Dr leader
JF-Expert Member
- Jun 28, 2016
- 1,041
- 1,294
MKE WANGU KAOLEWA
Namuombea laana, yeye na kizazi chake
Asipate cha maana, yeye na wazazi wake
Naamba kwa maulana, kumhusu mja wake
Mke wangu kaolewa
Nilifanya kila hali, wao wapate amani
Haramu au halali, chakula kiwe tumboni
Kupata sio sahali, hakuridhika mwandani
Mke wangu kaolewa
Bora angeniarifu, taraka yake nimpe
Hilo ameligharifu, hata nguo nisimpe
Hatukuwa na khirafu, tuligandana ja kupe
Mke wangu kaolewa
Kanitumia barua, hana haja ya taraka
Mimi ndo nitaamua, taraka au baraka
Sisemi nitamuua, ila hatapata faka
Mke wangu kaolewa
Na yule Shekhe kuwadi , aliyepewa utamu
Ndoa yenye uhasidi, kawabiriki, karamu
kabla siku ya ahadi, nitamtia hatamu
Mke wangu kaolewa.
✍️Abuuabdillah
Namuombea laana, yeye na kizazi chake
Asipate cha maana, yeye na wazazi wake
Naamba kwa maulana, kumhusu mja wake
Mke wangu kaolewa
Nilifanya kila hali, wao wapate amani
Haramu au halali, chakula kiwe tumboni
Kupata sio sahali, hakuridhika mwandani
Mke wangu kaolewa
Bora angeniarifu, taraka yake nimpe
Hilo ameligharifu, hata nguo nisimpe
Hatukuwa na khirafu, tuligandana ja kupe
Mke wangu kaolewa
Kanitumia barua, hana haja ya taraka
Mimi ndo nitaamua, taraka au baraka
Sisemi nitamuua, ila hatapata faka
Mke wangu kaolewa
Na yule Shekhe kuwadi , aliyepewa utamu
Ndoa yenye uhasidi, kawabiriki, karamu
kabla siku ya ahadi, nitamtia hatamu
Mke wangu kaolewa.
✍️Abuuabdillah