Mke wangu kanitenda, naomba ushauri

Mke wangu kanitenda, naomba ushauri

kimacho

Member
Joined
Feb 10, 2016
Posts
71
Reaction score
83
Miaka 13 iliyopita nilikuwa na mahusiano na Dada mmoja ambaye Leo hii ndio mke wangu lkn kabla sijamuoa tulipata mtoto mmoja kipindi napanga tufunge ndoa.

Ndugu zangu wakanitonya kuwa huyu wife anatoka na mtoto Wa Shangazi yangu na huyo first born wangu ni mtoto Wa huyo jamaa na mtoto wa yule ndugu yangu wanafana na first born wangu ktk kuchunguza sikujua ukweli nikapotezea nikaoa mpka sasa tunawatoto wawili huyu Wa sasa ni mm mwenyewe.

Tatizo limeanza nililonalo ambalo naomba mnishauli ni kuwa miezi miwili iliyopita nilisafiri kikazi wkt nipo mkoani wife alinipigia cm kuwa yule ndugu yangu kuna mzigo anamletea nikamwambia poa sasa nikiwa airport kuna jamaa yangu akanambia kamuona wife yupo maeneo usiku Wa sa5 na jamaa anamjua wife vizuri hawezi kumfananisha sikutaka kumpigia cm nilivyoludi dar nikamuuliza akabisha.

Nilipochukua cm yake nikakuta mwasiliano na yule ndugu yangu ambaye niliambiwa jamaa anamtafuna na hata first born wangu ni wake cm kama 8 za kufatana kumhoji kasema jamaa alipiga iliampe ulemzigo alikuwa anamuelekeza kuna mtu kampa amletee wife machale yakanicheza nikafanya nachokijua nikapata ukweli Wa Yale maongezi kumbe jamaa wanaelekezana na wife waonane wapi.

Then wanapnga jamaa aseme hayupo dar na mbaya jamaa kumbe anaiita mm taahira ananipigia cm ananiuliza akijua Niko wapi wanapanga na wife jinsi ya kunidanganya sababu huyu jamaa anaishi Arusha niliwaita wazazi wangu na wakwake mpka kwenye kikao wife aliapa miungu kuwa hakutoka nilipokuja kuwasikilizisha Yale maongezi wote walikaa kimya mpaka wife akaishiwa LA kuongea.

Mzee nikatoa talaka2 lkn wife na mamaangu ni marafiki kwahiyo mama kamchukua mkwewe anakaa nae mpaka EDA iishe waislamu ukiacha ndani ya miezi 3 unaweza mludia mkeo naombeni ushauli.

Mwakani nampango Wa kwenda kuishi Europe kwa muda sasa nawaza huyu mtu nikimludia nikamuacha home sindio itakuwa nimempa Uhuru Wa kufanya yake bora kila mtu aangalie maisha yake na hata nikiwa Europe niishi bila presha ya mke huku nyumbani tusaidiane mawazo wakuu kichwa kinanivuluga maana cjui nichukue uamuzi gani
 
Ulifanya mistake na sasahiv unaendelea kufanya mistake,piga chini mkuu chukua maamuzi magumu,usiangalie uhusiano uliopo kati ya wife na mother coz wote ni wanawake,pia usiangalie umegharamia kiasi gani,ukishindwa kupiga chin Basi kubali kugongewa na huyo ndugu yako
 
Achana na huyo Malaya Lea "mtoto wako" huyo mwengine DNA inahitajika japo hapa tz wanatoa majibu ya uongo kwa ustawi wa mtoto asipokuwa wako mpe huyo mwanamke mtoto wake muondoe kwa mama ako baki Lea mwanao



Unaonekana we ni dhaifu sana hata hilo ni lakuomba ushauri mwanaume anaongea Mara moja
 
Pole. Kuna mengi ya kufanya, mosi achana naye atakuumiza kichwa wakati yeye anakula raha. Pili, tafuta mke wa pili oa, tatu, lea watoto wako achana na habari za kuoa halafu tafuta 'girlfriend' mkihitilafiana hakuna 'commitment' yoyote. Nne, punguza mahaba kwa huyo 'the so called mkeo' weka passion yako kwenye ishu nyingine.

Pole sana na yatapita!
 
Kwa jinsi ulivyoandika ni wazi bado unampenda mkeo. Pia ni wazi ulishajua ukweli toka tetesi zilipoanza toka kwa ndugu zako lakini ukaamua kujipa moyo kuwa si kweli. Kitendo cha kutoa talaka 2 ilhali una kila ithibati kuwa anazini tena na binamu yako ni ushahidi tosha kuwa unampenda mkeo.
Mwenye hulka yake habadiliki mkuu na hapo mlipofikia hamna ndoa tena zaidi ya shaka. Hata kama akijirekebisha tabia kitendo cha yeye hata kutopokea simu utahisi yupo na mtu mwingine. Msingi wa ndoa kabla hata ya mapenzi ni kuaminiana. Mshapoteza imani kwenye mahusiano yenu hivyo hapo hakuna tena ndoa.
Piga moyo konde, muache moja kwa moja na uanze maisha mapya. Huyo mwanamke hana mapenzi na wewe na wala hakuheshimu. Kitendo cha kuitwa tahira na ndugu yako (bwana'ake) ni ishara kuwa hakuthamini hata chembe na kwao wewe ni kituko tu.
Mbali ya huyo mke hata mama yako japo ni mzazi wako nae si mtu mzuri kama anaweza kumhifadhi mtu aliyekudhalilisha ina maanisha kuna walakini juu ya upendo wake kwako. Wewe ni mwanaume inabidi usimame imara katika kutetea uanaume wako. Kuna maisha zaidi ya huyo mwanamke na kama usemavyo una mpango wa kwenda kuishi Europe, hiyo ndio nafasi yako ya kwenda kuanza upya.
Mwisho wa siku hapa wote ni wachangiaji tu, mwenye maamuzi ya mwisho ni wewe. Pole ndugu.
 
