Haya aendelee kumchamba huko kama itasaidia kuimarisha ndoa yake. Ni tabia ya ajabu imezuka na wenyewe wanaona ni sahihi kufanya hivyo kumbe hata hao unaowaandikia wanakuchoraKuna maneno yao wenyewe wanasema, kumchamba sijui...
Yaani kama ulikuwepo vile ndio hivyo hata dp huwa anarushaHata mimi mkewangu yupo hivyo, mkikosana tu status ya wasap na dp zinajaa vijembe. Nishampuuza. Hizo ni AKILI ndogo.
Mwanamke mwenye akili ndogo huwa yuko hivyo.
Kama anakuwekea wewe ,maanake ni kwamba anataka usome na uumie. USHAURI : Mwambie yaan simu cjui imeharibika,yaan sionagi status wala dp za wasap, halafu usiangalie uone kama ataweka
Wazee kwa vijana
wadada kwa wamama.
Jina la bwana lihimidiwe!
Kwa muda mrefu sana hili jambo huwa linatokea baadae linapotea kisha linajirudia tena!
Huyu wife wangu amekuwa akirusha vijembe sana huku whatsap status! Kwa uchunguzi nimegundua kila ikitokea tumepishana kidogo kauli haipiti dakika unakuta ameweka status whatsup:
Mara "USIZARAU DAFU EMBE TUNDA LA MSIMU", siku yingine utakuta "KIKIWA NDANI CHAKO KIKITOKA SIO CHAKO"
LIMEKUSHINDA LIMAO UNAFATA NDIMU"
"WE NI KONOKONO KAMA KONOKONO WENGINE"
"UKITAKA HALUA KUNDU PANUA"
Hizo baadhi ya vijembe ambavyo moja kwa moja najua vinanihusu mimi ni zaidi ya hapo nishamkanya kama anaona tofauti yoyote anieleze kuliko kuanika huko ili kila mtu ajue tumekosana lakini hasikii!
Nikaanza kufikiria niwe namjibu lakini haitakuwa fresh kidume kurushiana maneno mitandaoni. Yaani hata akinipigia simu bahati mbaya sijapokea nikija kuingia tu whatsapp nakuta "MBUZI KUWA NA NDEVU SIO NDIO UANAUME" au "MWANAUME BUKTA".
Kiukweli huwa inanikosesha amani maana kila nikimweleza polepole hanielewi hembu nisaidieni mawazo nifanyaje!
Mwanamke akigundua anachofanya kinakuumiza. Umekwisha !. Tena ukimuuliza kuhusu alichofanya anajua IMETICK ,atakusumbua wewe.Yaani kama ulikuwepo vile ndio hivyo hata dp huwa anarusha