoka kuzurula. Niliamua kuwaacha wakae na mama yao nikawaambia naenda nyumbani nikirudi nitawachukua. Walifurahi kumuona baba yao ambao ni kama miaka mitatu nilikuwa sijawaona.
Niliondoka lakini nikiwa sina furaha moyoni, nilirudi nyumbani nikaanza maisha ya kubangaiza. Nikawa fundi baiskeli kuziba pancha na matengenezo mengine ya baiskeli. Nikasahau kuhusu watoto nikaanza maisha upya na nikasema sitaki kuwa na mwanamke tena.
Ikapita miaka kadhaa nikasikia jamaa aliyekuwa amemuoa mke wangu amefariki, nikamfata mke wangu na kumwambia kama hatojali anisamehe turudiane maisha yaendelee ili tuweze kulea watoto wetu pamoja. Kwa shingo upande mke alinielewa ila akasema kwa sababu ya watoto amekubali vinginevyo asingekubali. Maisha yakaanza tena upya kwa kweli safari hii nilimpenda japo sikuwa na kipato cha kutosha. Ufundi baiskeli ulinipa pesa ya kula tu nayo siyo ya uhakika lakini maisha yalikuwa ya furaha.
Mke wangu alipata ujauzito, hiyo ilimsumbua sana maana homa ya hapa na pale zilikuwa hazikatiki. Tulihangaika hivyo hivyo mpaka akajifungua. Alipojifungua akagundulika ana VVU. Nilijiuliza sana UKIMWI umetokea wapi nani kauleta ni mimi au mke wangu? Kumbe yule jamaa aliyemuoa alikuwa HIV+ na ndiye aliyemwambukiza hayo yote alikuwa anayajua lakini hakuniambia chochote. Sijui virusi vilikuwa na nguvu gani alikonda ghafla mpaka nywele zikawa nyepesi sana. Nikaambiwa nami nikapime ili nijue hali yangu nikaenda, sikuamini macho na masikio yangu kuona na kuambiwa kuwa nina HIV+. Nilimlaumu mke wangu lakini naye akanilaumu mimi ndiyo chanzo kama nisingemwacha asingehangaika namna ile. Aliamua kuolewa kwa sababu aliamini siwezi kumrudia tena kutokana na jinsi nilivyokuwa namtolea maneno makali tukionana. Wakati anaolewa hakujua kama huyo jamaa ni mwathirika mpaka alipougua sana na kwenda kupima.
Baada ya miezi 11 tangu ajifungue mke wangu alifariki akaniachia mtoto mdogo wa miezi 11. Nilishindwa kumlea peke yangu maana watoto wangu wawili wote walikuwa wa kike waliolewa wakiwa na umri mdogo labda sababu ya shida za nyumbani walichoka wakaona bora waolewe. Mwanangu mdogo ni wa kiume nilishindwa kukaa nae nikampeleka kwa ndugu yangu ambayo ni kaka akakae na watoto wengine wa kaka.
Kwa sasa nipo natumia dozi ya HIV na maisha bado ni magumu sana.
Najuta kwa niliyoyafanya kwa sababu nisingefanya ujinga familia yangu ingekuwa inaishi maisha mazuri hata pesa nilizopata zingetumiwa na familia yangu zikaisha zote bado furaha ya mke na watoto wangu isingepotea.
Nawaomba wanaume wenzangu ukipata pesa usimsahahu mke wako aliyekuzalia watoto na kudanganywa na vimada ambavyo kazi yao ni pesa kwanza. Ukimaliza pesa wanakufukuza.
Najuta Najuta Najuta