Mkuu, yaani hadi umefikia kupata ushahidi then bado unakuja kutuomba ushauri...!!??
Anyway, ungekuwa karibu na mimi ningekuchapa makofi ili akili ikukae sawa.
Na kwakuwa sina la kukushauri, naomba tu nikupongeze kwa kupata mafanikio ya kwenda kuishi Europe this coming year
 
upo kwenye uislam, na una ushahidi mke ni mzinzi! kwa nini unahofia kumuongezea talaka ili ziwe 3?

Nb. Fanya kile ambacho akili yako inakutuma na si moyo wako.
Huyu jamaa hata angemkuta mkewe ameukalia, bado angekuja kuomba ushauri hapa.
Ninacho kiona ni kwamba jamaa bado anampenda mkewe na anaonekana yupo tayari kumsamehe
 
Wanaume kweli tunapungua I see. Hivi kweli wewe una evidence kabisa kwamba 1. Mtoto mmoja sio wako. 2. Una uhakika anatafunwa na njemba ingine. Lakini bado unavumilia?. Basi katika vitu ambavyo ni rahisi kuachana na mwanamke ni mwanamke kuchepuka. Hivi mnakwama wapi? Acheni kupenda kiboya hivyo. Ushauri sasa. Nyie waislam mnatoa talaka 3?. Basi malizia leo hii talaka ya mwisho. Msahau kabisa. Tena wewe una bahati karibu unasafiri. Sasa unakwama kwama wapi?. Ukirudi kamata chombo kipya. Na wao utakuta wameoana. Wewe kazana kusaka hela
 
Miaka 13 iliyopita nilikuwa na mahusiano na Dada mmoja ambaye Leo hii ndio mke wangu lkn kabla sijamuoa tulipata mtoto mmoja kipindi napanga tufunge ndoa.

Ndugu zangu wakanitonya kuwa huyu wife anatoka na mtoto Wa Shangazi yangu na huyo first born wangu ni mtoto Wa huyo jamaa na mtoto wa yule ndugu yangu wanafana na first born wangu ktk kuchunguza sikujua ukweli nikapotezea nikaoa mpka sasa tunawatoto wawili huyu Wa sasa ni mm mwenyewe.

Tatizo limeanza nililonalo ambalo naomba mnishauli ni kuwa miezi miwili iliyopita nilisafiri kikazi wkt nipo mkoani wife alinipigia cm kuwa yule ndugu yangu kuna mzigo anamletea nikamwambia poa sasa nikiwa airport kuna jamaa yangu akanambia kamuona wife yupo maeneo usiku Wa sa5 na jamaa anamjua wife vizuri hawezi kumfananisha sikutaka kumpigia cm nilivyoludi dar nikamuuliza akabisha.

Nilipochukua cm yake nikakuta mwasiliano na yule ndugu yangu ambaye niliambiwa jamaa anamtafuna na hata first born wangu ni wake cm kama 8 za kufatana kumhoji kasema jamaa alipiga iliampe ulemzigo alikuwa anamuelekeza kuna mtu kampa amletee wife machale yakanicheza nikafanya nachokijua nikapata ukweli Wa Yale maongezi kumbe jamaa wanaelekezana na wife waonane wapi.

Then wanapnga jamaa aseme hayupo dar na mbaya jamaa kumbe anaiita mm taahira ananipigia cm ananiuliza akijua Niko wapi wanapanga na wife jinsi ya kunidanganya sababu huyu jamaa anaishi Arusha niliwaita wazazi wangu na wakwake mpka kwenye kikao wife aliapa miungu kuwa hakutoka nilipokuja kuwasikilizisha Yale maongezi wote walikaa kimya mpaka wife akaishiwa LA kuongea.

Mzee nikatoa talaka2 lkn wife na mamaangu ni marafiki kwahiyo mama kamchukua mkwewe anakaa nae mpaka EDA iishe waislamu ukiacha ndani ya miezi 3 unaweza mludia mkeo naombeni ushauli.

Mwakani nampango Wa kwenda kuishi Europe kwa muda sasa nawaza huyu mtu nikimludia nikamuacha home sindio itakuwa nimempa Uhuru Wa kufanya yake bora kila mtu aangalie maisha yake na hata nikiwa Europe niishi bila presha ya mke huku nyumbani tusaidiane mawazo wakuu kichwa kinanivuluga maana cjui nichukue uamuzi gani
Achana na habari za kuoa fanya vitu vingine
 
Back
Top Bottom