Mke wangu ananishangaza sana matendo yake...

Mke wangu ananishangaza sana matendo yake...

Sasa ulitaka mjadili then akuunge mkono kila kitu? Yeye katoa mtazamo wake. Wewe kubali kutokubaliana. Ukianza wasiwasi wa ajabu utaharibu mahusiano yako kwa sababu za kijinga.

By the way mnakaa mnabishana mambo ya Diamond mpaka unakua na wasiwasi??? This remind me miaka ya nyuma demu wangu alikua anampenda sana Drake mpaka akawa anajiita sijui nani Drake eti na mimi nikawa naona wivu[emoji3][emoji3] baadae nkaona ulikua utoto tu....

Sasa na nyie mnaweza kugombana kwa sababu za kitoto mno.

Umefunga ndoa ya kanisani au msikitini???
 
Kafanye DNA test,siku za mbeleni mtagombana anaeza jikuta analopoka kuwa mtoto si wako, SIJUK UTAJISKIAJE....mkuu wanawake wa Sasa hawana STARA...ohooo!
 
Sijui kwann wanaume siku hizi mnapenda kuchimbachimba vitu visivyonamaana ivi mwisho mnajitia wasiwasi kwenye maisha yenu ivi mnafikiri hao baba zetu waliishi namalaika wenzetu mwanamke ilikuwainatokea akazaa nje watu wanakaa wanazungumza yanaisha sasa wewe kaa mguu upande mwanamke akuhisi unamwanamke mwingine uone vumbi lake
 
Sioni kama tunafanana
Mara nyingine kufanana na mtoto ni mentality unayojijengea ukiwa unaimani tangu mwanzo ni wako.Sasa hivi kwa kauli za mkeo unahisi sio wako,ila inawezekana ni wako.Nakupa mfano ,watoto waliozaliwa leo hii kama 20 mloganzila wasipowekewa lebo wakawekwa chumba kimoja wote kila familia iambiwe wakachague mtoto wao, je wataweza?
 
Tuna mtoto wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi 3 , Tulibahatika kupata mtoto kabla ya kuoana yaani kipindi cha upenzi ndio kipindi ambacho alipata mimba na baadae akajifungua ndipo nikaamua nimsogeze tuwe familia moja....

Jambo linalo nishangaza sana ni kauli zake tata...kama mmnavyo jua kuwa mama diamond amesema ukweli kuwa diamond sio mtoto wa mzee abdul ..

Sisi tumekuwa na stori za kawaida zinazo husiana na tukio kubwa lililo fanywa na mama diamond
Kwenye stori tunazoziongelea mke wangu anasema kumpakazia mtoto mwanaume ni jambo la kawaida ....hili jambo amekuwa akilirudia mala kwa mala pia kuna wakati akasema mtoto anapewa Baba mwenye uwezo wa kulea haijalishi kama sio wakwake kikubwa ni mtoto aende mahali salama

Nikamuuliza kama utani vile "kama shida ni malezi ya mtoto kwanini mwanaume asiambiwe ukweli kwamba uyo mtoto sio wako ila nataka umlee " akanijibu hakuna mwanaume atakae kubali kabisa kwaiyo ni lazima ukweli ufichwe ili maisha yaendelee..

Sijamuonesha kuwa naanza kumuhisi vibaya ila kwakifupi anaonekana kuwatetea sana wanawake wanao wapakazia mwanaume watoto wasio wao ...

Ananifanya niache kujiamini juu ya huyu mtoto tulie nae na ananifanya nipunguze mapenzi kwa mtoto huyu....

Msaada wenu je ? Kuna uwezekano wa kupima DNA kwa siri bila yeye kutambua ..
No kupima dna mnapima nyie wote 3
 
Back
Top Bottom