Mwisho wa kunukuu
 
........ Inaendelea
Baada ya kuambiwa niondoke nilienda kwa mwenyekiti wa mtaa kushtaki kuwa nafukuzwa na mke wangu na nikamweleza kila kitu kama nilivyoeleza sehemu iliyopita. Mwalimu akaitwa akaulizwa kwa nini anafanya vile akasema kwa sababu ni kwake na mimi nilikaribishwa tu pale kama mchepuko. Mwenyekiti nilimweleza mpaka nilivyokuwa namwachia pesa zote ninazozipata kazini, niliulizwa kama nina ushahidi wowote nikawa sina, yule mwanamke akashinda nikaondoka.
Baada ya kuondoka pale nikawa sina pa kwenda ndugu zangu wamenitenga na marafiki pia nikawa mtu wa kuhangaika. Ndipo nikapata wazo la kumtafuta mke wangu sikujua ameenda wapi. Baadae nikaambiwa alienda Bariadi nyumbani kwa wazazi wake, kwa kuwa nilikuwa napajua nikaenda mpaka ukweni sina mbele wala nyuma. Baba mkwe aliponiona hakutaka hata salamu yangu, nilipomsalimia kabla hajajibu aliniuliza nimefata nini? Nikamwambia nimemfata mke wangu. Nikajibiwa hapa mke hayupo ameolewa na sijui ameolewa wapi, alishindwa kukaa nasi sababu ya ugumu wa maisha na kutunza watoto ilikuwa kazi ngumu kwake na sisi ni wazee hatuwezi kumsaidia kwa chochote hivyo aliamua kuolewa kupunguza ugumu wa maisha. Na watoto wako anao wanalelewa na baba wa kambo. Nilisikitika sana hasa nikikumbuka wanangu sijawatunza inavyotakiwa na uwezo huo nilikuwa nao. Leo nimeenda nikiwa mikono mitupu watanielewa kweli? Niajipiga konde moyo nikasema liwalo na liwe naenda kumtafuta mke wangu huko alikoolewa angalau niwachukue wanangu hata kama yeye nikimwacha itakuwa sawa.
Nikaanza kumtafuta bahati nzuri nilimpata nikaonana nae. Kwanza nilianza kwenda kwa siri mumewe akiwa hayupo ndiyo naenda baadae ilibidi mumewe ajue kuwa mimi ndio baba wa watoto, na alipojua hakuwa na shida yoyote aliniambia hawa wanao mimi sina shida unaweza kuwachukua au kuwaacha wakae na mama yao. Nikajisemea moyoni nikiwachukua nitawapeleka wapi sina pa kuishi naishi kama mkimbizi popote kambi, wakati mwingine naenda stendi najifanya nasafiri nalala pale asubuhi naondoka kuzurula. Niliamua kuwaacha wakae na mama yao nikawaambia naenda nyumbani nikirudi nitawachukua. Walifurahi kumuona baba yao ambao ni kama miaka mitatu nilikuwa sijawaona.
Niliondoka lakini nikiwa sina furaha moyoni, nilirudi nyumbani nikaanza maisha ya kubangaiza. Nikawa fundi baiskeli kuziba pancha na matengenezo mengine ya baiskeli. Nikasahau kuhusu watoto nikaanza maisha upya na nikasema sitaki kuwa na mwanamke tena.
Ikapita miaka kadhaa nikasikia jamaa aliyekuwa amemuoa mke wangu amefariki, nikamfata mke wangu na kumwambia kama hatojali anisamehe turudiane maisha yaendelee ili tuweze kulea watoto wetu pamoja. Kwa shingo upande mke alinielewa ila akasema kwa sababu ya watoto amekubali vinginevyo asingekubali. Maisha yakaanza tena upya kwa kweli safari hii nilimpenda japo sikuwa na kipato cha kutosha. Ufundi baiskeli ulinipa pesa ya kula tu nayo siyo ya uhakika lakini maisha yalikuwa ya furaha.
Mke wangu alipata ujauzito, hiyo ilimsumbua sana maana homa ya hapa na pale zilikuwa hazikatiki. Tulihangaika hivyo hivyo mpaka akajifungua. Alipojifungua akagundulika ana VVU. Nilijiuliza sana UKIMWI umetokea wapi nani kauleta ni mimi au mke wangu? Kumbe yule jamaa aliyemuoa alikuwa HIV+ na ndiye aliyemwambukiza hayo yote alikuwa anayajua lakini hakuniambia chochote. Sijui virusi vilikuwa na nguvu gani alikonda ghafla mpaka nywele zikawa nyepesi sana. Nikaambiwa nami nikapime ili nijue hali yangu nikaenda, sikuamini macho na masikio yangu kuona na kuambiwa kuwa nina HIV+. Nilimlaumu mke wangu lakini naye akanilaumu mimi ndiyo chanzo kama nisingemwacha asingehangaika namna ile. Aliamua kuolewa kwa sababu aliamini siwezi kumrudia tena kutokana na jinsi nilivyokuwa namtolea maneno makali tukionana. Wakati anaolewa hakujua kama huyo jamaa ni mwathirika mpaka alipougua sana na kwenda kupima.
Baada ya miezi 11 tangu ajifungue mke wangu alifariki akaniachia mtoto mdogo wa miezi 11. Nilishindwa kumlea peke yangu maana watoto wangu wawili wote walikuwa wa kike waliolewa wakiwa na umri mdogo labda sababu ya shida za nyumbani walichoka wakaona bora waolewe. Mwanangu mdogo ni wa kiume nilishindwa kukaa nae nikampeleka kwa ndugu yangu ambayo ni kaka akakae na watoto wengine wa kaka.
Kwa sasa nipo natumia dozi ya HIV na maisha bado ni magumu sana.
Najuta kwa niliyoyafanya kwa sababu nisingefanya ujinga familia yangu ingekuwa inaishi maisha mazuri hata pesa nilizopata zingetumiwa na familia yangu zikaisha zote bado furaha ya mke na watoto wangu isingepotea.
Nawaomba wanaume wenzangu ukipata pesa usimsahahu mke wako aliyekuzalia watoto na kudanganywa na vimada ambavyo kazi yao ni pesa kwanza. Ukimaliza pesa wanakufukuza.
Najuta Najuta Najuta
Mbona hujamalizia kuwa kwa sasa umekufa?
 
Back
Top Bottom